Duh... Hii thread imefika kikomo??
Lete MkuuHaijafika kikomo kaka na ni kitambo sana.
Sasa nipo likizo kesho nitajitahidi tuendelee mpaka panapotakiwa.
Sawa mkuu tupo pamojaHaijafika kikomo kaka na ni kitambo sana.
Sasa nipo likizo kesho nitajitahidi tuendelee mpaka panapotakiwa.
Ha ha, hamna haja ya nguvu mkuu. Nakaribisha maswali ama hoja alafu tujadili kwa pamojaHizi nondo vipi wakuu, Kabaunyeri na The Emperor mmetuacha na Kiu, tunaomba mzilete wenyewe kwa hiyari ama sivyo tutatumia nguvu.
Asante mkuu mimi nilitaka kujua ilikuwaje Urusi pamoja na uwezo wake mkubwa wa Kijeshi akashindwa huko Afghanistan,na pia Marekani kushindwa huko VietnamHa ha, hamna haja ya nguvu mkuu. Nakaribisha maswali ama hoja alafu tujadili kwa pamoja
Asante mkuu mimi nilitaka kujua ilikuwaje Urusi pamoja na uwezo wake mkubwa wa Kijeshi akashindwa huko Afghanistan,na pia Marekani kushindwa huko Vietnam
Tuendelee tuendelee mkuuHivi vita ulivyovitaja hapo juu naweza sema vinafanana hasa ukiangalia sababu za kuanza kwake na matokeo yake baada ya kuisha yani kushindwa kwa mataifa hayo makubwa.
Kwanza tuanze na kusema kuwa baada ya vita vya pili vya dunia, U.S na U.S.S.R waliibuka washindi na hivyo kupelekea kuwa superpowers pekee duniani (kijeshi na kiuchumi). Lakini hawa jamaa walikuwa na itikadi tofauti sana hasa katika muonekano mpya wa kisiasa na kiuchumi duniani. Wamerekani walihubiri ubepari na wasoviet walihubiri ukomunisti. Kila mmoja aliamini kuwa mfumo wake ndio zitawezesha kuinua upya uchumi wa kidunia (mana vita viligharimu nchi nyingi sana kifedha, watu na mali). Hii tayari iliweka uhasama mana wote wababe na hakuna aliyekubali kushindwa. Kilichofuata hapo ni nani ataweza kushawishi nyingi zaidi zimuunge mkono katika hizo sera zake. Pia baada ya kulipuliwa kwa mabomu ya kiatomiki huko Japan, warusi walitia jitihada kubwa na hatimaye waliweza kutengeza ya kwao. Hii ndio mwanzo wa COLD WAR. Hii ilipelekea nchi ndogo hasa Africa, Asia na Amerika ya kusini kuwa katika hali flani ya tutoke vipi maana wasoviet wanakuja na sera zao na ahadi kibao, na hapo hapo warekani nao wanakuja na sera zao na ahadi kibao. Hii ilileta kuibuka vikundi na vuguvugu la kisiasa na kutetea sera tofauti na mara nyingine demokrasia iliposhindikana basi watu waliingia mwituni. Sababu kubwa ya kuchagua ipi ni ipi ilitofautiana nchi na nchi, historia ya taifa husika, jiografia na tamaduni za watu wake. Kumbuka pia mataifa mengine makubwa nayo tayari yalishachagua pande zao mapema kama China, Japan, Western Europe karibu nchi zote n.k. Pia hawa wababe walitumia mbinu kadhaa kutekeleza hiyo mipango yao kwa wale wabishi hata kupindua serikali na kuweka watu wao (puppet governments).
Much respect Emperor kwa Elimu