Nchi za Magharibi zatiwa wasiwasi na hasira na kuongezeka kwa ushawishi wa China barani Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG31N1228090495.jpg

Likiita Afrika "bara lisilo na matumaini" na kushangilia uvamizi wa Marekani nchini Iraq, jarida la The Economist la nchini Uingereza limekuwa halifichi mantiki yake ya "Eurocentrism" na "ukuu wa wazungu". Hivi karibuni, mfululizo wa ripoti zilizotolewa na jarida hilo "China barani Afrika" kwa mara nyingine tena zilitumia mtazamo huo finyu kueleza wasiwasi na ushawishi wa China barani Afrika na jaribio lake la kudhoofisha ushirikiano kati ya nchi zinazoendelea.Wasomi wa Afrika wamesema ushawishi wa China unaoongezeka barani Afrika unazitia wasiwasi nchi za Magharibi.

Kwanza kabisa, matokeo ya tafiti zilizotumiwa kwenye mfululizo wa ripoti hizi nyingi zimefanywa na nchi za Magharibi, zikinukuu tu maudhui ya kitabu kilichochapishwa na msomi wa Afrika nchini Uingereza, na hakuna kabisa vyanzo vya Kichina. Hebu fikiria, ikiwa mwandishi wa habari wa China aliandika ripoti juu ya "nchi za Magharibi barani Afrika", na tafiti nyingi zilizotajwa zilikuwa kutoka China, sijui kama makala kama hiyo itaeleweka. Vilevile tofauti na tukio moja moja la wachina wanaovunja sheria ambayo waandishi wanataja katika makala, kuna ushahidi mwingi za unyonyaji wa kikoloni na vitendo vya ufisadi vya biashara vya makampuni ya Magharibi barani Afrika vinavyoendelea kwenye sekta ya mafuta, gesi, biashara ya madini, mawasiliano ya simu, na nyanja nyingine nyingi. Cha kusikitisha ni kwamba, nchi nyingi za Magharibi na vyombo vya habari vinaendelea kuelezea sera zao za Afrika kama zinapiga hatua na kuwa endelevu.

Pili, pengine siku hizi ni vigumu sana kupata wataalam na wasomi wenye mtazamo hasi kuhusu uhusiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya China na Afrika. Wanaripoti wa jarida la The Economist hawana budi kutumia njia ya “kupandikiza” na kuunganisha maneno ya mtaalam na mtazamo wake binafsi. Kwa mfano, mwanaripoti anapouliza kimakusudi “kama uwekezaji wa China umesababisha ongezeko la ufisadi nchini,” mwanauchumi wa Kenya David Ndii anaweka lawama zaidi kwa wanasiasa nchini Kenya. Lakini baada ya sentensi hii, mwandishi anamnukuu eti mwanadiplomasia wa nchi za Magharibi "ambaye hajatajwa jina" akisema kwamba China imesababisha "kuporomoka kimfumo" barani Afrika. Kwa wazi, uchambuzi huu potofu ndio ishara inayoonekana zaidi kwenye mtazamo finyu walio nao wachambuzi wengi wa nchi za Magharibi katika kuutazama uhusiano wa China na Afrika. Hata hivyo, watu wasisahau kwamba katika miongo kadhaa iliyopita, nchi kama Canada na Ufaransa zilidhibiti rasilimali ya madini ya nchi za Afrika, na Marekani ilisaidia au hata kushiriki moja kwa moja katika mapinduzi ya kisiasa katika nchi nyingi za Afrika. Tumesikia wanadiplomasia wengi wa nchi za Afrika wakitoa tuhuma dhidi ya nchi za Magharibi za matamshi matamu au ya kulazimisha ili kupata kura kwenye Umoja wa Mataifa.

Koffi Kouakou, mtafiti mwandamizi wa Kituo cha Utafiti wa Afrika na China katika Chuo Kikuu cha Johannesburg, Afrika Kusini hivi karibuni alitoa makala akinukuu sentensi ya "hakuna nchi iliyo karibu na kina na upana wa ushiriki wa China katika Afrika" iliyotajwa kwenye makala ya The Economist, akisema katika suala la ushawishi, China tayari iko mbele, na hali ni nzuri kwa China sasa na katika siku zijazo. Hivi sasa China ni mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara barani Afrika, na makampuni ya China yamechangia moja ya nane ya pato la viwanda barani humo. Asilimia 70 ya mitandao ya 4G barani Afrika inajengwa na makampuni ya China. Wakati huo huo, takwimu zinaonyesha kuwa, kama chanzo muhimu cha uwekezaji wa miundombinu barani Afrika, kupitia pendekezo la China la "Ukanda Mmoja, Njia Moja", nchi za Afrika kwa kawaida zinaweza kujenga barabara, madaraja na reli ndani ya miaka 2.8, wakati Benki ya Dunia inahitaji miaka tisa. Kinyume chake, mpango wa Marekani wa Kujenga Dunia Bora zaidi B3W na mradi wa miundombinu ya lango la kimataifa wa Umoja wa Ulaya imesalia kuwa mipango tu.

Jarida la The Economist linamalizia mfululizo wa ripoti hizo kwa kauli hii: “nchi za Magharibi lazima ziongeze juhudi zake ili kuzipa nchi za Afrika njia mbadala za China.” Hali halisi ni kuwa waafrika si jinsi wanavyofikiria watu wa Magharibi. Kwa kuona kwamba Afrika sasa inaanza kustawi, nchi za Magharibi zinataka kunufaika na mafanikio yake. Hii kwa kweli si busara, na ni uamuzi wa Afrika kuchagua nani wa kushirikiana naye.
 
Hivi vita vya kiuchumi kwa maana wanajua Africa ni bara la kuvuna rasilimali zao...yaaani
 
Back
Top Bottom