Ziara ya Wang Yi barani Afrika na Amerika ya Kusini yaonyesha uhusiano wa kirafiki wa China na nchi nyingine za Kusini

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
1706076805571.png

Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, alifanya ziara barani Afrika na Amerika ya Kusini, ikiwa ni ziara yake ya kwanza nje ya nchi kwa mwaka 2024. Imekuwa ni desturi kwa Waziri wa Mambo ya Nje ya China kufanya ziara yake ya kwanza ya mwaka mpya katika bara la Afrika, desturi ambayo imedumu kwa miaka 34. Katika ziara ya mwaka huu, mara baada ya kutoka Afrika, Wziri wa Mambo ya Nje wa China, Wang Yi, alifanya ziara katika kanda ya Amerika ya Kusini, jambo ambalo linaonyesha jinsi China inavyotilia maanani uhusiano wa nchi nyingine za Dunia ya Kusini.

Wataalamu nchini China wanasema, uratibu wa karibu zaidi wa nchi za Kusini utasaidia kujenga mandhari ya usawa zaidi na tulivu ya dunia, jambo ambalo ni muhimu katika hali ya utatanishi inayoonekana katika dunia ya sasa.

Akizungumza wakati alipokutana na Waziri Mkuu wa Jamaica Andrew Holness, Wang Yi alisema China inatarajia kushirikiana na Jamaica kuongeza nguvu ya mikakati ya maendeleo, kupanua ushirikiano katika nyanja mbalimbali, kuboresha mawasiliano ya kitamaduni na kati ya watu na watu, na kuweka msingi imara wa maoni ya umma kuhusu urafiki kati ya nchi hizo mbili.

Naye Bw. Holness alisema, China haikusita kuisaidia Jamaica pale nchi hiyo ilipokumbwa na changamoto, pia imeunga mkono kithabiti maendeleo ya kiuchumi ya Jamaica na kuboresha maisha ya watu wa huko, hatua iliyoonyesha kwa wazi kabisa nia ya kweli ya China ya kuzisaidia nchi nyingine zinazoendelea.

Wang Yi alitembelea Jamaica baada ya kumaliza ziara yake nchini Brazil, ambako alikutana na rais wa nchi hiyo, Luiz da Silva na kufanya mazungumzo naye kuhusu uhusiano wa kina wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili. Pande hizo mbili zilisaini makubaliano ya kurahisisha upatikanaji wa visa ili kupanua zaidi mabadilishano ya wataalamu kati ya nchi hizo mbili.

Jamaica ilikuwa kituo cha mwisho cha ziara hiyo ya kwanza ya Waziri wa Mambo ya Nje ya China, baada ya kumaliza ziara katika nchi za Misri, Tunisia, Togo na Cote d’Ivoire za barani Afrika.

Kuimarisha ushirikiano na nchi nyingine zinazoendelea daima imekuwa ni kipaumbele cha sera ya China, ambayo inajitahidi kuratibu vizuri ushirikiano na nchi hizo ili kutimiza mandhari endelevu, yenye afya, na uwiano ya diplomasia duniani.

Wang Yi anasema, viongozi wa nchi za Afrika ambako alifanya ziara yake kwa mwaka huu, walisisitiza ahadi ya kuheshimu kanuni ya kuwepo kwa China Moja. Amesema linapokuja suala la maslahi makuu ya China, nchi za Afrika zimeonyesha msimamo thabiti na wa wazi, unaodhihirisha utamaduni mzuri wa kuungana mkono kati ya China na nchi za Afrika.

Profesa Li Haidong wa Chuo Kikuu cha Masuala ya Kigeni cha China, amesema maridhiano ya nguvu katika maslahi makuu ya kila upande na katika masuala ya kimataifa, ni msingi mkuu wa uhusiano wa China na nchi nyingine zinazoendelea. Akitolea mfano suala la Taiwan, Li amesema, nchi nyingi zinazoendelea zinasimamia kithabiti kanuni ya kuwepo kwa China moja, huku nchi chache, ambazo ziko tayari kutumika na Marekani, daima zinatafuta mvutano na China kuhusu suala hilo. Amesema ni muhimu kwa nchi za Dunia ya Kusini kushikilia msimamo wao kuhusu suala la Taiwan, na kuweka wazi kwa nchi za Magharibi kuwa, kufuata kanuni ya China moja ni maafikiano yaliyopo na kwamba uingiliaji wowote ama uchochezi katika Mlango Bahari wa Taiwan na nchi hizo za Magharibi haukubaliki.

Profesa Li pia anasema, nchi nyingi zinazoendelea zinavutiwa na Pendekezo la China la Ukanda Mmoja, Njia Moja (BRI), na mapendekezo mengine mengi ambayo amesema yanaunganisha nchi za Kusini kwa karibu zaidi na yanasaidia kuendeleza mipango yao binafsi ya maendeleo. Kutokana na hayo, ushirikiano na uhusiano kati ya China na nchi nyingine zinazoendelea ni wa kunufaishana, kuungana mkono, na kusimamia na kutetea maslahi yao ya pamoja.
 
Back
Top Bottom