nawashukuruni sana, kwa zenu nyingi salamu
ninamsifu maulana, kunivusha muda mgumu
simanzi ilinibana, litoweka tabasamu
asanteni wana jambo,nimefarijika sana.
Kinyau pokea salamu zangu za ramabirambi. Pole sana kwa msiba huo, lakini kama tulivyofundishwa, kazi ya Mungu haina makosa. Tuliza mawazo yanko, jisahahulishe na msiba huo uangalie yaliyoko mbele yako.
Pokea pole Kinyau, kaka'ko kuondokea
Muumba msisahau, mwenywe ameamua
kumbuka pia Kinyau, kaka'ko kumuombea
Kuondokewa Kaka'ko, Kinyau pokea pole
Nasema pokea pole, kwa sala nawaombea
Punguza pia kelele, mayowe kumlilia
kumbuka mengi ya kale, kaka'ko mlotendea
Kuondokewa Kaka'ko, Kinyau pokea pole
Mapenzi yake Muumba, kaka'ko kumchukua
Hakuna cha lambalamba, mganga wa kugangua
Avuta bila ya kamba, Muumba wetu wajua?
Kuondokewa Kaka'ko, Kinyau pokea pole
Ni kwake tulipotoka, na kwake tutarejea
Nimtajaye Rabuka, aliyeumba dunia
Na kila kiloumbika, mwenyewe kakiumbia
Kuondokewa Kaka'ko, Kinyau pokea pole
Kinyau pole sana kwa masaibu yalokukuta. Mola akupe faraja na subira.
Najua huzuni uliyoyano hapo kwani nami nimempoteza mwanangu wiki hii na najua uzito wa kumpoteza wa karibu yako. Mungu akusaidie Kinyau na akupe nguvu kipindi hiki
Ninapata faraja sana kwa kuwa nanyi ktk forums hii.
Sante sana na Mungu akubarikini ila mjue kuna kibarua kigumu ktk hospitali zetu za kulipia bongo.... kuna walakini kule na wizara ya afya wamekaa kimya ili wafe wengi
oh Msanii pole sana ndugu yangu, Mungu amlaze mwanao peponi. Salamu za pole ziifikie familia yako.
Hakika bwana alimpenda zaidi mwanao amemwita kwake mbinguni.Pole sana.
Lol,
msiba ni jambo kubwa. Poleni sana hatuna cha kusema manake uchungu wa msiba anaeujua mfiwa.
poleni sana tunawakumbuka katika sala ili mpate nguvu za kuendelea bila wapendwa wenu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.