Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
CCM tangu kuanzishwa kwake imekuwa na desturi ya kuongozwa na Mwenyekiti wa Taifa ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jambo hilo limetokea kwakuwa CCM imekuwa ikishinda kwenye uchaguzi na kutoa Rais.
Hayati Mwalimu Nyerere alikuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa. Mzee Ali Hassan Mwinyi alikuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa. Utamaduni na utaratibu huo ulimhusu pia Rais Mstaafu Mzee Benjamin Mkapa. Hata sasa,Rais Jakaya Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.
Uenyekiti wa Rais Kikwete unakoma mwaka 2017 kwakuwa alichaguliwa mwaka 2012 kwa mara ya pili ya miaka mitano. Sasa,uenyekiti wa CCM Taifa utakuwaje au nani atakuwa Mwenyekiti endapo Dr. John Magufuli atashindwa kwenye Urais hapo Oktoba 25?
Hayati Mwalimu Nyerere alikuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa. Mzee Ali Hassan Mwinyi alikuwa Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa. Utamaduni na utaratibu huo ulimhusu pia Rais Mstaafu Mzee Benjamin Mkapa. Hata sasa,Rais Jakaya Kikwete ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.
Uenyekiti wa Rais Kikwete unakoma mwaka 2017 kwakuwa alichaguliwa mwaka 2012 kwa mara ya pili ya miaka mitano. Sasa,uenyekiti wa CCM Taifa utakuwaje au nani atakuwa Mwenyekiti endapo Dr. John Magufuli atashindwa kwenye Urais hapo Oktoba 25?