Jamani nomba kuuliza kama kunamtu anajua nn kinaendelea juu ya huyu jamaa maana isije ikawa anarudi bana maana nilisikia kunawabunge pamoja na kamati ya nishart walikua wanamtetea sijui imefikia wapi?
Hachomoki na watu wake wote wana hali mbaya. NCCR mageuzi wametoa maelezo muda mfupi ITV juu ya wizi wake na pia baadhi ya wabunge tuliwasema wanaochumia tumbo. Tunawasubili tuwasikie ili waaibike zaidi.
Huyu Mhando na Mh. Mkono ni wezi tu hakuna jina zuri la kuwapa. CCM tunajimaliza wenyewe kwa kutetea maovu!
mgongano wa kimaslahi uliojitokeza kwenye swala zima la tanesco kwa kitendo cha wabunge ambao ni wajumbe wa bodi ya tanesco kutetea ufisadi huu? huwezi kuwatumikia mabwana wawili wakati mmoja ?? sasa unaongea kama mbunge saa ngapi na saa ngapi unaongea kama mjumbe wa bodi?? unalinda maslahi ya bunge au ya tanesco?? kama mbunge kazi yako ni oversight(kusimamia serikali(tanesco)) unawezaje kusimamia serikali wakati nawe ni sehemu ya serikali hiyo(mjumbe wa bodi)?? hii ni sawa na kuwa prosecutor na at the same time kuwa judge ktk kesi yako inayokuhusu. ni tz tu ndio inaruhusu upumbavu kama huu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.