Mwitikio wa Wananchi juu ya Hotuba kali ya JK dhidi ya TUCTA

Mnaoelewa juu ya ubovu wa kauli za yule jamaa ni wachache sana, na yeye analijua hilo, ndo maana akathubutu kusema kuwa ..."sihitaji kura zenu"...
Kwani broda hujasikia watu wanaandamana huko Tabora na Mbeya kuunga mkono hotuba yake?
Anyway, hata kama atashinda, wafanyakazi tumwondolee uvivu kwa kumpigia NO"
Kwa imani yangu ni kwamba mapenzi mema huanza na mtu kujipenda mwenyewe. Siamini kama unaweza kuwa wewe mwenyewe hujipendi halafu tukategemea ukapenda kwa mapenzi ya dhati watu wengine. Hivyo hivyo naamini kwa jinsi JK alivyotuudhi wafanyakazi wa nchi hii wakati huu ameonyesha chuki ya dhahiri kwetu na jamii nzima ya watanzania. Watoto wa mjini wana sema "punda afe mzigo ufike" ndivyo alivyotufanya na ndivyo anavyoamini. Pia ametufanya jogoo "yaani tuwike tusiwike kutakucha"

Hivyo kama jamii yenye nguvu na ndio wengine huwa tunafanikisha wizi wa kura kwenye chaguzi mbalimbali inabidi tubadilike sasa kwani inaonyesha wazi kwamba aina ya urafiki tulionao wafanyakazi wa tanzania na serikali iliyopo madarakani ni wa mashaka.

Hivyo kwa nia njema tu na nguvu tuliyonayo inabidi tuonyeshe kwamba pamoja tunaweza bila kikwete wala sisiem. Na kwamba sisi wafanyakazi kama jamii ambayo ni ya wafanya maamuzi ya hatma ya nchi tuonyeshe kwamba sisi ni aina ya jogoo ambaye asipowika hakukuchi na tuonyeshe hivyo october.
 
Tatizo la kuchagua mvuto badala ya nini atatufanyia limetukosti...sasa 2010 tufanye kweli tuchague mtu kwa sifa na agenda yake ya nini atatufanyia kama taifa na siyo mvuto............:target:
 
Nimeona picha za mji wa Tabora mjini hapo juu kama ni kweli kwamba hakuna uzushi katika hizo picha hao wadau wa tabora walioandamana nina wasiwasi kama hata hiyo spichi waliiangalia kweli. Siamini mtu mwenye akili timamu anaweza kuipongeza spichi ile. Atakuwa ni mtanzania wa namna gani huyo, sina majibu.

Na nyie sisiem muache kutopotoshea watu wetu, hivi kweli hata nyinyi mnashindwa kuwakataza watu wenu kuandamana kwa ajili ya ujinga hamjui kwamba historia itakuja kuwahukumu?

Kikweli mwisho wenu umekaribia. Dola zozote ambazo huishi kwa dhuluma mwisho wake unafahamika na dunia ina uzoefu huo. Endeleeni kudanganyana na kuwadanganya wananchi maskini wa tabora kuwapongeza kwa ujinga halafu mwisho tutakuja kuujadili hapahapa.

Changamoto kwa wananchi,wanamapinduzi na wapendanchi wa nchi yangu hii msimu wa uchaguzi ndio huu unakuja, hatuhitaji nguvu nyingi katika kupiga kampeni wala hatuhitajiki kutumia lugha kali bali ni kuwakumbusha tu wafanyakazi kwamba muungwana amesema hahitaji kura zetu kwa hivyo kwa kumpigia maana yake unampa mtu kitu ambacho hakihitaji na ndio maana haishi kutuahidi uongo kila wakati.

Shime wafanyakazi mustakbali wa taifa letu upo mikononi mwetu tukikumbuka watoto wetu maskini wenye elimu duni ndio warithi wa taifa hili bila sisi kusimamia hili, historia ina sisi.
 
Siwezi kukataa umma wa watanzania na mimi nikiwa mmoja wapo tulishiriki kumuweka madarakani,lakini pia ikumbukwe alikuja na ahadi nzito na kimamtiki kuwa amedhamiria kubadili mfumo wa kiutawala na kusema atahakikisha kila mtanzania ana pata maisha bora kwa nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya...huku tukikumbuka kuwa tulikuwa tumeshaelezwa na utawala uliopita kuwa ndege ya raisi ni bora kuliko njaa yetu na maghorofa ya benki kuu lazima yajengwe hata kama hela za kuweka mle hatuna....ilikuwa ni rahisi kwa muungwana kutushawishi kumchagua...

Lakini kwa aliyoyaongea wiki iliyopita!!!!!! Jamani hapana,hayavumiliki....najua mimi nitatumia huhuru wangu wa kidemokrasia kulipigilia msumari tukio lile mwaka huu,sidhani kama kuna risala yeyote itakayofuta taswira aliyojijengea mtuku mkuu wa nchi hii moyoni mwangu ya kuwa 'HANIJALI!!!!'

Pia najua watanzania wenzangu walio vijijini wamedhamiria kuwa kinyume nami,na ndo haswa waliompa mkuu wangu nguvu ya kusema kura yangu haina thamani kwake kwani wananchi wa karagwe, matombo,mgeta,mkuzi na sehemu nyingine huko vijijini watampa kura na kwa wingi wao lazima atashinda...

Ila katika yote nataka wajukuu zangu waje kukumbuka kuwa mimi babu yao nilikuwa mmoja wa watanzania niliyekataa kwa kutumia uhuru wangu wa kidemokrasia kuitwa mbayu wayu pale nilipodai haki zangu za kimsingi...
 
Nguvu ya ushindi ni umoja, hivyo tunachotakiwa kufahamu na kufanya ni kutambua nguvu yetu inayodhalilishwa na itoe matokeo ya ufahamu wetu kwani mazoea yanaweza yakamfanya mtu asifahamu vitu ya thamani kwake ni vitu gani na badala yake akachagua kupigiwa makofi ambayo ki msingi hayana maana yoyote na akasahau suala la msingi. Tuna wajibu katika kumkumbusha hili na ni wajibu wetu muda wa kupiga kelele umepita tufanye mambo.
 
Mimi niliangalia kwa makini sana, wapo waliokuwa wanashangili ili wakumbukwe kupewa angalau ukuu wa wilaya, wengine walikuwa kimya tu na wengine walishangilia ili wasionekane wanapingana naye.

Lakini sidhani kama ukumbi mzima wote walikuwa 100% nayeye, kama walikuwa hivyo basi hawakutumia ile ya Akili za mwenzio changanya na za kwako

...Ni kweli Mkuu, kuna wazee wengine hasa wanaume walioneka kuwa walikuwa hawafurahishwi kabisa na kilichokuwa kikiendelea pale!
 

Uandishi habari wa Tanzania...

Ripoti ya gazeti, tena headline news, ni mawazo ya bii kizee kimoja! Kila mtu ana mawazo, huwezi chukua ya bii kizee kimoja yakawa habari mjini.

Halafu huna hakika kwamba hicho bii kizee sio yeye mwenyewe mwandishi alimtafuta anaefanana nae kimawazo ili atoe maoni yake( mwandishi ) kupitia mdomo wa bii kizee Asha Omary. Hii si habari...
 

Uandishi habari wa Tanzania...

Ripoti ya gazeti, tena headline news, ni mawazo ya bii kizee kimoja! Kila mtu ana mawazo, huwezi chukua ya bii kizee kimoja yakawa habari mjini.


Kwanini mawazo ya "Bii kizee kimoja" yasiwe ni mawazo wakati kila siku tunasoma mawazo ya "msomi mmoja", sijui Profesa, sijui Waziri fulani? Au kwa vile ni "bii kizee" mawazo yake yapuuzwe?


Halafu huna hakika kwamba hicho bii kizee sio yeye mwenyewe mwandishi alimtafuta anaefanana nae kimawazo ili atoe maoni yake( mwandishi ) kupitia mdomo wa bii kizee Asha Omary. Hii si habari...

kwa hiyo mawazo ya mtu mmoja hayastahili kujulikana au hadi yawe mawazo ya wengi ndiyo yanapata uhalali wa kutolewa? Au ni kwa sababu ya kuwa ni bi kizee? Kama mwandishi anakubaliana kimawazo na mtoa mawazo je mwandishi asiyatoe mawazo hayo kwa vile yanakubaliana na ya mtoa mawazo? Kwako mawazo halali kutolewa ni yale yanayopingana na mwandishi ndiyo yanakuwa na uhalali?
 
mi naona kama nachananyikiwa kidogo, maana wafanyakazi na watetezi wao wakisimama kuichambua hotuba ya Rais, wanasema ameongopa. Rais na wenzake walio serikalini wakijibu hoja za wafanyakazi wanasema Mgaya na wenzake wanaongopa.

who is a liar now, or is it safe to conclude that both sides are liars? or there is a hidden agenda the public is not told?

need some help in this
 
mimi naona workers movements sasa naanza kuona, make hata uhuru ulianza na movements za watu mablimbali wakiwemo wafanyakazi, sasa nafikiri Raisi na crew yake wamesahau kuwa mfanyakazi mmoja sawa sawa na watu 20 so akiamua kureverse order badala ya kuwa clockwise then inakuwa anti-clockwise, so inabidi raisi aelewe kuwa is playing with FIRE, lakini si mnajua ule msemo usemao adui mwombee njaaaa, then tunahitimissha kuwa uchaguzi wa 2010 JK anaweza kuwa mshindi wa tatu iwapo watu watakuwa makini.
 
What did you expect kutoka kwa commentators wa STAR TV?...UmeshaWAHI ona wanapinga chochote anachosema JK?...Ingekuwa Channel 10 NDO NINGESHANGAA!
 
Wanaweza wakawa wamepata shinikizo/tishio kwamba wasipofanya hivyo watafutiwa sababu ya kufungiwa vyombo vyao vya habari. Hivi ikitoka directive kutoka State House kwamba vituo hivyo vinatakiwa viitoe hotuba hiyo mara kwa mara, wenye vyombo vya habari wana ubavu wa kukataa?

Kubenea alimwagiwa tindikali na hatimaye gazeti lake likafungiwa. Hakuna kisichowezekana kwa Serikali inayotaka ishinde uchaguzi kwa nguvu hata kama haina sifa za kuweza kushinda.
 
Pamoja na ujasiri na ukali wote alioonyeshaa mwanzo wa hotuba na kushangiliwa kama ngasa na wapambe ambao wengi walikua wana ccm, vijana tena kina mama, mwisho wa hutuba aliishia kusema ndugu zangu wafanyakazi tunawapenda,na serikali yenu ni sikivu na itajihidi kuona uwezekano wa kupandisha mishahara na baadae akatupa hadithi ya mbayumbayu alipo muuliza kongo'ta sasa mwanangu ameniuliza hivi baba ndege anasemaga?sijampa jibu mpaka leo
 
Ndugu,

Watanzania ile hotuba Mzee mzima alikuwa na jazba na maji yalikuwa shingoni,na gharama ya hotuba ile imemshushia hazi mheshimiwa kwa asilimia 60.Tungekuwa waelewa jamaa amefilisika kabisa kisiasa kwa sababu nchi yetu ni ya amani,umoja na mshikamano,sasa huyu vitisho vimeanza lini,maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi?Ajira je?

Na hawa wanaoshabikia hii,upeo wao wa kufikiria umeishia hapo,

Lakini Tumuombea huyu mheshimiwa kazi ya kuongoza watu,inahitajika busara,hekima na uvumilivu

Na ajue mapinduzi mengi hapa duniani yaliletwa na wafanyakazi,na haki inadaiwa,na hakuna mtu wa kukupa haki,

TUCTA MKO JUU SANA,MSIJALI VITISHO VYA CHURA HAVIMZUII NG'OMBE KUNYWA MAJI

Elisante Yona
 
Hivi sasa ni kuwa makini na kila comments zinazotolewa na hivi vyombo vya habari. Inaonekana vinatumiwa ili vimsafishe jamaa dhidi ya hotuba yake mbaya na ya aibu kuwahi kutolewa na kiongozi wa nchi hapa duniani kwa mwaka huu.
 
Wanazidi kumharibu Mh Mkwere! Vyombo vya habari vingekaa kimya sisi watanzania huwa tunasahau haraka sana.....
 
Back
Top Bottom