Ni kwanini wabunge wa CCM waendelee kung'ang'ania wakurugenzi wa miji wawe wasimamizi wa uchaguzi, licha ya hao wakurugenzi kukosa sifa?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Moja ya malalamiko makubwa kabisa ya chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema na wananchi walio wengi nchini, ni kukosoa suala la wakurugenzi wa miji kuwa wasimamizi wa uchaguzi Mkuu.

Ni jambo lililo wazi kuwa katika suala zito sana la uchaguzi Mkuu, ni lazima wanaopangwa kusimamia uchaguzi huo wawe watu waaminifu sana na watambulike kwa jamii kuwa watatekeleza "fairness" katika chaguzi hizo.

Lakini hoja hiyo inapingwa vikali na wabunge wa CCM na wanaendelea kuunga mikono kuwa hao makada wa CCM ndiyo wanaostahili kusimamia chaguzi hizo, katika mjadala wa miswada hiyo 3 iliyowasilishwa bungeni, ili hatimaye ipitishwe na kuwa sheria.

Tunatambua wazi kuwa hao wakurugenzi ni makada kindakindaki wa CCM, ambao wengi wao wameteuliwa kushika madaraka hayo, baada ya kushindwa kwenye kura za maoni ya kugombea ubunge kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Hivi itakuwaje hao wakurugenzi wasiwe "biased" katika chaguzi hizo?

Niwaulize saali dogo tu hao wabunge wa CCM, hivi kweli inaingia akilini, kwa pambano la mpira la Simba na Yanga, ukute amepangwa refa ambaye ni mshabiki kindakindaki wa timu mojawapo?

Hivi hiyo timu nyingine pinzani inaweza kukubali kuingia kwenye mechi hiyo??

Kama hao wabunge wa CCM wanajua wazi kuwa HAIWEZEKANI kabisa kwa hiyo timu pinzani kuingiza timu yao, je ni kwanini wao waamini vyama vya upinzani vinaweza kuingia kwenye uchaguzi, wakati wasimamizi (marefa) ni hao makada kindakindaki wa CCM??
 
Ccm wanataka mpaka watanzania wafe ndio wakubali suala la tume huru ya uchaguzi.
Ni dhahiri hao ma-ccm hawaitakii méma nchi hii, wao lengo lao ni kuimarisha maslahi binafsi ya chama chao tuu..........
 
Moja ya malalamiko makubwa kabisa ya chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema na wananchi walio wengi nchini, ni kukosoa suala la wakurugenzi wa miji kuwa wasimamizi wa uchaguzi Mkuu.

Ni jambo lililo wazi kuwa katika suala zito sana la uchaguzi Mkuu, ni lazima wanaopangwa kusimamia uchaguzi huo wawe watu waaminifu sana na watambulike kwa jamii kuwa watatekeleza "fairness" katika chaguzi hizo.

Lakini hoja hiyo inapingwa vikali na wabunge wa CCM na wanaendelea kuunga mikono kuwa hao makada wa CCM ndiyo wanaostahili kusimamia chaguzi hizo, katika mjadala wa miswada hiyo 3 iliyowasilishwa bungeni, ili hatimaye ipitishwe na kuwa sheria.

Tunatambua wazi kuwa hao wakurugenzi ni makada kindakindaki wa CCM, ambao wengi wao wameteuliwa kushika madaraka hayo, baada ya kushindwa kwenye kura za maoni ya kugombea ubunge kwenye maeneo mbalimbali nchini.

Hivi itakuwaje hao wakurugenzi wasiwe "biased" katika chaguzi hizo?

Niwaulize saali dogo tu hao wabunge wa CCM, hivi kweli inaingia akilini, kwa pambano la mpira la Simba na Yanga, ukute amepangwa refa ambaye ni mshabiki kindakindaki wa timu mojawapo?

Hivi hiyo timu nyingine pinzani inaweza kukubali kuingia kwenye mechi hiyo??

Kama hao wabunge wa CCM wanajua wazi kuwa HAIWEZEKANI kabisa kwa hiyo timu pinzani kuingiza timu yao, je ni kwanini wao waamini vyama vya upinzani vinaweza kuingia kwenye uchaguzi, wakati wasimamizi (marefa) ni hao makada kindakindaki wa CCM??
wew na hao unaowasemea mnapendekeza nani asimamie huo uchaguzi na lini mmeanza kuona hawafai wakati mlikua bungeni walifaaee 🐒
 
wew na hao unaowasemea mnapendekeza nani asimamie huo uchaguzi na lini mmeanza kuona hawafai wakati mlikua bungeni walifaaee 🐒

Hakuna siku waliwahi kuonekana wanafaa, na kilio kilikuwa hiki hiki, ila dhalimu magu ndio alikuja kufikisha mwisho wa uvumilivu wa tume ya uchaguzi inayowajibika kwa mwenyekiti wa ccm. Hakuna kuendelea kushiriki kwenye tume inayowajibika kwa mwenyekiti na makada wa ccm. Enough is enough. Kirahisi hivyo 🌈
 
Hakuna siku waliwahi kuonekana wanafaa, na kilio kilikuwa hiki hiki, ila dhalimu magu ndio alikuja kufikisha mwisho wa uvumilivu wa tume ya uchaguzi inayowajibika kwa mwenyekiti wa ccm. Hakuna kuendelea kushiriki kwenye tume inayowajibika kwa mwenyekiti na makada wa ccm. Enough is enough. Kirahisi hivyo 🌈
wewe kuna kitu ambacho huliliagi 🤣

my friend ulie, upasuke, inyeshe isinyeshe, ushiriki ama usishiriki mambo yanafanyika kama yalivyo pangwa.....

kwanza kadi ya kupiga kura yenyewe huna 🐒
 
Hakuna siku waliwahi kuonekana wanafaa, na kilio kilikuwa hiki hiki, ila dhalimu magu ndio alikuja kufikisha mwisho wa uvumilivu wa tume ya uchaguzi inayowajibika kwa mwenyekiti wa ccm. Hakuna kuendelea kushiriki kwenye tume inayowajibika kwa mwenyekiti na makada wa ccm. Enough is enough. Kirahisi hivyo 🌈
Tena Tindo huyo Magu, alitamka hadharani kuwa "ninakupa mshahara mzuri, nyumba na gari, halafu nisikie umemtangaza mpinzani kwenye jimbo lako, jihesabu kuwa umejifukuzisha kazi" mwisho wa kunukuu.

Hivi hao makada watiifu wa hiyo, wanawezekanaje kuaminiwa kusimamia uchaguzi Mkuu??
 
Back
Top Bottom