Sigma
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 5,006
- 1,254
Akizungumza na NIPASHE jana jioni kuhusu madai ya kufungwa kwa mgodi, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema suala hilo ni la kisheria na anachofanya Dk. Kigwangalla (Mbunge wa Nzega-CCM) ni kutafuta umaarufu wa kisiasa.
Ngeleja alisema kama kuna madai ya msingi Dk. Kigwangalla angefika ofisini kwake kuyasasilisha ili apate kauli ya serikali.
Mbunge huyu ni miongoni mwa wabunge wanaotunga sheria za nchi na yeye anazijua, lakini nashangaa anapohamasisha wananchi kuzivunja, alisema Ngeleja.
Hata hivyo, Ngeleja alisema wawekezaji wa mgodi wa dhahabu wa Golden Pride wapo kisheria na hawawezi kuondolewa kwa njia ya maandamano.
Alimtaka mbunge huyu kama ana madai ya msingi kuwasiliana angalau na Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) ili kujua kama mgodi huo una athari zozote za mazingira kulingana na madai yake.
Ngeleja alisema kama kuna madai ya msingi Dk. Kigwangalla angefika ofisini kwake kuyasasilisha ili apate kauli ya serikali.
Mbunge huyu ni miongoni mwa wabunge wanaotunga sheria za nchi na yeye anazijua, lakini nashangaa anapohamasisha wananchi kuzivunja, alisema Ngeleja.
Hata hivyo, Ngeleja alisema wawekezaji wa mgodi wa dhahabu wa Golden Pride wapo kisheria na hawawezi kuondolewa kwa njia ya maandamano.
Alimtaka mbunge huyu kama ana madai ya msingi kuwasiliana angalau na Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) ili kujua kama mgodi huo una athari zozote za mazingira kulingana na madai yake.