Nyumba aliyoishi RC wa Iringa Dr. Kleruu kabla ya kuuawa na Said Mwamwindi

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,353
Hii ni nyumba ya kihistoria iliyojengwa na muingereza ambayo baada Tanzania kupata uhuru nyumba hiyo ilianza kutumiwa na Mkuu wa mkoa ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mmoja wa wasomi wachache waliokuwa Tanzania ndugu Dr. Wilbert Kleruu.

Kwa wale wanaoijua historia na wale waliosoma sheria jina Said Mwamwindi na Dr. Kleruu (Said Mwamwindi v R (1972) HCD 212 ) sio majina mageni kwao.Pia kuna chuo cha Ualimu kimejengwa kuenzi kazi iliyotukuka ya Dr. Kleruu.

Kwa bahati mbaya nyumba hii haijatumiwa tena na wakuu wa mikoa waliofuata baada ya kifo cha Dr. Kleruu kutokana na kile kinachosemekana kuwa uoga.Nyumba hii imekuwa ikitumiwa na Jeshi.

12651002_10207312222856592_2445936983497422551_n.jpg

Mbaraka Mwinshehe naye amepata kumuimba dr. Kleruu
 
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!
 
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!


Angekuwa Mwamwindi police wangekuta bucha ya mgambo huko mashambani
 
Dr. Kleruu wapo wengi sana Nyakati hizi ila Majasiri kama akina Said Mwamwindi hawapo!!
Huyu Mkulima alimtandika Risasi RC akamtia kwny Trekta lake akampeleka kwa RPC akamwambia nimewaletea Mzoga Wenu.
Juzi kati hapa Mgambo tu wa TANAPA wameharibu mashamba ya Mahindi zaid ya heka 400 huko Mbeya kisa wamelima kwenye Hifadhi, halafu wanakijiji wanakimbilia ITV !!!

duh, hairuhusiwi kulima kwenye hifadhi mkuu, ulitaka wafanyeje
 
Nilitaka nishangae tangu lini Mwafrika akawa tayari kuuwa kwa ajili ya kutetea kile anachokiamini yaani itikadi? Sana sana ukisikia Mwafrika kaua ujue ni mapenzi tu hapo hamna kingine, ngono ndiyo namba moja!
siyo ngono tu hata msosi. Cheseya niga wewe kwenye menu!

Na ukiona mwafrika ameua ujue LAZIMA kwanza kajaribu kumroga marehem ikashindikana. Mwafrika akitaka kulipiza kisasi LAZIMA aanze kwa kukupiga juju ikishindikana ndio anatumia njia nyingine
 
Nilitaka nishangae tangu lini Mwafrika akawa tayari kuuwa kwa ajili ya kutetea kile anachokiamini yaani itikadi? Sana sana ukisikia Mwafrika kaua ujue ni mapenzi tu hapo hamna kingine, ngono ndiyo namba moja!

Toka enzi za Mwamwindi mpaka leo hii hadithi bado ile ile...we have not changed even an inch.

Mhehe usicheze na mke yake
 
hapana mwamindi alikua anapinga kuchukuliwa mke wake mdogo na Dr. Kleruu

Dr.Kleruu alipigwa Risasi Shambani kwa Mwamwindi akiwa Kaenda kumzuia asilime Mazao anayoyataka badala yake alime zao la biashara kwa Gharama zake halafu akawauzie vyama vya ushirika kwa bei waliyojipangia serikali halafu watalipa siku wakijiskia, hata Risasi alipigiwa shambani sio gesti wala kitandani.
Enzi zile ni enzi za Propaganda kama uliweza kuaminishwa Iddi Amin anakula watu na wewe ukaamini huwezi kuacha kuamini uongo eti kisa Kilikuwa uzinzi!
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom