North Mara: Kashfa ya maji ya sumu toka mgodini!

Exuper Kachenje na Claud Mshana

SERIKALI imesema kuwa, wamiliki wa mgodi wa North Mara walitoa maelezo ya uongo dhidi ya malalamiko ya wananchi kuwa mgodi huo unatiririsha maji ya sumu yaliyosababisha vifo vya watu, wanyama na kuathiri mazingira.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Balozi Khamis Kagasheki alisema hayo juzi baada ya kutembelea mgodi huo kwa maagizo ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili kujionea hali halisi na kujua ukweli wa mambo.

Wananchi wa maeneo yanayozunguka mgodi huo wamekuwa wakieleza kuwa kumekuwepo na sumu inayovuja na kuingia kwenye Mto Tigite na kusababisha vifo vya viumbe walio kwenye mto huo, wanyama wao waliokunywa maji hayo na kukauka kwa mimea iliyo kandokando ya mto huo unaotegemewa na vijiji vitatu.

Picha za magazeti na televisheni zimekuwa zikionyesha watu walioathirika vibaya kwenye ngozi na ambao walieleza kuwa walipata athari hizo baada ya kutumia maji ya mto huo, huku ikielezwa kuwa ng'ombe zaidi ya 200 wamekufa baada ya kunywa maji hayo.

Hata hivyo, Barrick ilikanusha madai hayo na kusema kuwa, uchunguzi uliofanywa na mgodi huo kwa kushirikiana na watendaji wa serikali pamoja na mganga wa wilaya hiyo ulionyesha hakuna ukweli wowote katika malalamiko ya wananchi wa eneo hilo.

Hata hivyo, Balozi Kagasheki aliiambia TBC1 kuwa katika ziara yake kwenye mgodi huo unaomilikiwa na Barrick Gold ya Canada amebaini kuwepo na athari kubwa kwa viumbe na mazingira.

Alisema awali alitembezwa na uongozi wa Barrick kwenye maeneo kadhaa na ikaonekana kuwa hakuna tatizo, lakini alitokea mwananchi mmoja aliyemwelezea kuwa ni msamaria mwema ambaye alimshika mkono na kumwambia kuwa maeneo aliyoonyeshwa sio ambayo yanalalamikiwa na kumpeleka kwenye tatizo halisi.

Alisema alimfuata msamaria huyo na kuonyeshwa hali halisi ambayo waziri huyo aliielezea kuwa "ni mbaya na ya kusikitisha" na akasema anashangazwa na kitendo cha uongozi wa mgodi huo kudanganya.

"Nasikitika sana uongozi wa mgodi kunidanganya. Niliyoyaona nitayapeleka kwa waziri mkuu... kwa kweli si nzuri, itabidi nifikishe ripoti kwa waziri mkuu," alisema naibu waziri huyo akionekana kukasirika.

Kagasheki, aliyekuwa akihojiwa na kituo cha televisheni cha TBC1, alisema inasikitisha zaidi kwa kuwa wakati mwingine inakuwa vigumu kuielewa serikali kwa matukio kama hayo na mimi kuwa naibu waziri wa wizara hiyo inayohusika na usalama wa watu na mali zao, atatekeleza wajibu wake katika kuhakikisha usalama wa wakazi wa eneo linalozunguka mgodi huo.

Katika wiki za hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti kutokea kwa vifo vya watu zaidi ya 21 na ng'ombe 200 huku wengine wakiathirika kutokana na kunywa maji ya Mto Tigithe unaopita katika Kata ya Kibasuka wilayani Tarime Mkoa wa Mara.

Diwani wa kata hiyo, ambaye aliibua malalamiko hayo, anashikiliwa na polisi na amefunguliwa mashtaka akidaiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu vifo hivyo.

Wiki iliyopita Jumuiya ya Kikristo Tanzania pamoja wanaharakati wengine wa mazingira na haki za binadamu, walitoa tamko kutaka wahusika hao wachukuliwe hatua, ikiwa ni pamoja na kumtaka waziri mwenye dhamana ya mazingira, Batilda Buriani ajiuzulu kutokana na kashfa hiyo.

Walisema kuwa, upo ushahidi wa kutosha kuwa watu walikufa kutokana na kunywa maji ya sumu na kwamba wapo tayari kuchukuliwa hatua ikiwemo kufikishwa mahakamani iwapo jambo hilo halina ukweli ambapo pia walitaka kuundwa kwa tume huru kuchunguza kashfa hiyo.

Nao Wabunge waliochangia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Batilda Buriani walitaka serikali kulichukulia suala la Mgodi wa North Mara kwa uzito unaostahili na kuunda tume kuchunguza madhara yanayodaiwa kutokea kwa wananchi waliotumia maji yenye kemikali katika Mto Tigite.

Mbunge wa Tarime (Chadema), Charles Mwera alisema serikali inapaswa kuwawajibisha wote waliopima maji hayo na kusema kuwa, hayana kemikali hatari na kuongeza kuwa waziri atakapokuja kujibu hoja aeleze amefanya ziara ngapi katika maeneo hayo.

Mto huo wa Tigite unategemewa na zaidi ya familia 2,534 walio katika vijiji vya Kewanja, Nyangoto na Matongo ambazo zinaathirika moja kwa moja. Pia vijiji vya Wegita, Nyakurungu na Nyarwana wanaathirika na mto huo ambao unaungana na Mto Timbe unaopita kijiji cha Mtongo na baadaye kuelekea Ziwa Victoria.

Tangu mapema mwezi Mei, wakazi wa vijiji hivyo wamekuwa wakilalamika kuwa kumekuwepo na uvujaji wa takataka zenye sumu kutoka mgodi huo na kwamba mifugo yao ilifariki kutokana na kunywa maji ya mto huo. Pia walidai mimea iliyo pembezoni mwa mto huo inakauka na kwamba waliona samaki wengi wakiwa wamekufa.

Barrick, ambayo inadai kuwa mgodi huo hautoi kabisa maji machafu yenye sumu, imeeleza kuwa kuvuja kwa takataka hizo zenye sumu kulitokana na vitendo vya wakazi wa vijiji hivyo kuharibu mabomba kwa lengo la kuhujumu.

Mgodi huo umekuwa na matatizo na wananchi wa maeneo yanayouzunguka tangu ulipoanzishwa, baadhi yakitokana na wananchi kutoridhika na fidia waliyopewa kwa kuhamishwa eneo hilo, uchafuzi wa mazingira na mapigano ya mara kwa mara yanayotokana na wananchi kuvamia mgodini kila wakati miamba inapolipuliwa.


Source: Mwananchi

Hivi Kikwete anasoma au anapata habari kama hizi? na kama hapati au whatever kisingizio atakachotoa kuhusiana na hili, je anaendelea kujiita kuwa ni Raisi wa Tanzania na kamanda mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama wa watanzania wote (ikiwemo hawa wa North Mara) ?
 
Mods unganisheni hizi zote...thread na ile ya mwanakijiji tuwe tunachaningia pamoja...
Nmara,Nmara,Nmara,ohhhhhhhh

Sidhani kama kuna tatizo lolote hii ikiwa hapa peke yake watu wakachangia pia. Wanaochafua mazingira huko North Mara lazima waanikwe vya kutosha hapa jamvini.
 
Kiwango cha Usaidi ni (Cynide)wanayo sema.Hili Jambo limekaaa kisiasa zaidi ya ukweli wa kawaida....Ukiangalia hiyo report ni ya kijiji kilichomba mbali na mgodi wa dhahabu wa North Mara ambao ni nyamwanga.Yes the river falls zinakwaenda mpaka uko na wao huja kulishia ng'ombe pande hizo?Kwanini watu wa nyamongo 2Km from mine site and 3-4 Km kutoka maji yenye cynide yalipo wasiathirike all that long?

Kuna kitu kinaitwa Rom pad 7km kutoka mgodi uliko lakini karibu na mashimo zinakichimbwa dhahabu ambako ndio maji hayo yapo....kila mgodi maji hayo yapo.Na yamehifadhiwa kwa ungalifu wa hali ya juu na kuwa monotored every day.Hatujasikia malalamiko haya...RESOLUTE NZEGA,BULYANHULU KAHAMA,GEITA MWANZA,TULAWAKA BIHARAMULO,WALA BUZWAGI KAHAMA.Ni Tarime tu!!!Hatujiulizi ni kwanini?Ina maana wa tarime tu barrick inaamua kuyamwaga kwa makusudi?Kwa mtizamo wa kawaida si kweli....

Ukweli ni kwamba intruders(wez wa mawe ya dhahabu)baada ya shimo moja kusimama uchimbaji wakawa hawana cha kufanya kwa kuwa wanategemea production iwepo ili na wenyewe waweze kupata mawe yenye dhahabu..sasa baada ya kukosa..wakaamua kutafuta kitu mbadala cha kuiba wapate kipato...see sasa wameiba carpet hilo a linalo zuia maji yasiingie ardhini na kuwa contaminated na maji salama yanayo tumika kwa matumizi ya binadamu.

Maji yakatiririka kwenda mtoni ng'ombe wakanywa.Binadamu kwa kweli sina uhakika....kwangu mie sijaona muathirika hata mmoja zaidi ya meneno ya mwenyekiti huyu....je hilo ni tatizo la nani?Wananchi ? au Barrick?Tungalie katika upanda wake hata hao walio iba....au kukata hilo carpet ni wananchi wa mbali na eneo la mgodi..hii naweza sema ni ukosefu wa uelewa..kwani wakijiji wa nyamongo wao hawajawahi fanya makosa hayo.Wanajua madhara.

Wanaposema kiwango kidogo cha Usaidi(cynide)ni kweli kwa kuwa cynide nyingi inakuwa imesha tumika kwa kazi yake...hicho kinachopelekwa uko ni kwa sababu ya kuhifadhiwa na kuendelea kuwa treated mpaka itakapo fika 0.00%.Na hii hufanyika kwa kuongeza maji mengi.

Ukisikia spinning ya hali ya juu ambayo bado imeangukia pua basi hapa kwa maelezo haya (utetezi wa wachafuzi wa mazingira) ni makao makuu.
 
Serikali kiziwi, yenye upofu na ububu katika masuala yanayohusu wananchi wake! Nifahamuvyo mimi, mkataba wa wananchi na watawala wao ni kwamba serikali na dola yake iwalinde wananchi in return of the priveldge wanazopata. Tanzania yetu ulafi umeongoza. Serikali haina cha kusaidia. Kila mtu afe kivyake. Maajabu ni kwamba kuna mtu bado anakwenda kwenye chumba cha kupiga na kura na kusema next time ccm, Lord have mercy!
 
duh! Ishu ni kwamba wamedanganya serikali na imeumiza wananchi. Kazi ya serikali ni kulinda wananchi. Wapelekwe mahakamani na walipe fidia...kila senti. Ikiwezekana wafilisiwe. Tunakuwa kama jalala, kazi kuleta kampuni zilizooza kufanya kazi Tanzania. HATUTAKI!
Alafu...Wewe ukinunua gari bovu alafu ukaenda kugonga mtu utasema kosa sio lako? U do indeed think differently from others!

nimeipenda sana hiyo in red, inawezekana huyu Buswelu ndiye Dr Burian mwenyewe au mtu wa karibu naye au ndiye aliyeaandaa report iliyosomwa na bi burian mjengoni...inauma sana kama mtanzania anaweza akasema kodi za serikali ni muhimu kuliko maisha ya watanzania!!we need people to think differently in a positive way siyo hata matope unayanadi ni different thinking while what he is saying/writing does not involve thinking at all...in short Buswelu did not think,he/she just wrote.
 
MKUU wa Wilaya ya Tarime, Frank Uhahula amesema kwamba uongozi wa Kampuni ya Barrick inayochimba mgodi wa dhahadu wa North Mara haukudanganya kuwaonyesha maeneo yanayotiririsha maji yanayodaiwa kuwa na ‘sumu’ kwenye Mto Tigithe.

Kauli hiyo ya Uhahula inaelekea kupingana na aliyotoa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamisi Kagasheki alipofanya ziara kwenye mgodi huo kupata uthibitisho wa maafa makubwa yanayodaiwa kusababishwa na sumu inayotiririka hadi kwenye maji ya mto huo.

Mto huo unategemewa na maelfu ya wakazi wa eneo la Nyamongo lenye kata tatu za Kibasuka, Kemambo na Matongo. Maji ya mto huo hupitia kijiji cha Kewanja ambako ndiko tindikali asilia (siyo sumu) aina ya paf (potential acid forming material) huingilia kutoka kwenye rundo la mawe machafu yaliyowekwa na Barrick eneo la Gokona.

Lakini Uhahula, ambaye alikuwa anajibu maswali ya wataalamu, wabunge na mawaziri katika msafara wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ya Bunge chini ya Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai, Jumatatu iliyopita, alisema Barrick hawakuwaficha chochote.

“Naapa haki ya Mungu, hapa tulifika,” alisema Uhahula huku akiashiria kukata shingo kwa kidole alichogusisha kwenye mchanga msafara huo ulipofika kushuhudia dimbwi dogo la maji mekundu mithili ya damu yaliyojikusanya kutoka kwenye mawe yenye tindikali ya paf katika eneo la Gokona.

“Naona imeingia siasa katika suala hili, maana hapa tulifika na pale tulifika pia,” alisisitiza Uhaula huku akionyesha maeneo hayo.

Hata alipoulizwa na Ndugai kwamba Kagasheki alidanganywa wapi, Uhahula alijibu hakuna.

“Tulipokuja na Barrick tulipandia pale, hatukusimama hapa tulipo,” alifafanua Uhahula akionyesha tofauti ya kama mita tano hivi.

Kamati hiyo ilitembelea maeneo yote yanayolalamikiwa ya Nyabirama, hasa Gakona ambako ni chimbuko la mkasa huo.

Eneo lote chini ya tuta kubwa kuelekea kwenye shamba la migomba ya ndizi limejaa maji yanayovuja kutoka kwenye mabwawa ya kuhifadhia maji yenye tindikali hiyo ya paf katika eneo hilo. Majani yote yanaonekana yamenyauka kutokana na tindikali hiyo ambayo kwa asili iko kwenye miamba inayochimbwa madini.

Tindikali hiyo ndiyo inadaiwa na wakazi wa Nyamongo kwamba, imesababisha vifo vya watu na mifugo kadhaa katika vijiji vya Nyakunguru, Nyarwana, Weigita na Nyangoto.

Wiki iliyopita wakazi hao walidai tindikali hiyo ilisababisha vifo vya watu 21, lakini kamati ya Ndugai iliambiwa vifo vimefikia watu 43, ng’ombe 401, mbuzi 523, kondoo 185, punda 63 na mbwa 227. Taarifa hiyo haina uthibitisho wa wataalamu.

Aidha, Kamati ya Ndugai iliambiwa pia kwamba kuna wagonjwa kadhaa walioathiriwa na tindikali hiyo pamoja na vumbi linalotokana na umwagiliaji wa maji hayo na linalotimuka kutokana na upasuaji miamba.

Vilevile, wanadai kwamba nyumba nyingi zimepata nyufa kutokana na mtikisiko wa shughuli za upasuaji na nyingine kupigwa na mawe. Pia wanadai kuwa vyanzo vyote vya maji vimepata tindikali.

Hata hivyo, wataalamu mbalimbali kutoka Baraza la Mazingira (Nemc), Bonde la Ziwa Victoria (Lake Victoria Initiative), ofisi ya Mkemia Mkuu na Barrick walisema kiasi cha tindikali hiyo ya paf (ph) haina uwezo wa kusababisha madhara hayo.

Kuthibitisha kwamba sumu hiyo pamoja na cyanide inayotumiwa kusafishia madini eneo la Nyabirama hazina madhara, Mtaalamu wa mazingira wa Barrick, Samwel Hailu na Ofisa Mawasiliano wa kampuni hiyo, Tewell Tewell walikunywa maji hayo. Kamati ya wataalamu wa mazingira, afya, Mkemia Mkuu imepewa siku 14 kukamilisha kazi ya kubaini tatizo hilo.

Wiki iliyopita Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Balozi Khamisi Kagasheki alisema kuwa alitembelea mgodi huo kwa maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili kujionea hali halisi na kujua ukweli wa mambo.

Akisimulia aliyokutana nayo katika mgodi huo, Balozi Kagasheki alisema alipokwenda alipokelewa vizuri na uongozi wa mgodi huo na kumtembeza katika maeneo waliyoeleza kuwa ndiyo yanayodaiwa kuwa chanzo cha kuvuja kwa sumu hiyo.

"Nilikwenda kutembelea mgodi wa North Mara, nikifuata maagizo aliyoyatoa Waziri Mkuu alipokuwa akitoa majumuisho ya hotuba yake ya bajeti. Nilipofika huko uongozi ulinipokea vizuri na kunitembeza katika maeneo waliyoeleza kuwa chanzo cha kuvuja sumu hiyo," alisema Balozi Kagasheki na kuongeza kuwa baadaye msamaria mmoja alimwambia kuwa wanamdanganya kuna eneo ambalo hali hiyo inaonyesha wazi athari za sumu hiyo.

"Baada ya kumfuata msamaria huyo nilijionea hali halisi, nikasikitika sana kwa sababu uongozi wa mgodi ulinidanganya. Niliyoyaona nitapeleka kwa Waziri Mkuu, kwa kweli si nzuri, itabidi nifikishe ripoti kwa Waziri Mkuu," alisema naibu waziri huyo akionyesha kukasirika na kusikitika kwa tukio hilo.
 
hawa nao yaani kunywa maji ndo kipimo kuwa maji hayana sumu??mbona kazi ipo hapa ..haya ngoja tusubiri
 
Ebu anagalia hii hapa fact,

13th July 2009..... Source NIPASHE







headline_bullet.jpg
Itawasilishwa bungeni na kujadiliwa



Job.jpg

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Job Ndugai.



Taarifa ya uchunguzi wa mgodi wa North Mara ulioko wilayani Tarime mkoa wa Mara, imekamilika na itakabidhiwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, leo na wabunge kupata nafasi ya kuijadili wiki hii.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Job Ndugai, ambayo ilifanya uchunguzi wa sakata zima, aliliambia gazeti hili katika viwanja vya Bunge mwishoni mwa wiki, kuwa kamati yake imekwisha kukamilisha kazi ya kuandika ripoti.
Kamati hiyo ilikwenda North Mara kufanya uchunguzi huo, wiki mbili zilizopita, kufuatia madai ya
wananchi wa eneo hilo kuwa maji ya mto Tigithe ambayo wanayatumia kwa matumizi yao na mifugo, yamechafuliwa na sumu inayotiririka kutoka kwenye mabwawa ya mgodi huo na kuingia mtoni.
Bila kuzungumzia kwa undani mambo ambayo Kamati yake imebaini, Ndugai alisema: “Sisi tupo na wananchi, hatuwezi kuwakumbatia wawekezaji.”
Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Kongwa (CCM), alisema Kamati yake imefanya kazi yake kwa usahihi na umakini mkubwa.
Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alisema kutokana na unyeti wa ripoti hiyo, atairuhusu Kamati ya Ndugai kuiwasilisha bungeni ili umma uweze kujua ukweli wa sakata zima. "Nitampa nafasi Mwenyekiti kuiwasilisha taarifa yake baadaye, kwa sababu ina 'public interest', tusubiri niipate," alisema Spika Sitta katika majibu yake ya maandishi kwa Nipashe.
Serikali ilifikia uamuzi wa kuchunguza madhara ya maji ya mto Tigithe kutokana na malalamiko ya wananchi wanaotumia maji hayo kuwa yamechafuliwa na sumu inayotoka katika mabwawa ya mgodi wa North Mara, unaomilikiwa na kampuni ya Barrick Gold Tanzania.
Kumekuwa na madai ya vifo vya watu zaidi ya 40 huku mamia ya mifugo ikidaiwa kufa; watu wengine wanadaiwa kuwa ni wagonjwa kutokana na madhara ya maji hayo.
Mimea pia imekauka kandokando ya mto huo.
Katika hatua nyingine, habari kutoka Mara zinasema licha ya Serikali kutamka kuwa maji ya mto huo kuwa hayafai kwa matumizi ya viumbe hai kutokana na kubainika kuwa na sumu, bado mgodi huo wa North Mara unaendelea kutiririsha maji yanayoingia kwenye mto huo, ambao maji yake yanatumiwa na binadamu na mifugo.
Mapema mwezi huu, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hamisi Kagasheki, alitangaza kuwa maji ya mto huo hayafai kwa matumizi ya binadamu, baada ya kujionea mwenyewe jinsi maji ya sumu yanavyotiririka kutoka kwenye mabwawa hayo hadi mtoni.
Siku chache tu baada ya kauli hiyo Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ikishirikiana na ile ya Nishati na Madini, zilifanya ziara na kujionea hali halisi sambamba na kukutana na wananchi na uongozi wa mgodi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Batilda Burian, akitoa taarifa ya serikali mara baada ya kikao cha majumuisho ya kamati hiyo kwa waandishi wa habari alisema maji hayo hayafai kwa matumzi ya binadamu.
Alisema kutokana na maji ya sumu kuendelea kuvuja na kuingia mtoni, itabidi wananchi watafutiwe vyanzo vingine vya maji, na kwamba kazi hiyo ifanyike haraka iwezekanavyo ili kunusuru maisha ya watu na viumbe wengine.
 
Haya, naona hii issue imelala mpaka uchaguzi...ripoti ya wataalum ilidai kuna haja ya upelelzi zaidi. Waliodaiwa waathirikia wamepimwa na la...hakuna uhusiano wa kisayansi. Kama ni hivyo basi watnzania tunastahili tuzo ya siasa.

Kama haitoshi sasa naona NGO zilizorusha madai bila ushahidi wa kisayansi zinaanza kubanwa....

Barrick Gold Corporation and African Barrick Gold would like to take this opportunity to respond to false allegations made by Foundation HELP, a non-governmental organization located in the Tarime District of Tanzania.
We are deeply concerned that Foundation HELP continues to circulate alarming material which attributes serious health ailments to the operations of the North Mara mine. The material in question features photographs of two persons, a young male and an elderly female, with severe skin conditions. Devoid of medical evidence of any kind, these images are the basis for a "call to action" against the mine and have been distributed widely via the internet by activist groups.
African Barrick Gold has taken a series of actions consistent with our commitment as a responsible corporate citizen. To be clear, any credible claim of a health issue associated with the company's operations (whether involving an employee or community member) would be assessed and any necessary medical assistance provided.

We have attempted to identify and locate these two individuals. Although we enlisted the assistance of government and village leaders, we have been unable to do so. No one has come forward or indicated they know these persons or could assist us.

We then consulted with a team of medical experts, namely Dr. Robert Weiss, President, Dermatology Society of South Africa, Dr. Rob Barbour, Chief Medical Officer for Barrick Gold Corporation, Dr. Mark Divall, an occupational health physician based in South Africa, and Mr. Yahya Kishahu, an occupational health specialist and academic with Muhimbili University College for Health Sciences of Tanzania.
They each examined the photographs and provided their assessment of the possible causes of the medical conditions afflicting the two individuals. Their analysis is limited to the images circulated and, to arrive at a comprehensive conclusion, a full medical examination and case history would be required.
Based on their assessment, however, the image of the elderly woman (identified as Mama Otaigo, allegedly from Weigita village) shows a condition that is entirely consistent with vitiligo, a chronic disorder that causes depigmentation of patches of skin. The causes or origins of this disease is largely unknown but is widely considered to have an immunological basis.
The image of a young boy (identified as Paul, allegedly from Nkerege village) is consistent with a form of ichthyoids (Lamellar), an inherited skin disorder which causes plate-like scaling of the entire body surface and is present at birth.
These medical disorders are chronic, long-term diseases caused by genetics, immunological or other conditions. They were not caused by impacts associated with the North Mara operation over the past year, as claimed by Foundation HELP.
As Dr. Weiss stated, "there is no doubt that neither of these conditions are the result of contaminated water." Furthermore, the two villages cited by Foundation HELP are located some 30 to 35 kilometers away from North Mara and both are upstream from the mine.


To our knowledge, Foundation HELP has made no effort to have these cases brought to the attention of authorities or a qualified medical professional. No effort has been made to contact the company or the mine.
Thus, we have concluded that Foundation HELP's claims are neither credible nor motivated out of concern for these two individuals. This organization is not raising awareness of a public health concern or seeking assistance for these alleged victims. Rather, this material exploits the ill-health of others to mobilize anti-mining sentiment and harm the reputation of our companies.
ABG has requested that Foundation HELP cease from repeating and circulating these defamatory allegations. Regrettably, their response has been to ignore this appeal, to circulate this material more widely, and avoid taking any responsibility for the truthfulness of their claims. For this reason, ABG directed legal counsel to contact this organization to seek a retraction of this material from circulation. We continue to strongly urge all those involved with Foundation HELP to be accountable and refrain from repeating these false allegations.
We are also concerned about the health and well-being of this young boy and elderly woman. On humanitarian grounds, ABG's medical professionals would welcome the opportunity to provide assistance by directing them to the appropriate medical experts.
As leaders in corporate social responsibility, Barrick and ABG are committed to making a positive contribution to local communities. To date, we have invested US$40 million in community programs and initiatives in Tanzania, including vital health programs which have benefited tens of thousands of people.
We will continue to ensure that our stakeholders have accurate information about the impact and benefits of our operations in Tanzania, today and in the future.
 
Taarifa kwa vyombo vya habari: Kujibu taarifa zilizotolewa kwenye gazeti siku ya Jumapili, tarehe 21 Juni 2009

Mara, Juni 23 2009 – Uongozi wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara unapenda kukanusha vikali shutuma zilizotolewa na gazeti la Mtanzania la Juni 21 2009, likidai kwamba watu 21 na zaidi ya ng’ombe 200 kutoka Kata ya Kibasuka, wilaya ya Tarime wamekufa kutokana na kunywa maji yenye Kiwango Kidogo cha Uasidi kwenye Maji ya Mto Tigithe. Taarifa hiyo iliyoandikwa na mwandishi wake Bw Christopher Gamaina ikimnukuu kwa kirefu Diwani wa Kata ya Kibasuka na kuvumisha kuwa vifo hivyo vimesababishwa na uvujaji wa maji kutoka Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.

Tunapenda kusema kwamba malalamko haya si ya kweli na ni batili. Taarifa hiyo haikufanyiwa uchunguzi, ina malengo mabaya, na siyo ya msingi kabisa; jambo ambalo limethibitishwa na mamlaka zinazohusika.

Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania inapenda kutoa ufafanuzi kama ifuatavyo;
  • Mnamo Juni 15 2009 Mgodi wa Dhahabu wa North Mara ilipokea nakala ya barua ya malalamiko kutoka kwa Diwani wa Kata ya Kibasuka iliyotumwa kwa ofisi ya Waziri Mkuu.
  • Barua hiyo ilidai kwamba watu 18 na zaidi ya ng’ombe 200 kutoka kata ya Kibasuka wilaya ya Tarime wamekufa kutokana na kunywa maji yenye kiwango kidogo cha uasidi ya mto Tigithe .
  • Mara baada ya kupata taarifa hizo mgodi wa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara uliwasiliana na mamlaka husika ili kuzihimiza kufanya uchunguzi.
  • Mnamo tarehe 21 Juni 2009, timu ya uchunguzi iliundwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime kuchunguza malalamiko hayo.
  • Timu hiyo iliyowajumuisha Afisa Afya Mkuu wa Wilaya, Afisa Maendeleo ya Kilimo na Mifugo wa Wilaya, Mkuu wa Polisi wa Wilaya pamoja na Afisa Afya wa Mkoa walitembelea vijiji vilivyotajwa kwenye barua hiyo ambavyo ni pamoja na kituo cha afya cha Nyarwana, ambacho kwa mujibu wa barua hiyo kilikuwa na taarifa muhimu za kuthibitisha shutuma hizo. Timu hiyo ya uchunguzi iliongea na mkuu wa kituo hicho na kuchunguza kumbukumbu za matibabu ambapo zote zilishindwa kuthibitisha shutuma hizo.
  • Zaidi ya hayo wakati Diwani wa Kata ya Kibasuka alipokutana na timu hiyo ya uchunguzi, alishindwa kuthibitisha vifo vya watu hao 21 aliowaripoti. Pia alishindwa kuandaa mkutano na wafugaji wa ng’ombe 200 aliodai wamekufa na vilevile alishindwa kuonyesha mizoga yao. Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pia ilitoa taarifa kwamba Diwani huyo wa Kata baadae alidai kwamba vyombo hivyo vya habari vilimnukuu vibaya.
Mgodi wa Dhahabu wa North Mara inakusudia kufungua rasmi malalamiko kwa Baraza la Habari Tanzania na kuchukua hatua zozote muhimu ili kuepusha shutuma zisizo na ukweli zinazokusudia kuchafua heshima yake na kusababisha msuguano na jamii inayouzunguka.

Kuhusu Shirika la Dhahabu la Barrick
Shirika la Dhahabu la Barrick ni kampuni ya uchimbaji madini inayoongoza ulimwenguni. Hisa za Barrick zimeorodheshwa katika soko la hisa la huko Toronto na New York.

Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania inaendesha migodi minne nchini Tanzania. Ambayo ni Bulyanhulu, North Mara, Tulawaka na Buzwagi.

Imetolewa na:
Teweli Kyara Teweli
Uhusiano na Mawasiliano
Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Tanzania,
Kitalu 1736, Br. Hamza Aziz,
S.L.P 1081, Dar es Salaam
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

NB:
Kwanini Barrick?
Kwanini uchunguzi wa mambo ya namna hii usiwe na SOP yake inayofuatwa nchi nzima badala ya kila tukio kutafutiwa njia yake ya kuchunguza?

Kwanini tume ya Haki za Binadamu isipewe jukumu la kuchunguza tuhuma za aina hii au kitengo fulani chini ya Jeshi la Polisi na taasisi za haki
Hawa ndio Barrick, kazi kubadili tuu majina, wakawa ABG, sasa ni Acacia!. Why?.

P.
 
Back
Top Bottom