Ndugulile: Magufuli hajui sheria, anakurupuka tu...

Nadhani alitaka kusema SUMATRA ambayo ina deal na surface and marine transport.

Ingawa pia tumeelezwa hapa kwamba waziri ana mamlaka kisheria kuongeza nauli ya kivuko.
Nadhani hapa ndipo kuna mkorogano, nani ni nani kwa sheria gani!
SUMATRA ni mamlaka iliyo chini ya Serikali kudhibiti vyombo vyote vya majini na nchi kavu vinavyomilikiwa na mashirika ya umma na binafsi na siyo EWURA! Hivyo nauli ya vyombo hivi hupangwa na SUMATRA

Kuhusu vivuko vya Kigamboni na vile vilivyomo katika maeneo mengine vinamilikiwa na Wakala wa Serilkali yaani TEMESA na hivyo mamlaka ya kuvidhibiti ni Wizara ya Ujenzi. Hivyo nauli za vivuko hivi unapangwa na Wizara moja kwa moja na si SUMATRA.

KInachogomba hapa ni kauli ya kibabe na kuwadharau wabunge wenzake ya MHe. Magufuli. Na hii ni tabia yake hata katika sherehe nyingine za kiserikali anapokuwa anawakaribisha wakubwa wake wa kazi kuzindua miradi ambayo iko katika majimbo yaliyo chini ya wapinzani hutoa maneno ya kejeli kwa wapinzani na viongozi wake wanabaki kukenua meno tu! Ni vizuri Rais na Waziri Mkuu waanze kumkemea ili kukomesha tabia hii
 
Live Channel Ten Mbunge wa Kigamboni Anamuumbua live Live Magufuli na Wazara yake kuwa Hawana haki ya kuongeza Nauli Mpya kwani hiyo mamlaka amaepewa EWURA tena lazima Wadau washirikishwe...

Kasema nini? na yeye kafanya nini?
Kama ni hivyo , basi huko kukurupuka ni sehemu ya Ilani wanayoitekeleza.
 
Naomba mwenye uelewa na haya mambo atusaidie, Energy and Water Utilities Regulatory Authority inaingiaje hapa? Au ile WATER inamaanisha na boti, vivuko, kambale nk.
ninavyoelewa mamlaka yanayohusiana na vivuko ni WAKALA WA UFUNDI NA UMEME (TAMESA) ndio wanaongia hapo.
 
Live Channel Ten Mbunge wa Kigamboni Anamuumbua live Live Magufuli na Wazara yake kuwa Hawana haki ya kuongeza Nauli Mpya kwani hiyo mamlaka amaepewa EWURA tena lazima Wadau washirikishwe...

Naona Dr. kwa Dr. wanaumbua dah kazi ipo
 
Watanzania sometimes lazima tujilaumu, kile kivuko kinavukisha watu wangapi kwa siku?
Nina uhakika kinaweza kuingiza milioni 20 kwa siku, ukitoa gharama unaweza kupata 5-10m a day by just charging 100.
Something is wrong somewhere.

Milioni 20 ni sawa na litre 10,050 kwa bei ya sasa. Kivuko kina fanya kazi kuanzi saa 10 alfajiri hadi 7 usiku..unafaham kinatumia litre ngapi? Ukiweka na maintenance na gharama nyinginezo?
 
tuwe wahalisia, hivi sh. mia sasa hivi unaweza kununulia nini? Hata Andazi linauzwa sh. Mia mbili, leo hii nauli unataka iwe sh. mia!
 
tuwe wahalisia, hivi sh. mia sasa hivi unaweza kununulia nini? Hata Andazi linauzwa sh. Mia mbili, leo hii nauli unataka iwe sh. mia!

inasikitisha kuona wananchi wenye uwezo wa ku reason, wana Opt kuwa mizigo.
Au Wanadhani kuishi kigamboni we are vanurable and so entitled to Dezo.?
Ngoja waarabu wasikie kuwa kuna watu wanalilia bure.
Camerun ameshapata taarifa kupitia kwa prince Charles alipokwenda kule, hivyo wanachofanya ni kukumbushia tu, wala Magufuli siyo lengo lao bali kisingizio.
 
Napenda Kutoa Shukrani zangu kwa dhati kwa wabunge wa mkoa wa Dar es salaam katika kupigania haki za mwananchi na katika shughuli zao za kila siku za kuwaletea wananchi maendeleo....!

Niwapongeze sana kwa umoja wao bila kujali itikadi au chama! lakini huo ''UMOJA'' unanitia shaka...,inavyoonyesha there is something behind kuhusu huo umoja wa mnyika,mtemvu,iddi azzan, na ndugulile
pamoja na wabunge wengine

Dar es salaam Kumekuwa na majanga mbalimbali kama mabomu gongo la mboto,mafuriko ya juzi kati na matatizo ya kila siku kama usafiri hususani fulani,uchafu wa jiji na mambo mengi ya msingi ambayo yamekuwa ni kama kidonda sugu kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam! Hivi mbona Hamjawahi kukaa pamoja na huo umoja wenu kuongelea matatizo ya jiji la Dar es salaam zaidi ya kumsema mtu kama mnatumiwa na mtu flani hivi huku mkipata sapoti kubwa ya waandishi wa habari...!

Napenda nihoji Huo Umoja wenu mbona hamkukaa pamoja kutolea Tamko mafuriko ya Jangwani au mabomu gongo la mboto! ambayo ni matatizo ya msingi yaliyowakabili wananchi zaidi ya kukaa kikao na kumsema Masaburi Na hivi leo Mmetoa tamko la Pamoja Kumsema Magufuli...,Mnatumwa na nani? Ndio maana Masaburi aliwaambia Tumieni Akili Kufikiri na Sio *&(&*...

Umoja wenu unanitia shaka! kana kwamba vile mnatumiwa kisiasa kumwangamiza mtu flani...,na sio kuongelea matatizo ya wananchi nashangaa sana kuhusu suala la Magufuli mlivyolivalia Njuga! wakati kuna matatizo ya msingi

Kweli umoja wa wabunge jiji la Dar es salaam unanitia shaka
 
Live Channel Ten Mbunge wa Kigamboni Anamuumbua live Live Magufuli na Wazara yake kuwa Hawana haki ya kuongeza Nauli Mpya kwani hiyo mamlaka amaepewa EWURA tena lazima Wadau washirikishwe...

EWURA? Mbona sipati concept hapa, EWURA na kivuko cha kigamboni wapi na wapi?
 
Au wakati ule hao wabunge walitaka kujiongezea posho ya kufanya kazi yao ya kawaida hadi ifike 200,000/- kwa siku ili wapate pesa ya kulipia kuvuka hadi Kigamboni?

Anyway, ni vp hao wabunge wapo kimya kuhusu mambo ya maana, mfano:
1. Mfumiko wa bei uliotoka 4% wakati serikali ya Kikwete ikiingia madarakani hadi 20% ya sasa,
2. Kupanda bei ya mafuta (petroli/dizeli) ambazo huongeza gharama za usafiri na usafirishaji, na hatimaye kuongeza bei ya bidhaa, mikataba ya kifisadi,
3. Wananchi kutoshirikishwa kutoa maoni kuhusu katiba mpya (baada ya kuiandika kwa kiswahili),
4. Ufisadi...
 
Live Channel Ten Mbunge wa Kigamboni Anamuumbua live Live Magufuli na Wazara yake kuwa Hawana haki ya kuongeza Nauli Mpya kwani hiyo mamlaka amaepewa EWURA tena lazima Wadau washirikishwe...

EWURA???
Mbunge amechemka big time...
 
busara ZA MNYIKA HAPO SIZIONI
yeye alipokuwa na hoja za kudhibiti bei za vyakula
hakuna mbunge wa ccm aliemuunga mkono
sasa na yeye anakubali kutumika 'kumuangamiza magufuli'
 
busara ZA MNYIKA HAPO SIZIONI
yeye alipokuwa na hoja za kudhibiti bei za vyakula
hakuna mbunge wa ccm aliemuunga mkono
sasa na yeye anakubali kutumika 'kumuangamiza magufuli'

Hao wabunge wa CCM ndiyo wameingia mkekenge. Kijana anwaingiza mjini, CCM kweli ni sikio la kufa....... hii issue itawaletea mgogoro mkubwa wasipoangalia by then Mnyika hatakuwepo..... Watakapokwenda kusitakiana na kuyajadili ndani ya chama kama wanavyopenda kusema!!

Nafikiri anachokifanya Mnyika ni kusaidia kuchochea mgogoro ndani ya CCM!!
 
Back
Top Bottom