Ongezeni matawi mengi tunapata shida sana hasa mwisho wa mwezi tafuteni mbinu nyingine za kuhudumia wateja wenu kiukweli mnakera sana
 
Matawi ni machache, inabidi kusafiri umbali fulani kufuata tawi/ATM. Pia ATM unaweza kukuta ziko 3 lakini 1 tu inafanya kazi foleni inakuwa kubwa sana. Zaidi ya hayo, naipenda NMB nikilinganisha na nyingine ZOTE za kiwango changu.
 
Unakuta madirisha ya matela Ni 9 lakin tella Mmoja tu, shida kwel kwel, jirekebisheni tutawakimbia ,muige wenzenu wanafanyaje mfano crdb!..
 
Bank ya NMB ina utaratibu wake ambao ni kuwajaza wateja bila kujali kama watapata huduma bora au bora huduma.
 
Nmb nibenki amboyo inatukela Sana kwa utaratibu wao mbovu Sana foreni kubwa hakuna viti vya kukaria unaweza ukasimama kwenye foreni mpaka ukapata kizungu zungu. Tunaomba waboreshe huduma zao.
 
Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.

Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta ? Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe ?Siri?)
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom

Mi ningependa kujua kuhusu kadi zenu mpya za tanzanite,pia ningepata mchanguo Wa makato kukusu usomaji Wa salio kwa kutumia mobile na utoaji,pia kwa kadi za kawaida na hizi mpya.
 
Sijajua kama limeshajibiwa hili ila kwa vile customer care ni kumhudumia mteja individually naomba mjibu tu hata kama ninauliza mara ya 111100.

Je mna mpango wa huduma za pesa kwa mtandao? hii namaanisha kuwa kuwe na app kwenye simu za adroid na iOS ambayo mtu akiwa na data tu anaweza kuhamisha pesa, kuona statement ama kuangalia balance bila makato ya kijinga kabisa kama ya sasa. Sijui mnakuaje bank za Tz, eti huduma ya bank mpk niwe na vocha kwenye simu alafu *150*66#, hapo bado bank na nyie mnakata (eti gharama za kuangalia salio) huu ni wizi wa wazi wazi. Sasa kama natumia wi-fi au sipo Tanzania siwezi ona salio/statement/transfer monies.

Wenzetu walishapiga hatua hizo zamani sana, mpaka ukipoteza kadi unapewa nyingine free na haraka.
Je mna huo mpango ama lazima tuwafaidishe wenye mitandao ya simu na nyie?

rant rant rant rant
 
Sijajua kama limeshajibiwa hili ila kwa vile customer care ni kumhudumia mteja individually naomba mjibu tu hata kama ninauliza mara ya 111100.

Je mna mpango wa huduma za pesa kwa mtandao? hii namaanisha kuwa kuwe na app kwenye simu za adroid na iOS ambayo mtu akiwa na data tu anaweza kuhamisha pesa, kuona statement ama kuangalia balance bila makato ya kijinga kabisa kama ya sasa. Sijui mnakuaje bank za Tz, eti huduma ya bank mpk niwe na vocha kwenye simu alafu *150*66#, hapo bado bank na nyie mnakata (eti gharama za kuangalia salio) huu ni wizi wa wazi wazi. Sasa kama natumia wi-fi au sipo Tanzania siwezi ona salio/statement/transfer monies.

Wenzetu walishapiga hatua hizo zamani sana, mpaka ukipoteza kadi unapewa nyingine free na haraka.
Je mna huo mpango ama lazima tuwafaidishe wenye mitandao ya simu na nyie?

rant rant rant rant

Hapa Kz tu JPM atamaliza
 
Sometims wahudumu wenu hapo bank house wanazingua wait one day nitaibuka na dingi wangu mdogo JPM
 
Ni kwanini msiwe na special programs za kuwawezesha wahitimu wa vyuo mbalimbali kuwapa loan under special guidance, wafanye maandiko(proposals)kwenye vikundi kama wanaanzisha miradi yamaendeleo ili kupunguza shila kubwa ya kutangatanga na ajira!
 
Ndugu, NMB, nitawezaje kupata mortgage kupitia NMB? AC yangu pia iko pale kwa muda tu..naomba maelekezo ya kutosha maana kila nikienda kwenye tawi langu mlimani city, wale wakina mama wanadai bado hamjaanza hio huduma, au hawajui?!
 
bolesheni huduma zenu mnaongoza kwa huduma mbovu mtu ukienda ku deposit unatumia masaa mawili mnaongoza kwa huduma mbovu
 
Mshahara wangu uko benki kwenu mwajiri kaniandikia barua mniwekee mshahara tangu alhamis hadi leo sijaupata tatizo ni nini?
Au inachukua siku ngapi?
 
Ukweli huduma ni mbovu katika branch zenu, ku deposit unakaa hadi masaa matatu ukiwa katika foleni na simu huruhusiwi kutumia sasa kazi zetu nje zitaendaje?

Madirisha ya tellers ni mengi ila utashangaa linafanya kazi dirisha moja kati ya madirisha 8. ATM ndio taabu kila mara hazina pesa na risiti, customer care nao lugha hazieleweki.

Yaani ni bora utunze pesa kwenye kibubu kuliko NATIONAL MICROFINANCE BANK
 
Back
Top Bottom