Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
- Thread starter
- #61
Ilboru ni ya 13, Msalato ya 17Mhhh, hatari sana.
Its not that bad, but not very good either.
Naomba kujua Ilboru na Msalato zimeshika nafasi gani.
Ilboru ni ya 13, Msalato ya 17Mhhh, hatari sana.
Its not that bad, but not very good either.
Naomba kujua Ilboru na Msalato zimeshika nafasi gani.
ukiangalia utitiri wa shule kwa sasa ilboru, Tabora school (The Head of Tanzania), mzumbe,kilakara IMO bado wanafanya vizuriTabora na Ilboru mbona nao wanafanya hivyo lakini hawapo kwenye kumi bora, tatizo nini ???
Anaweza Mkuu. Asubiri Vyuo Vikuu vitoe vigezo vyao kwa kila koziMkuu mwabangu wa kike kapata div 3 anaweza pata chuo kwa udhamin Wa serikali alipenda sana asome medicen
Asante mkuuAnaweza Mkuu. Asubiri Vyuo Vikuu vitoe vigezo vyao kwa kila kozi
Ha ha ha ha Waboisia, tupo pamoja wakuu!Sijaangalia ni ya ngapi mkuu,
Lakini haipo kwenye kumi bora jamani.
Nimesikitishwa sana
Chuo atapata ila sio kwa MDMkuu mwabangu wa kike kapata div 3 anaweza pata chuo kwa udhamin Wa serikali alipenda sana asome medicen
Vigezo tayari vishatolewa na TCUAnaweza Mkuu. Asubiri Vyuo Vikuu vitoe vigezo vyao kwa kila kozi
Masikini!Ilboru ni ya 13, Msalato ya 17
Vigezo vipoje mkuu msaada tafadhariVigezo tayari vishatolewa na TCU
Mkuu, TCU hutoa vigezo kwa ujumla. Kila chou kina mamlaka ya kutoa vigezo vyake, bila kuviathiri vile vya TCU, kwa kila koziVigezo tayari vishatolewa na TCU
Hili swala nimeliwaza pia..kwa miaka hii miwili feza boys wamefichwa kabisaje siyo mpango wa wizara na wa ndalichako kuitumia Kibaha kama pilot kwa jinsi wanavyojua wao ili ionekane ktk miaka hii mi 3 ya Jiwe shule za serikali zimerudi kileleni na kupoteza za private
Nimeona,ukiangalia utitiri wa shule kwa sasa ilboru, Tabora school (The Head of Tanzania), mzumbe,kilakara IMO bado wanafanya vizuri
Mwanzo mwanzoni, napenda kuweka mambo yafuatayo wazi ili nisieleweke vibaya. Mosi, napenda sana kuimarika kwa elimu na kuongezeka kwa ufaulu. Kuimarika kwa elimu na kuongezeka kwa ufaulu kunatupa matumani ya kupata wataalamu wa kada mbalimbali za kisayansi na kijamii katika kusongesha mbele gurudumu la Taifa letu pendwa la Tanzania. Wanafunzi wanapaswa kusoma, kuelimika na kufaulu.
Pili, napenda Shule zote bila kujali ni za Serikali au za watu binafsi. Elimu bora yaweza kupatikana popote. Naomba nitanie kidogo. Katika miaka ya tisini na elfu mbili mwanzoni, 'wenye akili' walikuwa wakisoma katika shule za Serikali. Kusoma shule binafsi kulikuwa ni kujianika kuwa una walakini katika ufaulu wako. Ni kama waliofeli ndio waliokuwa wakisoma Shule binafsi. Mambo yakabadilika hivi karibuni.
Katika matokeo ya mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne na sita, Shule za Serikali hazikuwa zikifua dafu. Zilitupwa nje hata kwenye Shule kumi bora za kitaifa na hata hazikutoa wanafunzi bora wa kitaifa. Hata zile 'Shule za Vipaji Maalum' za Kibaha, Mzumbe, Ilboru, Msalato na Kilakala hazikufua dafu. Suala hili si tu lilikuwa likisumbua vichwa vya viongozi wetu, bali hata wadau wa elimu kama mimi.
Hivi punde, Baraza la Taifa la Mitihani nchini limetangaza matokeo ya kidato cha sita. Niweke wazi kuwa nimefarijika sana. Ni kwakuwa Shule za Serikali 'zimerejesha heshima yake' kupitia kwa Shule ya Sekondari ya Kibaha iliyoongoza katika matokeo hayo. Kwa kupitia kwangu kwa haraka kwa matokeo hayo, nimeiona pia Shule ya Sekondari ya Mzumbe katika nafasi ya nne kitaifa. Ilboru, Tabora Wavulana na Tabora Wasichana hazikufanikiwa kuingia kumi bora.
Sikufurahia kwakuwa nazichukia Shule binafsi, la hasha. Nimefurahi kwakuwa wadogo zetu wanaojiunga na Shule za Serikali tulikopitia kuanzia Msingi hadi Sekondari watatiwa moyo na matokeo haya na kuziamini Shule za Serikali. Wataamini kuwa hata katika shule za kiserikali kuna ufaulu endapo kutakuwa na nidhamu,juhudi na kujitoa. Kibaha wameonyesha njia, wamekuwa 'Chilongola' baada ya miaka mingi kupita.
Hongera Shule ya Sekondari ya Kibaha na hongera kwa Shule ya Mzumbe kwa kutoa mshindi wa kwanza kitaifa!
" Shule ya kibaha kuongoza kitaaifa ni matunda ya serikali ya CCM , na hii ndio CCM mpya bwana" -Alisema Humphrey Polepole.Hapo Ni matunda ya awamu ya 5! Tungefanya makosa kumchagua Edward wa Ukawa.
Huo ndo mwongozo mkuu,after that competion ndo kitu kinachofanyika chuo,..sidhani kama vyuo tena vinaweka cutoff points!!Mkuu, TCU hutoa vigezo kwa ujumla. Kila chou kina mamlaka ya kutoa vigezo vyake, bila kuviathiri vile vya TCU, kwa kila kozi