Ni ushirikina mtupu, Anaongelewa nani hapa?

Kweli una allergy na ben 8 oclock.
Alichosema ni logical reasoning tuu.yaani km kaenda kote na kapigwa bao ni mwenzie kamzidi kitu.ndio kauliza km ni kuzidiwa kwa ukaribu na devil mwenyewe.

YESU ALIKATAA MADARAKA YA
Devevil alipojaribiwa.watu hawajajifunza tuu illussion ya devil. Huyo ulijishtukia kazama sana kwa hao wazee wa hell waliomuahidi power km zilizomfikisha kk hapo bila jijua watamfikisha vilipo 8izee ccm. Kupata power na umasikini,ujinga,uchawi na najisi ktk nchi na makafara mabaya.

Wewe ni great thinker mkuu.Unajua logical reasoning ndiyo tatizo

Taifa liko katika vita dhidi ya wanaokata viungo vya binadamu kwa imani potofu za kishirikina.Kumbe kuna watu wanashindanisha u-pro wa haya mambo?Tena wabunge wasomi ambao hawaamini katika weledi wa taaluma zao katika karne hii?

Kumbe ndiyo maana hata mabadiliko ya tabia nchi hatuyatilii maanani kwa kuwa wanasiasa wengine hawaamini kwamba mvua inatokana na kulinda mazingira.Wanaamini mvua inatengenezwa kishirikina
 
Mzee wa kuwa kwamba...
Bariadi line inatisha sana. Alianza mzee wa vijisenti sasa mzee wa kujaza watu mapesa ameamua naye kufunga kazi.
 
Mzee wa kuwa kwamba...
Bariadi line inatisha sana. Alianza mzee wa vijisenti sasa mzee wa kujaza watu mapesa ameamua naye kufunga kazi.

Khaah kwani ndiye huyo?Si alikua anachuana na..Basi sitachangia tena hii thread na post zote zilizopita nakanusha.Natanguliza apology,lol
 
Haah nyinyi mnajua leo kwamba siasa za Tanzania ndumba imetawala? Ingia hivi hivi uone labda Yesu Kristo awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako ndipo utakuwa salama.
 
Kweli una allergy na ben 8 oclock.
Alichosema ni logical reasoning tuu.yaani km kaenda kote na kapigwa bao ni mwenzie kamzidi kitu.ndio kauliza km ni kuzidiwa kwa ukaribu na devil mwenyewe.

YESU ALIKATAA MADARAKA YA
Devevil alipojaribiwa.watu hawajajifunza tuu illussion ya devil. Huyo ulijishtukia kazama sana kwa hao wazee wa hell waliomuahidi power km zilizomfikisha kk hapo bila jijua watamfikisha vilipo 8izee ccm. Kupata power na umasikini,ujinga,uchawi na najisi ktk nchi na makafara mabaya.

Duh! Unaweza kuandika tena katika lugha fasaha? Hasa hiyo paragraph ya 2.
 

Alhamisi, Machi 21, 2013 07:26 Na Mwandishi Wetu


UONGOZI KAMATI ZA BUNGE

*Mbunge maarufu akutana na waganga hoteli ya Lamada
*Aulizwa, akana, amkamatisha mwandishi polisi Oysterbay


MMOJA kati ya wabunge maarufu kutokana Kanda ya Ziwa, Kambi ya Upinzani, (jina tunalihifadhi kwa sasa), ametajwa kutumia njia za kishirikina katika kuwania uongozi wa moja ya kamati za Bunge.

Mbunge huyo ambaye hata hivyo juzi alibwagwa katika kinyang’anyiro hicho, anadaiwa kufanya kitendo hicho wakati wa uchaguzi wa kamati hizo mwaka 2010 jijini Dar es Salaam, na akashinda.

Mbali na kiongozi huyo, pia uchunguzi wa Rai kupitia vyanzo mbalimbali vya habari umebaini kuwa, wanasiasa wengi nchini pamoja na watendaji waandamizi serikalini wamekuwa wakijihusisha na masuala ya ushirikina katika kulinda na kutetea nyadhifa zao.

Kundi jingine ambalo linatajwa kujihusisha na vitendo vya kishirikina ni watendaji au wastaafu ambao kwa namna moja au nyingine wamejikuta wakiwa na kesi mahakamani, hivyo kukimbilia kwa waganga kutafuta kinga kutokana na kuchanganyikiwa kunakosababishwa na madhila yanayowakabili.

Taarifa za uhakika ambazo Rai inazo zimedai kuwa, baada ya kutambulishwa kwa waganga hao, Mbunge huyo alikwenda kukutana nao katika hoteli ya Lamada iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kupata msaada ili ashinde.

Baada ya kukutana nao na kueleza ni nini alikuwa akihitaji kutoka kwa waganga hao, walikubaliana malipo na ndipo kazi ya ‘kumrekebeshia’ mambo yake ikaanza.

Masharti aliyopewa:

Kwa mujibu wa uchunguzi wa Rai, Mbunge huyo alitakiwa na waganga hao achukue karatasi na kundika yale yote ambayo alitaka waganga wayafanye, ili kufanikisha azma yake.

Katika karatasi hiyo (nakala tunayo) ikiwa na sahihi yake, Mbunge huyo pamoja na mambo mengine alitaka asaidiwe kushinda uenyekiti wa moja ya kamati nyeti za Bunge, na kuwataka wamdhuru (Mbunge kijana) aliyekuwa tishio kwake, kwa kumuandika jina.

Baada ya hapo, alichukuliwa na kupelekwa Ziwa Victoria maeneo ya Musoma ambako alivuliwa nguo na kuogeshwa maji ziwani, akavikwa shuka jeusi, kisha akapelekwa Mombasa, Kenya, ambako pia aliogeshwa maji ya Bahari ya Hindi na kufanyiwa matambiko mengine.

Baada ya kurejea Dar es Salaam akiwa ‘mzito’ kutokana na mchakato wa uganga, alishiriki uchaguzi na kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti, ingawaje hakuna uthibitisho kama alishinda kwa uwezo wa nguvu za giza 2010.

Pia kwa mujibu wa taarifa zilizopo, Mbunge huyo alitoa mamilioni ya shilingi kwa ajili ya shughuli hiyo, pamoja na kutoa fedha kuhakikisha taarifa hizo hazivuji, ambapo baadhi ya namba za akaunti alizotuma fedha Rai inazo.

Hatua alizochukua kukabiliana na Rai:

Jumapili iliyopita (Machi 17), kiongozi huyo alipigiwa simu na kuulizwa juu ya ushiriki wake katika vitendo vya ushirikina, lakini hakukubali wala kukataa, bali alimtaka mwandishi akakutane naye katika baa moja maarufu maeneo ya Masaki jijini Dar es Salaam saa 9:30 mchana, kwa ajili ya kutoa ufafanuzi.

Mwandishi alifika eneo la tukio saa 9:40 akiwa ameambatana na mtu mwingine, na dakika chache baadaye, Mbunge huyo alifika na kusaliamiana kisha kuketi pamoja.

Sekunde kadhaa baada ya mbunge huyo kukaa, walifika watu wawili ambao walikaa kwenye viti katika meza ya pembeni, na mwingine wa tatu akasimama nyuma ya mwandishi.

Baada ya watu wale wawili kuketi, mara moja walihamia kwenye meza aliyokuwapo kiongozi huyo na mwandishi, na wakajitambulisha kuwa wao ni askari polisi kutoka Kituo cha Oysterbay, na kwamba wanamuhitaji mwandishi kwa ajili ya mahojiano kituoni.

Mwandishi alitii sheria bila shuruti, na wakati wa kulipa ankara, wale polisi waligundua kuwa mwandishi hakuwa peke yake, bali aliambatana na mtu mwingine, hivyo wakasema na yule mtu mwingine pia anahitajika kwa mahojiano.

Baada ya malipo ya vinywaji kufanyika, askari watatu, mwandishi na mwenzake pamoja waliingia ndani ya gari la Mbunge huyo (namba za usajili tunazo) huku akiendesha yeye mwenyewe na kwenda kituoni Oysterbay.

Kituoni hapo, Mbunge huyo alipelekwa chumba tofauti na mwandishi, lakini polisi walipotaka kuchukua maelezo, mwandishi aligoma na kuwataka wasubiri hadi wakili wake atakapofika, jambo ambalo polisi walikubali.

Lakini muda mfupi baadaye, walikuja kumwambia mwandishi kuwa anaitwa ofisini kwa OC-CID, lakini kabla ya kumpeleka yeye na mwenzake, waliwakagua na hawakukuta chochote kile.

Baada ya kufika kwa OC-CID, mwandishi aliulizwa kwa nini amekataa kuandika maelezo, naye akajibu kuwa hajakataa, ila angependa aandike maelezo mbele ya wakili wake.

Lakini mwandishi aliwaomba polisi awape maelezo kwa mdomo ili wajue ni nini hasa kinaendelea, kwa sharti kuwa mbunge naye aitwe ili asikie nini mwandishi atawaeleza polisi.

Polisi bila ajizi, wakamwita mbunge huyo, na ndipo mwandishi akamueleza mbunge yote aliyoyafanya, jambo ambalo lilisababisha kiongozi huyo kusawajika kabisa, ilhali akikanusha kwamba hahusiki.

Baada ya hapo, akawaambia polisi kuwa yeye binafsi hana ugomvi na mwandishi, lakini alitaka mwandishi aisaidie polisi kwa kuwataja wabaya wake (waliotoa siri), ambapo baadaye mwandishi aligundua kwamba kitu kikubwa ambacho mbunge huyo alikuwa akikitaka, ni ile karatasi aliyoandikisha kwa waganga, na ndio sababu iliyofanya mwandishi na mwenzake kupekuliwa.

Sakata hilo lilimalizika kwa mwandishi kuombwa na polisi kwamba ikiwezekana asimwandike mbunge huyo, kwa sababu habari hiyo itachafua na kufuta heshima yake mbele ya jamii. Baada ya hapo mwandishi aliachiwa na kuondoka.

 

What a JOKE; Karne hii ya 21 bado tuko HUKO na UBUNGE wote huo MAENDELEO yatapatikana kweli? Na kuwa kwenye KAMATI HIZO ni ULAJI sio MAENDELEO ya Wananchi...
 
Tanzania kuna mambo kweli kama angeambiwa mkono wa albino au mguu ndo utamfanya ashinde kuwa mwenyekiti kwenye hivyo Kamati kweli asinge tekeleza hilo ?viongozi Tanzania mrudieni Mungu ushetani autatupa maendeleo yoyote
 
Haah nyinyi mnajua leo kwamba siasa za Tanzania ndumba imetawala? Ingia hivi hivi uone labda Yesu Kristo awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako ndipo utakuwa salama.

This is my best post kwa asubuhi ya Leo.Mungu akubariki sana
 
Back
Top Bottom