Biashara kati ya China na Afrika inazidi kukosa uwiano? Ukweli uko hapa

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111322968403.jpg


Kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa na Wizara ya Biashara ya China, jumla ya biashara kati ya China na Afrika iliongezeka kwa 1.5% mwaka 2023 kuliko mwaka 2022, na kufikia rekodi mpya ya kihistoria ya dola za Marekani bilioni 282.1. China imekuwa mwenzi mkubwa zaidi wa kibiashara barani Afrika kwa miaka 15 mfululizo. Wakati huohuo, vyombo vingi vya habari vya Afrika pia vimegundua kuwa pengo la biashara kati ya Afrika na China limeongezeka hadi dola bilioni 64 za kimarekani kutoka dola bilioni 46.9 mwaka 2022.

Kinachostahiki kufahamika kwanza ni kuwa, ikiwa ni jiwe kuu la msingi na kichocheo cha uhusiano kati ya China na Afrika, kiwango cha biashara kati ya China na Afrika kimeendelea kuweka rekodi katika miaka 15 iliyopita, hali hii inaonyesha kwamba ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya pande hizo mbili umekuwa na uhai wenye nguvu. Mwaka 2023, wakati kiwango cha biashara duniani kilipungua kwa 5% kuliko mwaka 2022, kiwango cha biashara kati ya China na Afrika kiliweza kukua kwa 1.5% - kikiwa juu ya kiwango cha ukuaji wa 0.2% cha biashara ya nje ya China mwaka jana, na hii inaonyesha ustahimilivu mkubwa wa biashara kati ya China na Afrika. Pia, muundo wa biashara kati ya China na Afrika unaendelea kuboreshwa. Mwaka 2023, uagizaji wa China wa karanga, mboga na maua kutoka Afrika uliongezeka kwa 130%, 32% na 14% mtawalia, huku usafirishaji wa magari mapya ya nishati, betri za lithiamu na bidhaa za jua za China barani Afrika ukiongezeka kwa 291%, 109%, na 57%, na kusaidia mabadiliko ya nishati ya kijani barani Afrika.

Tatu, kutokana na athari kama vile mgogoro wa Russia na Ukraine, machafuko katika Mashariki ya Kati, na kupanda kwa kiwango cha riba cha dola za Marekani, bei ya bidhaa za maliasili imeshuka duniani kote katika mwaka 2023, na Afrika nayo pia haikunusurika. Kwa mfano, China ni muagizaji muhimu wa madini ya kobalti kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Bei ya wastani ya kobalty kwa tani mwaka 2022 ilikuwa dola 63,700 za Marekani, lakini hadi mwisho wa mwaka wa 2023, bei yake ilikuwa imeshuka hadi chini ya dola 30,000. Maliasili ni bidhaa muhimu zinazouzwa nje kwa nchi za Afrika. Ni hali halisi ni kwamba uwiano wa biashara ya nje barani Afrika bado unategemea kwa kiasi kikubwa bei ya maliasili. Hata kama kiwango cha biashara kitabakia bila kubadilika au hata kuongezeka, mapato ya biashara ya Afrika pia yanaweza kupungua. Ni kwa sababu hii kwamba pengo la biashara kati ya Afrika na China liliongezeka mwaka jana.



Kwa kweli, ili kupunguza pengo la biashara lililopo kati ya China na Afrika, China imefanya jitihada mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kufungua "njia ya kijani" kwa mauzo ya nje ya bidhaa za kilimo za Afrika, na kusaidia bidhaa za Afrika kuingia katika soko la China na la kimataifa kupitia majukwaa kama vile Maonyesho ya Kimataifa ya Uagizaji Bidhaa ya China, Maonyesho ya Uchumi na Biashara ya China na Afrika. Hadi sasa, nchi 27 za Afrika zimenufaika na sera ya China ya kutotoza ushuru kwa asilimia 98 ya bidhaa. Hili ni dhihirisho la uhusiano wa kirafiki kati ya China na Afrika, na ni hatua ya kuendeleza uchumi wa Afrika, kusaidia Afrika kukuza uwezo wake wa uzalishaji na kukuza uchumi mseto wa Afrika.

Wakati wa Mkutano wa kilele wa BRICS uliofanyika mjini Johannesburg Agosti mwaka jana, Rais Xi Jinping wa China aliwaambia viongozi wa Afrika kwamba China itaendelea kuongeza juhudi zake za kurekebisha kukosekana kwa uwiano wa biashara, ikiwa ni pamoja na kuzisaidia nchi za Afrika kuzalisha chakula zaidi na kuanzisha viwanda vya usindikaji barani Afrika. Hata hivyo, kutatua tatizo la kukosekana kwa uwiano wa biashara haitakuwa ndani ya muda mfupi, na China na Afrika bado zinahitaji kufanya kazi kwa bidii ili kupata uwiano katika biashara, kwa mfano, kutengeneza bidhaa zenye ushindani na endelevu badala ya kuuza nishati na madini tu.
 
Back
Top Bottom