Daah asee Mkuu ulichokisema ni ukweli mchungu. Mipango yangu haijakaa fresh lkn naitamani rx 8 ya atleast 2009 kuanzia model hio nasikia hazina shida Sana kuna mhindi mmoja anayo hapa town aliniambia. Hivi Mkuu ngoja nichomeke swali langu hapa kuna gari linaitwa NISSAN CIMA model ya 2005 Cc 4500 V8 unaweza kua unaifaham na performance zake zilivo? Kuhusu kua v8 sio shida maana ulaji wake mafuta ni kama hio Mazda tu. Shida yangu ni kujua kama hua unakutana nazo hapo ofisini Mkuu.solution yake ndio hiyo mkuu unavua jiko unaweka jiko jingine tatizo mnao miliki magari mm mnanishangaza sana watu mnaagiza magari ya mpaka milion 50 lkn kuagiza spea za laki 5 au mbili tatu hata milion mnashindwa mwisho wake magari yanakufa na kuozea magereji.mtu anahangaika wee kutafuta spea wakati ukiingia online unakuta bei ya kutupwa sana.
mfano wa engine unakuta gari imesumbua control box au nozel au sensor yoyote ile bongo haipatikani ila ukiagiza unaipata badala ya kuagiza wanashauriana na fundi na kushusha engine na kuweka engine tofauti modification nyingi mwishowe gari linakuwa bovu zaidi