Mchaga
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 1,378
- 204
Muombe MunguKatika pilika pilika zangu za kimapenzi nimejikuta nimenaswa na penzi la mtoto wa Kizanzibar. Ni msomi anafanya shahada ya pili kwenye mambo ya Finance, nina maana ameenda shule! Anatoka familia yenye maadili. Ni mrembo. Mapenzi ni mwake, hakuna nilichokosa mara zote nilizokutana naye mechi zimekuwa zikiisha kwa suluhu na hakuna anayehitaji penalti wala msaada wa refarii.
Kuna tatizo moja, yeye ni muislam na mimi ni mkristo...tumejadili hili...anadai yeye haina shida. Kiti moto atakuwa ananipikia na hata kuoka. Nilimweleza siwezi kuacha pombe, yeye hajawahi kunywa ila akiwa na mimi namlazimisha walau sparkling wine robo glass, maana macho yake yanaita, chuchu embe tango, tiGo imo ya kutosha kwa kweli ni mrembo. Ukiweka na kiswahili chake cha Kizanzibar Masa nazimia. Nimemuonya asije JF kuna wakorofi.....!
Mabibi na mabwana hii imekaaje? hasa kwenye suala la dini...nisingependa abadili wala mimi nibadili. Sasa tukipata mtoto (Morgan Tsvangirai)
Malezi yake yatakuwaje? Huyu Mzanzibar tunaendana sana na hili la mahusiano yetu bila shaaa tutazidisha dumisha muungano, ule ufa tutauziba.
Any advise wakubwa.....
NB: Kibunango kuanzia leo mimi shemejio!