Nini hatma ya katibu mkuu wa Nishati na Madini?

link haifanyi kazi labda michuzi kafuta post
Yaani watu na akili zenu mnategemea Breaking news kwa source ya mpiga picha Michuzi!? you must be joking. pale ukipewa taarifa ya mnuso leo wapi hapo wala usiwe na mashaka ndio habari zao pale.
JF haiwezi kukosa Breaking News halafu awe nayo Michuzi hii aiclick kwenye ubongo wangu.
 
link haifanyi kazi labda michuzi kafuta post

Ya kafuta cheki post namba 45 hapo juu, nilichukua screeshot kabla hajafuta. Naona na Mods tayari wameshachakachua title ya thread. Badala ya "Jairo Kajiuzulu" imekuwa "Nini hatma ya Katibu mkuu wa Nishati na Madini?" Sasa kama tayari ameshajiuzulu na tayari kawekwa katibu mwingine, tutakuwa tunamjadili nani hapa? BTW hatujadili hatma yake hapa. Hatma yake tayari inajulikana. Mods mtufanye sie wa kuja. Nina wasiwasi wataondoa na hii screenshot toka kwa Michuzi. Waiache ibaki hapo, tupime hivi vyombo vyetu vya habari. Michuzi amekuwa na tabia ya kuweka habari nyeti halafu anazitoa. Kama ile ya Watanzania waliomlalamikia Balozi wa Tanzania Saudi Arabia haujulikani hatma yao imeisha vipi na kama balozo kachukuliwa hatua.
 
Kamtindo alikofanya Jairo, mbona ni kafasheni kalikoshamiri sana, na ni maagizo ya wakubwa zake, yeye ni mtekelezaji tu na bahati mbaya ndyo imemkuta yeye.
 
Bila Ngeleja na Malima kuondoka ni upuuzi mtupu. Fedha zilitumika kulainisha wabunge ili Ngeleja na Malima wasipate wakati mgumu kuwasilisha Bajeti. Swali kama bajeti inatokana na fungu la hazina na wizara ya fedha, Fedha hizi tayari tulikwisha julishwa na Mkulo kwenye bajeti yake. Kwa nini Ngelaja and the Group wapate kiwewe hata kuhonga wabunge. Ni kitu gani kinafanywa kwenye fedha za bajeti? Na je hizo 50m sio fedha za walipa kodi?
Je kikao cha kuchangisha si kilifanyika ofisini kwa Ngeleja? Jairo si alipewa maagizo tu naye akatekeleza. Kama kwa EL, Karamag, Na Msabaha. Kama kwa Yona, Mramba na Mgonja. Kama kwa Chenge, EL na RA. Kama kwa EPA RA, Mkapa, na hawa lazima waondoke wote.
 
hii ndio michuzi alichofanya jana
 

Attachments

  • michuzi.docx
    594.8 KB · Views: 31
Hiki ni kiini macho tu, ingefaa system nzima ikawa overhauled. Ni aibu kwa nchi kama hii yenye a lot of resourses ambayo investors wanaikimbilia kuwa giza.
 
Back
Top Bottom