yeye alieidhinisha kuuwa kwake yeye amebaki hai?Na hata MUNGU alibariki kifo chake
yeye alieidhinisha kuuwa kwake yeye amebaki hai?Na hata MUNGU alibariki kifo chake
Huyu Mwamwindi alizikwa wp? nataka nikaone Kaburi lake...... mtu madhubuti huyu
Siyo kweli! Mwamwindi aliua kwa vile alikuwa provoked na huyo RC. RC alimfuata shambani kwake akiwa anasimamia vibarua, shamba ambalo lilikuwa kubwa sana na wakati huo ndo siasa ya ujamaa na kujitegemea ilikuwa imeshika kasi, Mwamwindi wakawa wanamwona kama bepari fulani hivi. Maana jamaa alikuwa amejiimarisha sana katika maswala ya kilimo, ieleweke kwamba enzi hizo watu waliokuwa na combine harvester walikuwa wa kuhesabika na Mwamwindi akiwamo. RC alipofika shambani kwa Mhehe akawa anamchomachoma tumbo kwa fimbo yake (kama ya Nyerere) huku akisema hili tumbo lina mirija ya unyonyaji. Hapo hapo Mhehe akahamaki ndo akaenda kuchukua riffle yake na kummiminia risasi hapo hapo shambani. Wacha niishie hapo maana hadithi ya Mwamwindi ni ndefu sana! Wewe kijana wa jana nawe unajidai kutuletea hadithi ya Mwamwindi?
Kwani kwangu umeniona kuna mahali nimesema alinyang'anywa mke mdogo? Wacha upotoshaji mkuu!ulichoandika ni sawa na nilichoandika ni sawa pia!
lol!Nilitaka nishangae tangu lini Mwafrika akawa tayari kuuwa kwa ajili ya kutetea kile anachokiamini yaani itikadi? Sana sana ukisikia Mwafrika kaua ujue ni mapenzi tu hapo hamna kingine, ngono ndiyo namba moja!
Haswaaaaa! Natamani tuwe na akina Mwamwindi kama 1000 hivi tuone nini kitatokea!Kwa hiyo mwandindi alichokozwa kumbe ?
Nyakati ngumu hazipiti ila Watu wagumu wanapita.
R.I.P Mwamwindi hakika wewe ni shujaa wa aina yake.
hasira hasara!Na mimi ndivyo nilivyo adithiwa, wa lisema siku yenyewe ilikuwa ni Chrismas kama nakumbuka vizuri.
Inaelekea Dk. Kleruu (RIP) alipata taarifa kuhusu Mwamwindi kuwepo shambani kwake akiwa na wafanyakazi wake - nadhani mwaka huo ndio itikadi za ujamaa zilikuwa zimepamba moto nchini, mabepari wakawa wanafananishwa na wanyama,wakaitwa wanyonyaji, wanaibwa kwa nyimbo za kejeri na chuki - yaani wananchi walikuwa primed kuwaona mabepari kama ni wabaya kuliko wakoloni.
Misimamo ya kuchukia Ubepari nchini ilikuwa ina walakini sana, kuna baadhi ya wananchi waliokuwa na uwezo kifedha walipata wakati ngumu sana kwa kunyaganywa mali zao walizo chuma kwa jasho lao!!
Atittude zilizokuwa zimejengeka wakati huo ndizo zilimpa jeuri Dk.Kleruu kwenda kumudhihaki/dhalilisha Mr.Mwamwindi skiwa shambani kwake - kisa? Mwamwindi ni bepari, eye witness walisema walimuona Dk.Kleruu ameshikilia kifimbo akikisukuma sukuma kwenye tumbo la Mwamwindi - hakuna mwanamume worthy his salt angeweza kuvumilia provocation ya kiwango hicho - alicho kosea Mwamwindi ni kule kwenda kuchukua Rifle kutoka nyumbani kwake na kurudi shambani kumpiga risasi Dk.Kleruu - sasa time lag ya kutoka shambani kwenda nyumbani kuchukua bunduki na kurudi tena shambani hasira zilipashwa kuwa zimepungua ndio maana mahakama ilimuhukumu kunyongwa kutokana na kuonekana kwamba iliuua kwa kukusudia "murder case"
Kama Mwamwindi angekuwa na bunduki shambani alafu Dk.Kleruu akaja akamu-provoke hapo angehukumiwa kuua bila ya kukusudia akafungwa kwa muda.
watu wana hasira,sijui kwaniniNinaposoma kauli za wadau hapa ninapatwa na hofu sana. Ndani ya mioyo ya watu yapo mengi sana. Ukipewa uwezo wa kuyaona unaweza bakia umejifungia ndani..
Kwann ? sasa ww alitaka akubali kunyanyashwa shambani kwake ?hasira hasara!
lakini kufa ni lazima au unasemaje ?ni heri mbwa anayeishi, kuliko simba aliyekufa!
Mwamwindi alikuwa kichaa tu, ukoo wao una asili ya uchizi, wala sio wa kusifiwa.Angekuwa Mwamwindi police wangekuta bucha ya mgambo huko mashambani
Haya mambo ya Mwandindi kuchukuliwa mke wake mara sijui ikawaje au ndio mdada Lady Jay D ameii
Chukua hii Ndi ndi ndi toka kwa Mwamwindi sijui Mwandindi ikimaanisha ukicheza na ndindindi ya mtu anakusepesha kama Dr.Kileruu
Kwani kwangu umeniona kuna mahali nimesema alinyang'anywa mke mdogo? Wacha upotoshaji mkuu!
Wewe ndo unayepotosha. Toka lini mkuu wa mkoa akaenda oparesheni peke yake, na gari la ofisi, bila walinzi hata dereva!!!!Acha kupotosha umma.
Ilikuweje aende peke yake bila mtu mwingine yeyote, dereva, askari, mkuu wa Wilaya.Dr.Kleruu alipigwa Risasi Shambani kwa Mwamwindi akiwa Kaenda kumzuia asilime Mazao anayoyataka badala yake alime zao la biashara kwa Gharama zake halafu akawauzie vyama vya ushirika kwa bei waliyojipangia serikali halafu watalipa siku wakijiskia, hata Risasi alipigiwa shambani sio gesti wala kitandani.
Enzi zile ni enzi za Propaganda kama uliweza kuaminishwa Iddi Amin anakula watu na wewe ukaamini huwezi kuacha kuamini uongo eti kisa Kilikuwa uzinzi!