Nini asili ya jina Tanganyika na Nani alilitunga jina hili?

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
5,012
Kumekuwepo maswali ya watu wengi wakitaka kujua ASILI ya JINA la TANGANYIKA.

Ili kuweza kuhakikisha mjadala unakuwa endelevu na msomaji anapata majibu sahihi, tumeonelea ni vema kuweka mjadala huu kwa pamoja:

ILIANZA HIVI:
Jamani nimekuwa nikijiuliza sana jina la Tanganyika lilitokeatokea vipi, kama lilitungwa ni nani aliyelitunga na maana yake ni nini. Naomba wataalamu wa historia wanijuze tafadhali.

=============
Baadhi ya maoni:
Neno Tanga ni la Kiarabu limetokana na neno Tanja na Waarabu walipofika pwani ya Afrika mashariki ijulikanayo kwa sasa kama Tanga, waliufananisha na mji uitwao Tangier (Morocco) na kwa kuwa Tanga kulikuwa na msitu unaoingilika (Nyika) na ili kutofautisha kati ya Tanja ya mjini na Tanja ya nyikani, ikaitwa Tanganyika ikimaanisha kutofautisha baina ya Tanga (mji) na kuingia (Ushenzini) Tanga-nyikani.

Huwezi kuuondoa Uarabu uliopo Afrika, hata ufanye nini, kwani Uarabu mwingi upo Afrika kuliko huko kunakojulikana kwa sasa kama Uarabuni. Huo ndio ukweli. Amini usiamini.

Bora wewe umetoa maelezo yenye mashiko!!!

Ningependa kuongezea kidogo:

Wajerumani walivyokuja waliipenda sana milima ya Usambara hususani Usambara Mashariki (Amani). Walikuta wenyeji Wasambaa, Wabondei na Wadigo maeneo yale.

Wabondei walikuwa wakiyaita maeneo ya tambarare yanayoelekea bahari ya Hindi NTANGA(au TANGA kwa kiswahili chepesi) wakimaanisha Shambani.

Hiyo ndio source ya jina Tanga. Kazi ikawa kwenye maeneo ya interior ya Tanzania. Wasambaa na Wabondei waliyaita maeneo ya mbali na kwao kwa jina la NYIKA (sawasawa na jina KYASAKA kwa kichagga). Wajerumani walivyowauliza wenyeji jina la maeneo yaliyoko mbali na kwao ukiachilia mbali eneo la pwani ya bahari ya Hindi walisema ni NYIKA. Ndipo wajerumani walipoamua kulipa koloni lao la DUTCH OSTA AFRIKA jina la TANGANYIKA meaning TANGA na NYIKA ZAKE au TANGA INCLUDING ITS INTERIOR LANDS

Katika muendelezo wangu wa kutafuta kiini cha la Matatizo yetu, leo hii najikita ktk kuelezea kuhusu Jina la Tanganyika yaani asili yake na ni nini mana yake, kwa wale ambao bado hawafahamu...

Tanganyika ni Muunganiko wa maneno mawili yaani Tanga na Nyika. Maneno haya yaliunganishwa pamoja na kuunda neno Moja Tanganyika, na hili lilifanywa na Wajerumani waliokuwa wakitawala Nchi yetu kipindi hicho!

Wajerumani walikuja na jina hilo baada ya kuanza kutawala Nchi yetu ambayo Mpaka wake kwa Upande wa Kusini ni Mto Ruvuma na Magharibi ni Ziwa kubwa lilokuja kupewa Jina la Tanganyika (na Wajerumani).

Kumbuka Wajerumani walivyofika walikaa kwanza Pwani ambapo walijenga Bandari ya Dar na pamoja na Tanga, sasa Eneo la nchi yao au yetu lilikuwa linatoka Tanga mpaka kwenye Ziwa (baadae Tangayika), na mji wa Tanga peke yake ndio uliokuwa umepimwa yaani Mipango Miji lkn kutoka Tanga mpaka kwenye Ziwa kulikuwa na Misitu mizito yaani Nyika au kwa kifupi kulikuwa hakujapimwa hivyo wakaamua kuliita lile Ziwa Tanga-nyika yaani kati ya Tanga na Nyika au misitu minene.

Baada ya Waingereza kuja walitaka kubadilisha jina la Nchi iliyokuwa inaitwa Ujerumani ya Afrika Mashariki, kulikuwa na majina manne ambayo waliyapendekeza nayo ni New Maryland, Windsorland na Victoria, lakini pia Majina ya Kilimanjaro na Tabora yalipendekezwa na mwishowe Gavana aliyekuwa anajulikana kwa jina la Alfred Milner akaamua kuchukua jina Ziwa ambalo lilibatizwa Tanganyika na Wajerumani kama jina la Nchi yao!

Nafikiri ndio moja ya sababu ya Mlm.Nyerere kulikataa jina la Tanganyika baada ya Uhuru kwani kwake yeye bado lilikuwa ni jina la Mkoloni kama vile ilivyokuwa Ghana- Gold coast, au Zimbabwe na Zambia- Rhodesia, Malawi -Nyasa land na Hata Afrika Kusini au South Africa kuna kipindi ANC walikuwa hawalitaki kwamba ni jina la Kizungu na walitaka kutumia Azania badala yake!
 
mwalimu wangu wa historia aliniambia.
Limetokana na mzungu m1 aliyekua anajaribu kuelezea wasomaji wa kitabu chake alichokiandika.
Alikuwa anawaelekeza sehemu ambapo raw materials znapatikana.
Akawa anasema.

From tanga to nyika land .
Mean interior of Tz.

Ndo ikawa inaitwa
Tanganyika.
 
Nikirejea historia, kabla ya kuja kwa wakoloni, hapakuwa na tanganyika kama nchi. kulikuwa na jamii za wabantu aambazo zilikuwa na tawala zao kamili. Baadhi ya tawala hizo ni:
1. Milambo Kingdom
2. Yao kingdom,
3. Buha kingdom.
4. Bahaya kingdom na nyingine nyingi. hapakuwa na jina jina tanganyika kama nchi.

Wapelelezi(explores walipofika katika maeneo haya, walianza kusign mikataba ya kutwaa maeneo ya east Africa. eneo lote kutoka kigoma, likapewa jina tanganyika jina lililokuwa likitumiwa na wenyeji wa kigoma/ujiji- kuita eneo lao lilikuwa na maji ya kutosha ndilo ziwa tanganyika.

hivyo hata wakati wa kudai uhuru, kwa kuwa maeneo yote yaliyokuwa chini ya mjerumani yalitambulika kama tanganyika, hata wapigania uhuru walibaki kulitumia jina hilo kwani tayari lilikuwa limeshazoeleka sehemu tofauti za ardhi yetu.

nawasilisha tafadhali.
 
Mwanakili90

Huyu mzungu alikuja lini, kwa hiyo ina maana kabla huyu mzungu hajaja hatukuwa na jina? Kama tulikuwa nalo lilikuwa lipi kuna anayeweza kujua.
 
Last edited by a moderator:
Kuna sehemu kati ya Muheza na Tanga katika Mkoa wa Tanga ambayo inaitwa Tanganyika inawezekana ikawa ndiyo chanzo cha jina hilo kutumika kwa nchi nzima.
 
Huyu mzungu alikuja lini, kwa hiyo ina maana kabla huyu mzungu hajaja hatukuwa na jina? Kama tulikuwa nalo lilikuwa lipi kuna anayeweza kujua.
Kaka nadhan umepata pcha jnsi lilivopatikana.

Kabla ya kujulikana ilo kuliku kunaitwa interior from indian ocean.
Then huyu mzungu ndo akaja na jinsi yake ya kuelezea.
Mean from Tanga to nyika land.
Maana alikutana na majan maref na mapori ambavyo coast hayakuwepo ambayo na wenyej waliziita nyika thats y akawa anatoa direction kwamba ukiwa tanga then u move to nyika land.
Ndo Tanganyika ikawa created ivyo.
 
Asante ntagunga kwa mchango wako, kwa hiyo maana hasa ya neno tanganyika ni maji au nini? Na kwa nini kigoma ikawa maarufu zaidi kiasi cha jina kutoka huko kuwa maarufu zaidi mpaka kuruthisha nchi nzima kuitwa hivyo?
 
Last edited by a moderator:
mhh,which z which!? Inasemekana jina tanganyika lilitoka na neno Sanganigwa(karibu,according to waha),wakati huo alifika Mzungu fulani maeneo ya ujiji na wakazi wa huko wakawa wakimlaki hivyo,sanganigwa..inasemekana alishindwa kutamka kwa ufasaha,akaishia kusema tanganyika(sanganigwa),.ofcourse mimi hii naiona somehow true kuliko nyingine za kuunga unga..
 
Ukifuatilia sana utagundua nchi yetu ilikuwa vipande vipande
Mfano nzuri ni Kilwa, ilikuwa ni nchi kamili ambayo ndiyo
ya kwanza kwa A.Mashariki kuanza kutumia fedha zake
yenyewe. Ukija Mtwara pale kati kulikuwa na nchi kamili ambayo mpaka
wake unaishia sehemu moja inaitwa Jiwe la mzungu kule Lindi na unaanzia
eneo fulani kule Msumbiji. Mzee mmoja alijaribu kufuatilia wakati wa Utawala
wa Mwalimu akataka kuidai hiyo nchi lakini kilichomkuta...... si mada yangu hapa
Kuhusu Tanganyika na mimi pia sijui.
 
Neno Tanga ni la Kiarabu limetokana na neno Tanja na Waarabu walipofika pwani ya Afrika mashariki ijulikanayo kwa sasa kama Tanga, waliufananisha na mji uitwao Tangier (Morocco) na kwa kuwa Tanga kulikuwa na msitu unaoingilika (Nyika) na ili kutofautisha kati ya Tanja ya mjini na Tanja ya nyikani, ikaitwa Tanganyika ikimaanisha kutofautisha baina ya Tanga (mji) na kuingia (Ushenzini) Tanga-nyikani.

Huwezi kuuondoa Uarabu uliopo Afrika, hata ufanye nini, kwani Uarabu mwingi upo Afrika kuliko huko kunakojulikana kwa sasa kama Uarabuni. Huo ndio ukweli. Amini usiamini.
 
Neno Tanga ni la Kiarabu limetokana na neno Tanja na Waarabu walipofika pwani ya Afrika mashariki ijulikanayo kwa sasa kama Tanga, waliufananisha na mji uitwao Tangier (Morocco) na kwa kuwa Tanga kulikuwa na msitu unaoingilika (Nyika) na ili kutofautisha kati ya Tanja ya mjini na Tanja ya nyikani, ikaitwa Tanganyika ikimaanisha kutofautisha baina ya Tanga (mji) na kuingia (Ushenzini) Tanga-nyikani.

Huwezi kuuondoa Uarabu uliopo Afrika, hata ufanye nini, kwani Uarabu mwingi upo Afrika kuliko huko kunakojulikana kwa sasa kama Uarabuni. Huo ndio ukweli. Amini usiamini.

Duuh!!!!!!!
 
Neno Tanga ni la Kiarabu limetokana na neno Tanja na Waarabu walipofika pwani ya Afrika mashariki ijulikanayo kwa sasa kama Tanga, waliufananisha na mji uitwao Tangier (Morocco) na kwa kuwa Tanga kulikuwa na msitu unaoingilika (Nyika) na ili kutofautisha kati ya Tanja ya mjini na Tanja ya nyikani, ikaitwa Tanganyika ikimaanisha kutofautisha baina ya Tanga (mji) na kuingia (Ushenzini) Tanga-nyikani.

Huwezi kuuondoa Uarabu uliopo Afrika, hata ufanye nini, kwani Uarabu mwingi upo Afrika kuliko huko kunakojulikana kwa sasa kama Uarabuni. Huo ndio ukweli. Amini usiamini.


Asante FaizaFoxy.
 
Thanks to all walionchangia naendelea kujifunza ingawa naona kuna mawazo tofautitofauti.
 
Kuna sehemu kati ya Muheza na Tanga katika Mkoa wa Tanga ambayo inaitwa Tanganyika inawezekana ikawa ndiyo chanzo cha jina hilo kutumika kwa nchi nzima.

Neno Tanganyika nila kibantu; na mfano kwa washona lina maana ya mahala maisha yanapoanzia. Ni vipi limekuwa jina la nchi yetu hiyo history siifahamu vizuri lakini la weza kuwa lilianza kutumika rasmi kama jina la nchi wakati wa scramble and partition for Africa ambapo ramani ya Africa ndipo ilipochorwa na mipaka ya nchi kuwekwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom