Ngeleja Apiga stop Maandamano Nzega ya kupinga uwepo wa Mgodi

Akizungumza na NIPASHE jana jioni kuhusu madai ya kufungwa kwa mgodi, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema suala hilo ni la kisheria na anachofanya Dk. Kigwangalla(Mbunge wa Nzega-CCM) ni kutafuta umaarufu wa kisiasa.
Ngeleja alisema kama kuna madai ya msingi Dk. Kigwangalla angefika ofisini kwake kuyasasilisha ili apate kauli ya serikali.
Mbunge huyu ni miongoni mwa wabunge wanaotunga sheria za nchi na yeye anazijua, lakini nashangaa anapohamasisha wananchi kuzivunja, alisema Ngeleja.
Hata hivyo, Ngeleja alisema wawekezaji wa mgodi wa dhahabu wa Golden Pride wapo kisheria na hawawezi kuondolewa kwa njia ya
maandamano. Alimtaka mbunge huyu kama ana madai ya msingi kuwasiliana angalau na Baraza la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) ili kujua kama mgodi huo una athari zozote za mazingira kulingana na madai yake.

Sigma, KTY Waziri Ngeleja hayuko katika nafasi yoyote ile kupinga Maandamano! Haya locus yoyote ile kwa kweli.

Na kauli yake imenishangaza sana. Hususan anaposema Mbunge na wananchi wanavunja sheria, sheria ipi? Sidhani kama yeye kwa utaalamu wake kisheria au hata uzoefu wake tu anaweza kusema kama alivyosema. Kusema kwamba eti kufanya maandamano ya amani ni kuvunja sheria ni upotofu wa hali ya juu!

Nadhani Mwandishi wa NIPASHE alimnukuu Waziri wetu vibaya au basi Waziri alikuwa amechoka sana na kazi siku hiyo, ukizingatia ilikuwa Ijumaa!
 
Kigwangala kweliumedhamiria? hvi unafahamu kuwa serikali ya kijiji kinachozunguka mgodi walisainiana mkataba na mgodi kuhusu kupewa hudumaa za kijamii? je nani anafuatilia utekelezaji huu, mimi ninatarifa za kina kuwa jambo hili siku hizi halitekelezeki, unajiamini na upo pamoja katika mapambano dhidi ya mafisadi hata kwa gharama yoyote, jitokeze unijibu kwani kwa sasa ninatafakari kulifikisha suala hili kwa CHADEMA

@Miradibubu, hizo taarifa ninazo japokuwa kuna afisa mmoja alifanya ghiliba akauiba mkataba baina ya mgodi na serikali ya kijiji cha Lusu na hivyo wazee wale wa kijijini hawana nyaraka yoyote ile na ni miongoni mwa watu wa Nzega wenye hasira na mgodi, maana mgodi waliahidi kuwatekelezea mambo mengi halafu wakafanya usanii wakakimbia mpaka leo hawajafanya lolote! Ila kama unazo nyaraka tuwasiliane hapa: mbunge.nzega@gmail.com na uniletee hizo nondo tuongeze nguvu kwenye hoja yetu!

Wala usihofu kuhusu azma yangu kwenye hili au msimamo na uwezo wangu kwenye kufuatilia issues...siogopi, sichoki mpaka kieleweke!
 
Bora wandamane tu sehemu za migodi zinatakia zionekane kwa kulingana na thamani ya eneo husika sio vijiji vyenye migodi vinakuwa nyumaaa kimaendeleo
 
Ha ha ha Kigwangala hiyo ndiyo CCM lazima wakukabe koo,uwe ndani ya hicho chama utetee wananchi subiri ni imani yangu wanakuhesabia wakuchakachue.Hicho ni chama cha maslah binafsi.
Sina shaka na wewe kwani najua ulivyoongoza mgomo wa madaktari Muhimbili kudai maslahi yao ila wasiwasi wangu ndani ya chama hicho cha ghilba ambacho hakijali tena maslahi ya wengi jitihada yako haita fika mbali.


Watu wa namna hii sisiem wanawaona kama watoto wanaotaka kumpiga changudoa wa baba yao.Lazima watamwambia huna adabu!!. ulitakiwa uwaambie wazee na siyo kumchungulia baba yako moja kwa moja. Mara utishiwe na laana lukuki.
 
@Miradibubu, hizo taarifa ninazo japokuwa kuna afisa mmoja alifanya ghiliba akauiba mkataba baina ya mgodi na serikali ya kijiji cha Lusu na hivyo wazee wale wa kijijini hawana nyaraka yoyote ile na ni miongoni mwa watu wa Nzega wenye hasira na mgodi, maana mgodi waliahidi kuwatekelezea mambo mengi halafu wakafanya usanii wakakimbia mpaka leo hawajafanya lolote! Ila kama unazo nyaraka tuwasiliane hapa: mbunge.nzega@gmail.com na uniletee hizo nondo tuongeze nguvu kwenye hoja yetu!

Wala usihofu kuhusu azma yangu kwenye hili au msimamo na uwezo wangu kwenye kufuatilia issues...siogopi, sichoki mpaka kieleweke!


Pongezi kwa sana Mh. kwa kuwa out of box la uzandiki na unafiki.

Mungu atakupigania tu pale utakaposimamia haki ila ukienda kinyume atakuacha na ndo mwanzo wa mafisadi kukuondoa kama walivyomfanya Lukas Saleli
 
Dr, good job. We tafuta umaarufu kama wakati muafaka kama huu unajitokeza. Huo ni umaarufu mzuri hivyo usiachie nafasi hiyo.
 
Back
Top Bottom