Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Kama mnakumbuka kuna kijana aliniomba mtoko juma lileee lililopita, nikaja hapa kuomba ushauri wa kivazi cha kutupia. Nawashukuru saaana, maana kila aloniona alinisifu kuwa nimependeza, maana hata barabarani wanaume walinivunjia shingo. Tuyaache hayo.
Wiki iliyopita nilimtembelea shoga yangu ambaye alikuwa anasoma huko mikoani, sasa akaniletea photo album yake ili niangalie picha wakati yeye anapika. Lahaula lakwata, si nikaona picha zake nyingi alizopiga na yule kijana wa mtoko, tena wakiwa katika mikao ya hasara hasara. Yaani huhitaji kuuliza kama ni mtu na mpenziwe kwani kila kitu kilikuwa kinajionyesha.Mara shoga akaja, nami kwa shauku nikamuuliza kama yule ni mpenziwe? Naye akanijibu kuwa alikuwa mpenzi wake wakati walipokuwa wakisoma wote huko kanda ya ziwa, lakini waliachana siku nyingi tangu akiwa kidato cha tatu, baada ya kumfumania na shangingi moja huko mitaani. Kwa kuwa walikuwa wamepishana vidato, yule kijana aliwahi kumaliza, na hawajaonana zaidi ya miaka mitatu sasa na wala hajui yuko wapi.
Nilijaribu kudadisi tabia zake kwa ujumla, akaniambia kwamba ni kijana mtulivu ila ana wivu sana na pia ana mkono mwepesi kupiga pale kunapotokea kutofautiana, aliendelea kusema kuwa ni mtu mwenye hasira za haraka asiye na subira, ila anajua kupenda na ni mnyenyekevu kweli. Mwenzenu limenishuka shuu, Je nimweleze kuwa huyo kijana anataka niwe na uhusiano naye au nijikaushe, na niachane na huyu kijana kimya kimya, maana hata kumkubalia sijamkubalia ila tunachat sana FB na SMS kila siku……………..
Wiki iliyopita nilimtembelea shoga yangu ambaye alikuwa anasoma huko mikoani, sasa akaniletea photo album yake ili niangalie picha wakati yeye anapika. Lahaula lakwata, si nikaona picha zake nyingi alizopiga na yule kijana wa mtoko, tena wakiwa katika mikao ya hasara hasara. Yaani huhitaji kuuliza kama ni mtu na mpenziwe kwani kila kitu kilikuwa kinajionyesha.Mara shoga akaja, nami kwa shauku nikamuuliza kama yule ni mpenziwe? Naye akanijibu kuwa alikuwa mpenzi wake wakati walipokuwa wakisoma wote huko kanda ya ziwa, lakini waliachana siku nyingi tangu akiwa kidato cha tatu, baada ya kumfumania na shangingi moja huko mitaani. Kwa kuwa walikuwa wamepishana vidato, yule kijana aliwahi kumaliza, na hawajaonana zaidi ya miaka mitatu sasa na wala hajui yuko wapi.
Nilijaribu kudadisi tabia zake kwa ujumla, akaniambia kwamba ni kijana mtulivu ila ana wivu sana na pia ana mkono mwepesi kupiga pale kunapotokea kutofautiana, aliendelea kusema kuwa ni mtu mwenye hasira za haraka asiye na subira, ila anajua kupenda na ni mnyenyekevu kweli. Mwenzenu limenishuka shuu, Je nimweleze kuwa huyo kijana anataka niwe na uhusiano naye au nijikaushe, na niachane na huyu kijana kimya kimya, maana hata kumkubalia sijamkubalia ila tunachat sana FB na SMS kila siku……………..