Mwanangu wa kiume miaka 4 lakini haongei ni kupiga makelele tu

Habari za majukumu ndugu zangu,Nina mtoto wa kiume miaka 4 Sasa lakini haongei ni kupiga makelele tu ana dalili hizi hapa chini
1. Ukimuita jina lake hageuki
2. Anapiga makelele tu
3.kuna wakati Anakuwa anaziba masikio
4. Anatamka sauti zinazojirudiarudia lkn hazieleweki
5. Anapenda kuning'iniza vitu mfano chaja za simu,waya,funguo,ama kitu chochote akishika yeye n kuning'iniza anaweza kutoka chumban na nguo ya ndani ya mamake akaja nayo sebuleni ananing'iniza ( anapenda sana hicho kitu)
6. Mikono yake kama imelegea hata kuanza kula mwenyewe alichelewa na saiv anakula mwenyewe Ila anasambaza chakula ukimpa wali maharage atakula 10% asilimia 90 utakuwa kasambaza chini
7. Anapigapiga kidevu chake
8. Anapenda vitu vyake tu ,
9. Hapendi kucheza na watoto wenzake anajitenga nao hata wakiwa 200 yeye atakaa pekeake anafanya vitu vyake
10. Ukimtuma kitu hawez kuleta maana hakuna kitu anaelewa
11. Kuna nywele zilinyolewa akiwa mchanga Hadi hazijaota. Sehem zingine znaota lakini hiyo sehem hazioto

Nilishampeleka Kwa waganga wanasema mizimu,kurogwa, hospital Wanasema usonji(Autism),maji ya mwamposa alishatumia ,Niko naendelea kutafuta tiba naomba mnisaidie Niko TAYARI kutoa MILION 5 CASH Kwa atakayenisaidia mtoto huyu kuongea. Naumia Kwa sababu ni mwanaume siwezi kuweka emoji za kulia. Naumia sana. Namba zangu ni 0689590080.
Dah!
Pole sana.
Huyo mtoto anaonekana ana dalili za Usonji (Autism). Kuna mtaalamu fulani kwenye runinga aliwahi kutuchambulia hiyo hali.

Msaada hapo ni kumpeleka kwa madaktari bingwa wa watoto na wataalamu wa afya ya akili.

Note:
Usipoteze muda wala pesa zako kwa watu watakaojitokeza na kujifanya wanaweza kuondoa hiyo hali, kiuhalisia hiyo hali huwa ni ulemavu ubongo na mwili wa kudumu lakini kupitia msaada wa kidaktari inaweza kuboreshwa kwa kupunguza madhara ikiwemo mtoto kuweza kutulia, kukua, kuwasiliana na kuishi na jamii. Zaidi ya hapo usitegemee makubwa sana labla msaada wa imani ya miujiza.
 
Habari za majukumu ndugu zangu,Nina mtoto wa kiume miaka 4 Sasa lakini haongei ni kupiga makelele tu ana dalili hizi hapa chini
1. Ukimuita jina lake hageuki
2. Anapiga makelele tu
3.kuna wakati Anakuwa anaziba masikio
4. Anatamka sauti zinazojirudiarudia lkn hazieleweki
5. Anapenda kuning'iniza vitu mfano chaja za simu,waya,funguo,ama kitu chochote akishika yeye n kuning'iniza anaweza kutoka chumban na nguo ya ndani ya mamake akaja nayo sebuleni ananing'iniza ( anapenda sana hicho kitu)
6. Mikono yake kama imelegea hata kuanza kula mwenyewe alichelewa na saiv anakula mwenyewe Ila anasambaza chakula ukimpa wali maharage atakula 10% asilimia 90 utakuwa kasambaza chini
7. Anapigapiga kidevu chake
8. Anapenda vitu vyake tu ,
9. Hapendi kucheza na watoto wenzake anajitenga nao hata wakiwa 200 yeye atakaa pekeake anafanya vitu vyake
10. Ukimtuma kitu hawez kuleta maana hakuna kitu anaelewa
11. Kuna nywele zilinyolewa akiwa mchanga Hadi hazijaota. Sehem zingine znaota lakini hiyo sehem hazioto

Nilishampeleka Kwa waganga wanasema mizimu,kurogwa, hospital Wanasema usonji(Autism),maji ya mwamposa alishatumia ,Niko naendelea kutafuta tiba naomba mnisaidie Niko TAYARI kutoa MILION 5 CASH Kwa atakayenisaidia mtoto huyu kuongea. Naumia Kwa sababu ni mwanaume siwezi kuweka emoji za kulia. Naumia sana. Namba zangu ni 0689590080.
Pole sana Kaka kwa Mwanao. Lakini sikiliza Madaktari wataalam.

Shida ya Mwanao sio Ndogo ni Kubwa.

Swala la kuongea sio issue sana lakini hizo tabia zingine alizo nazo zinafanya lionekane kubwa.

Nakushauri kwa sisi Madaktari wa Miti Shamba( bush doktas) usimleta tutakulia pesa zako bure.

Mpeleke kwa Paediatrician na Medical Psychologist angalau utapata unafuu wa namna ya ku cope naye.

Hiyo ni Autism haina Dawa.
 
Pole sana Kaka kwa Mwanao. Lakini sikiliza Madaktari wataalam.

Shida ya Mwanao sio Ndogo ni Kubwa.

Swala la kuongea sio issue sana lakini hizo tabia zingine alizo nazo zinafanya lionekane kubwa.

Nakushauri kwa sisi Madaktari wa Miti Shamba( bush doktas) usimleta tutakulia pesa zako bure.

Mpeleke kwa Paediatrician na Medical Psychologist angalau utapata unafuu wa namna ya ku cope naye.

Hiyo ni Autism haina Dawa.
😭
 
Mtoto inabidi aanze kukaa na kusimama akiwa na miezi mingapi maana wangu ana miezi mitatu ila hapendi kulala lala ana taka kusimama simama
Katika hali ya kawaida, mtoto
Miezi
0-1 analala tu bila kugeuka
1-2 anageuza kichwa/shingo
3-4 anakaza shingo
4-5 anakaa kwa kuegemea kitu
6-7 anakaa bila kuegemea kitu
7-8 anabilingita (rolling) akilala
9-10 anatambaa
11-12 anasimama
Kuanzia mwaka mmoja anaweza kutembea.

Nocte:
Wapo watoto wanaoweza kuwahi hatua fulani (hiyo haina maana kila hatua itawahi, kuna hatua atasimama zaidi bila kusonga mbele) au kuchelewa hatua fulani (hiyo haina maana hatua zote zitakazofuata atachelewa) kuna kitu wanaita growth compansation mechanism, mtoto mwenyewe anaweza kuifanya automatically au jamii ikaifanya kwa mtoto kwa kujua au kutokujua.

Lakini ikiwa mtoto atachelewa zaidi ya miezi mitatu kuvuka hatua inayotakiwa (kwa mfano ikiwa mtoto anatakiwa mpaka kufikia miezi 12 awe anaweza kusimama) halafu akafika mpaka mwaka mmoja na miezi mitatu hajaweza kusimama, hapo inabidi juhudi za haraka zifanyike, na ikiwa juhudi hizo zitafanyika bila kuzaa matunda basi inatoa picha mtoto atakuwa na tatizo kubwa ambalo litahitaji muda mrefu zaidi kutatuliwa kitaalamu.

Mwisho wapo watoto ambao wanawahi kusimama (kwa kushika kitu) wakiruka hatua ya kutambaa, hiyo haina maana kuwa mtoto atatembea bila kutambaa, kadri atakavyotaka kutembea mtoto atarudia kwanza kutambaa. Zoezi la kutambaa ndio zoezi muhimu na bora zaidi kumuandaa mtoto kuja kutembea vizuri siku akianza kusimama. Mpe mtoto muda na nafasi ya kutambaa kadri atakavyo, usimharakishe, siku akichoka kutambaa mwenyewe atatamani kusimama na kutembea.
 
Anadalili za ububu

Ana dalili za polio

Ana dalili za mental retardation

Ana dalili za teratogenic conditions (fatilia kipindi cha mimba mama yake alikuwa anapenda kutumia vilevi au vyakula gan)

Wakat anazaliwa alilia? Na kama alilia alitumia muda gan Toka azaliwe mpka kulia?

Muanzishie doz ya mayai, vichwa vya samak wabichi, maziwa mabichi, mboga za majani, karanga na maharage. Yani kifupi apate protein ya kutosha
Wewe...sio Doctor hizo Dalili za polio .....?

Rubish
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom