NECTA yatangaza upya Matokeo ya Kidato cha Nne 2012

The government nullified form four national Examination results of 2012, I think this is for the interest of few(politician). Once you send raw material with low quality to the industry,expect to get poor,poor product.
 
Sio research kama umezoea neno la KUHAKIKISHA-wa kwangu alipata p28-sasa hivi hajabadilika kitu ni ilele,kama unataka kuhakikisha sema nikutumie namba.Hii ni Machungu zaidi ya kwanza-Watanzania mahakama gani inafaa kwenda kwa hili?!!!!!
 
Serikali inachukulia watu wote ni wajinga wasijue tunaelewa kila kitu kinachoendelea huko,hakuna mabadiliko yyte yaliyofanyika pengine ni kwa wachache wenye wajomba na baba wakubwa au mashangazi serikalini ndo waliofaidika lkn napo faida cjaiona cozi watapatika wafaulu wengi katika kundi la wajinga utakua umeokoa nn hapo au ni sifa tu za kuwa na 1 nyingi kimuonekano lkn kiundani mbumbumbu
 
Mimi sijivunii kuona wamafunzi waliofeli wakifaulishwa kwa sababu za kisiasa. Hebu fuatilia mnyororo huu wa namna tunavyoandaa Taifa lisilowajibika kwa kuchukua mfano wa hawa vijana

2002: Walianza darasa la kwanza. Ada ya shule ya msingi ilifutwa: Bahati iliyoje
2005: Wako darasa la nne. Mitihani ya kwenda darasa la tano ilifutwa. Wakapita mpururo
2010: Wakiwa form two. Mitihani ya form two haikuwa kigezo cha kuwapeleka kidato cha tatu
2012: Matokeo yalikarabatiwa ili waonekane wamefaulu

Sasa kama watangulizi wao ambao hawakuwa na "bahati" kama hizi wameweza kujenga maghorofa yakaporomoka, wakafanya makandarasi wa kujenga barabara waazimwe kutoka China/Ujerumani/Japan, wataalam wa fedha waazimwe kutoka Ulaya/Marekani, wakapasua vichwa badala ya miguu na kuwafanya akina Mwandosya, Zito Kabwe na Mwakyembe wakakosa imani nao na kwenda kutibiwa India; hebu tujiulize swali hili kubwa

Watakapofika chuo kikuu na kuendelea na "bahati" hii, hivi hatuoni kwamba itatwezekana sasa tukaandaa madaktari watakaoweka mioyo ya kuku kwa binadamu na kujenga magorofa kwa mabua?

Hebu jamani tuangalie mustakhbar wa Taifa badala ya kufurahi "miteremko" hii inayoletwa na wanasiasa

Inawezekana nikaudhi watu lakini uzalendo umezingatiwa

Chas Mike
 
Heri ya wale waliofaulu kwa haki ambao nafsi zao zinayafahamu matokeo yanayowapa pia Ole wao wale waliopata nafasi
kimabumashi kwani huko mbeleni hawatakuwa na bahati hiyo ya mtende kuota jangwani kwani Taifa litaangamia kwa kukosa maarifa, hakuna tabu kwani kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani.
 
kiukwel kama ndo hiv taifa linaangamia.ilibid baraza waoneahe msimamo tena msimamo thabit.kwa hil hapaaaaaaaaana! wamechemka.
 
jaman mbona cku za kwenda shule ndo zinasogea lakn wa2 hatujui 2naenda shule gan!,post zatatoka lin jaman!?au hamna kwenda advance kwa waliomaliza 4m4 2012?
 
Matokeo yakimagumash hamon aibu, bado mnapga kelele kuhs post mcwaze mnaweza vukishwa six xo kuwen kmya 2 wajomba!@mc shanex@
 
SERIKALI ni dubwana flani la ajabu sana,eti halioni hata njia linakoelekea,jamani? majanga!! huku chuo kikuu ndo kuna vichwa maji mpaka unaweza ukajiuliza tatizo ni nini?,mi niko chuo kikuu TEOFILO KISANJI,MBEYA,lakini mambo ya huku ni masikitiko makubwa.sijui hawa watu walipitishwa kivipi mpaka kufika huku.wengi hawajitambui.majanga!
 
Back
Top Bottom