Mwanamke: Kama unaishi na mwanaume wa aina hii, basi pinga usikubali kuwa mjinga

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
119.jpg

Na ukijaribu kunipiga tu, utajua mimi ni mwanamke wa namna gani, hutakuja kunisahau..........!

Uzoefu unaonesha kwamba baadhi ya wanaume au wanawake hutumia kile walichokiona kutoka kwa wazazi wao katika ndoa zao. Tabia za wazazi huakisi sana maisha ya watoto wao hususan katika maisha yao ya ndoa, labda kama watajitambua na kujivua gamba, lakini vinginevyo watakuwa wanatumia kile walichokiona na kujifunza kutoka kwa wazazi wao.
Kwa mfano mwanamke anayeishi na mwanaume mnyanyasaji na mpigani, ni dhahiri kama wana mtoto wa kiume anakuwa na uwezekanao mara saba zaidi kuja kuwa mnyanyasaji kwa mkewe atakapokuwa mkubwa. Na kama ni binti ana uwezekanao mara tatu zaidi kuja kuwa mtu wa kupata vipigo atakapokuwa ameolewa. Hapa wa kulaumiwa ni wazazi, kwa sababu wao ndio wamewafanya wawe hivyo. Kwa kuwa wazazi ndio mashujaa wa watoto wao, huakisi tabia halisi za wazazi wao.

Hebu fikiria una miaka sita na unasikia ukiwa kwenye chumba chako baba yako anapompiga mama yako! Mama yako anapiga mayowe na kulia akiomba msaada! Unamsikia baba yako akimpiga mama yako ngumi na mateke na kumwita majina machafu machafu ambayo kimsingi hutakiwi kuyasikia. Utafanya nini ukiwa ni mtoto na uko katika mazingira kama haya? Ukweli ni kwamba huwezi kuondoka! Na unakuwa huna uchaguzi zaidi yakukubali kuishi na wazazi wako ambao kimsingi aina ya maisha wanayoishi sio kama mke na mume bali mume na mtumwa wake ambaye ni mama yako. Unalazimishwa kuishi hivyo, hutaki hata marafiki zako waje nyumbani kwenu. Mama kila siku ana manundu mwilini kwa vipigo kutoka kwa baba yako. Na si hivyo tu, baba kila siku akirudi nyumbani anaaanza kufoka! Na sasa siri zenu zote ziko nje. Pale mtaani familia yenu imekuwa ni gumzo, huna raha kama watoto wengine. Balaa gani hili!
111.jpg

Mie bado nawalaumu wanawake wanaokubali ujinga huu, ingawa kuna watu wananishambulia humu jamvini, lakini kwa hili siwezi kulinyamazia. Ni ujinga tu ndio unaosababisha wakubali kuishi kwenye ndoa za namna hii. Kama wewe ni binadamu kamili ambaye umezaliwa ukiwa na akili zako timamu, kwa nini ukubali kuishi na mwanaume mfuajaji ? Kama unataka kuishi na mwanaume wa aina hii, basi pinga usikubali kufanywa gunia la mazoezi. Simama imara ukiwa umeshika kikaango na umwambie, ‘Njoo unipige uone. Na siku ukijaribu kunipiga tu, utajua mimi ni mwanamke wa namna gani, hutakuja kusahau.' Au kama huwezi hilo basi zuia upigwaji kwa njia nyingine. Lakini uzoefu unaonesha kwamba, njia iliyo bora kabisa ni kuondoka kwenye uhusiano huo.

Kama uko kwenye ndoa ya mateso na unajikuta huwezi kutoka, umekubali kuwa fuko la mazoezi la mumeo, jiulize ni kwa nini. Anzia kwa wazazi waliokulea na kujiuliza kama wewe siyo mama yako ambaye alikubali kupokea vipigo kwa mumewe huku akiendelea kuvumilia na kuishi katika ndoa hiyo ya mateso. Kama ndivyo, basi kataa kuwa mama yako. Anza safari ya kuwa wewe ambaye huko tayari kuwa mtumwa wa mtu kwa kuhofia kusimama mwenyewe kwa miguu yako. Amua sasa na utamudu, kwani wewe ni binadamu kamili na huhitaji kukamilishwa na mtu mwingine.
 
mmmh! binafs nawza kuvumilia kila kitu but not kichapo manake pakifika hapa jamani tunatembezeana. uuuwiiiiiiiiii khaaa eeeh! ndipo litakapo timia lile neno mpalestina.

cheza vyovyote na mimi but usiniguse kwa kipondo lol! vingine vyote navumilia ila hili hapana na nilishalisema kabisaa.
 
mmmh! binafs nawza kuvumilia kila kitu but not kichapo manake pakifika hapa jamani tunatembezeana. uuuwiiiiiiiiii khaaa eeeh! ndipo litakapo timia lile neno mpalestina.

cheza vyovyote na mimi but usiniguse kwa kipondo lol! vingine vyote navumilia ila hili hapana na nilishalisema kabisaa.
gfsonwin nilisahau kuweka angalizo usichangie hii mada....................LOL
 
mmmh! binafs nawza kuvumilia kila kitu but not kichapo manake pakifika hapa jamani tunatembezeana. uuuwiiiiiiiiii khaaa eeeh! ndipo litakapo timia lile neno mpalestina.

cheza vyovyote na mimi but usiniguse kwa kipondo lol! vingine vyote navumilia ila hili hapana na nilishalisema kabisaa.

Uendelee hivyo hivyo hakuna sababu yoyote ya mwanaume kukunyanyasa kwa vipigo, kama ameshindwa basi afunge virago siyo kutaka kukuharibu reception yako au kukutia ulema.
 
Asante mtambuzi kwa ushauri mzuri kwa wa dada na jua leo wergine watapima waone.
 
Hii uliyosema ndio saikolojia ya human development. Mazingira mtu aliyokulia na tabia za wazazi zinachangia muonekano na tabia ya mtoto/mtu. Kubadilika si rahisi labda kama utapata washauri na ukaelewa chanzo cha tatizo lako.
 
mmmh! binafs nawza kuvumilia kila kitu but not kichapo manake pakifika hapa jamani tunatembezeana. uuuwiiiiiiiiii khaaa eeeh! ndipo litakapo timia lile neno mpalestina.

cheza vyovyote na mimi but usiniguse kwa kipondo lol! vingine vyote navumilia ila hili hapana na nilishalisema kabisaa.
gfsonwin kw akweli mambo mengine nayo yanatakiwa yaangaliwe
Uko ndani ya nyumba na watoto wanasikia mama yao anapigwa anaomba msaada na kelele juu
Au mara anatoka mbio ndani ya chumba nguo mkononi au imeraruliwa na makovu anakimbia
Watoto wanaangalia na kusikia aina kwa aina za matusi yasiyoweza hata kusemeka
Je ni aiona gani ya malezi unawapa watoto wako
Je watakua wakiwa na wazo gani kichwani mwao
Kuwa baba ni katili na mwenye matusi
Kuwa baba anatumia nguvu zake dhidi ya mama kwa kuwa mama hajiwezi au hawezi kumjibu
Ustaarabu ni kukaa na kuyamaliza bila hata watoto kujua kuwa mama na baba wana ugomvi ndani ya nyumba
Yaani mkitoka master bed room mnacheka as if dakikka tano zilizopita mlikuwa mnagombana wala watoto hawaelewi ugomvi wenu wala nini
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tukilaumu wazazi basi tulaumu na wazazi wao maana kama kosa liko kwenye inheriting the abuse trait pake yake na mtenda hahusiki then this is an endless and recurring problem.
wazazi watalaumu wazazi wao ambao watalamu wazazi wao and so on....
mpaka kwa Adamu(was he abusive too ?)
Sijui ila hili tatizo ni kama Ukimwi kwamba to stop it 'It begins with you'...
Binafsi I will not (Namuomba sana Mungu anisaidie) rise a hand over my wife.
Najua the minute the hand lands on her body I will receive more pain than she probably will because I will put a scar in her heart that will probably never heal if not taking so long to heal.
Yani mama akipigwa the whole family will have to suffer the pain. Unamuambiaje mtoto I am your father and I love you wakati anajua umeinflict pain on their beloved mother?
The best gift you can give your children is to love their mother, trust me!
 
binafsi hii hali ilishanikuta wakati tuko wadogo ila nakumbuka nikiwa darasa la saba na mimi ndo nilikuwa wa mwisho kwetu, siku moja nilimwambia mama ni kwa nini asiondoke pale nyumbani coz alikuwa anapigwa sana, mama akasema akiondoka tutateseka nilimwambia kuwa kama ikitokea akakuua je nani atatulea? akakosa jibu, baada ya kile kipindi akapigwa tena ma baba mie nilikuwa nimeenda shule niliporudi nilikuta mother analia kuwa ameumizwa! mie nilishikwa hasira na kumwambia: wewe kaa tu si umeamua mwenyewe kukaa. nililia sana na kumlaumu mama kuwa anajitakia mwenyewe, ila baada ya mie kwenda sekondary aliondoka na mpaka sasa anasema mie ndo niliemshtua. Hali kama hiyo nilishaapa siwezi kuivumilia hata siku moja coz nilishaona.
 
Uendelee hivyo hivyo hakuna sababu yoyote ya mwanaume kukunyanyasa kwa vipigo, kama ameshindwa basi afunge virago siyo kutaka kukuharibu reception yako au kukutia ulema.

unajua hakuna sababu yyte ya mimi kudhalilishwa mbele ya wanangu duh! kimada mlete lala naye miye wala hanipi shida manake mwili ni wako ila kipondo kabisa umenifanya miye mwanao ama?? hvi aisee hapa tupigane wewe ukirusha ngumi miye narusha mwiko hata stuli hivi humo ndani hamnaga hata visu ama pasi. namkumbuka mama mmoja aliweka pasi kwenye umeme moto namba 3 tena ikapata moto ile mbaya ile bwana anakaribia na ngumi yake mkononi mama kainyanyua pumbavu tiya kifua bwana kaungua kifua umbo la pasi. akabaki kulala mika manka umenichoma manka umenichoma. baada ya hapo mwanamke akampeleka mumewe hosp na mpaka leo nidham khaa!!!!!!!!!!!
 
gfsonwin kw akweli mambo mengine nayo yanatakiwa yaangaliwe
Uko ndani ya nyumba na watoto wanasikia mama yao anapigwa anaomba msaada na kelele juu
Au mara anatoka mbio ndani ya chumba nguo mkononi au imeraruliwa na makovu anakimbia
Watoto wanaangalia na kusikia aina kwa aina za matusi yasiyoweza hata kusemeka
Je ni aiona gani ya malezi unawapa watoto wako
Je watakua wakiwa na wazo gani kichwani mwao
Kuwa baba ni katili na mwenye matusi
Kuwa baba anatumia nguvu zake dhidi ya mama kwa kuwa mama hajiwezi au hawezi kumjibu
Ustaarabu ni kukaa na kuyamaliza bila hata watoto kujua kuwa mama na baba wana ugomvi ndani ya nyumba
Yaani mkitoka master bed room mnacheka as if dakikka tano zilizopita mlikuwa mnagombana wala watoto hawaelewi ugomvi wenu wala nini
Mr Rocky kweli mi ni mtu nipendaye sana amani na nidham ila usinivunjie heshima yangu. eti wanangu wako hapo miye nakula mabao nalia kwa b/rum? kwakosa gani hasa? hata kama ni nini hakuna mwenye hayo mamlaka aisee baba yangu mzazi japo ni wa zamani alkn hakuwah kunipiga hadi leo hii nazeeka sembuse wewe umenikuta mkubwa?

nifanyie yote yasiyoumiza mwili wangu ama kujeruhi mwili but not this one hivi jamani nisiseme manake kweli sifichi ile roho ya mpalestina itaonekana laivu. wacha tugawane majengo bana kwani nini? weye ukienda hosp miye naenda cage.

panapokosa tuongee na unipe muda kwa kujitetea na nikiona nataka yaishe kwa amani nakuangukia magotini nisamehe. zaid ya hapo hapana aisee.
 
Mtambuzi nishashuhudia sana haya mambo ya mama kupigwa na baba kwa familia jirani yetu
Kila siku ilikuwa ni kipigo kutoka kwa baba kwenda kwa mama yule
Yaani ni painful unapomuona huyo mama kesho yake na mangeu bado anahangaika kumhudumia the same man ambaye jana yake alimtwanga makofi na mateke
Bado anampikia na kumfulia licha ya kwamba ana maumivu ya kipigo
Yaani unhisi maumivu anayopata yule mama
 
Last edited by a moderator:
Kujitetea dhidi ya vipigo toka kwa mume/boyfriend ni muhimu sana. Mtambuzi halafu si kila aliyeona Baba akimpa vipigo mama huwa anarithi tabia hiyo mbaya naye kuitumia katika mahusiano yake. Katika mazungumzo na rafiki zangu wa karibu kuhusu swala hili wengi ambao walishuhudia vipigo dhidi ya mama zao hawajawahi kumgusa GF/Wife au hata kwa kibao kimoja au hata kumfinya. Nawadharau sana wanaume ambao hushindwa kumaliza tofauti zao na maGF/wake zao kwa njia za amani na kuamua kutumia vipigo.

unajua hakuna sababu yyte ya mimi kudhalilishwa mbele ya wanangu duh! kimada mlete lala naye miye wala hanipi shida manake mwili ni wako ila kipondo kabisa umenifanya miye mwanao ama?? hvi aisee hapa tupigane wewe ukirusha ngumi miye narusha mwiko hata stuli hivi humo ndani hamnaga hata visu ama pasi. namkumbuka mama mmoja aliweka pasi kwenye umeme moto namba 3 tena ikapata moto ile mbaya ile bwana anakaribia na ngumi yake mkononi mama kainyanyua pumbavu tiya kifua bwana kaungua kifua umbo la pasi. akabaki kulala mika manka umenichoma manka umenichoma. baada ya hapo mwanamke akampeleka mumewe hosp na mpaka leo nidham khaa!!!!!!!!!!!
 
Kujitetea dhidi ya vipigo toka kwa mume/boyfriend ni muhimu sana. Mtambuzi halafu si kila aliyeona Baba akimpa vipigo mama huwa anarithi tabia hiyo mbaya naye kuitumia katika mahusiano yake. Katika mazungumzo na rafiki zangu wa karibu kuhusu swala hili wengi ambao walishuhudia vipigo dhidi ya mama zao hawajawahi kumgusa GF/Wife au hata kwa kibao kimoja au hata kumfinya. Nawadharau sana wanaume ambao hushindwa kumaliza tofauti zao na maGF/wake zao kwa njia za amani na kuamua kutumia vipigo.
BAK umesema umesema kwa hekima sana ila kama jitu halina hekima hii aisee wewe mwaga mboga miye namwaga ugali kama mbwai na iwe mbwai kwani nini bana????............ khaaa!.................... ukiona mama anyedhalilishwa kwa kichapo utamuonea huruma halafu usiku jitu linakupekua eti linataka unataka????.................... aisee utaitafuta revola ama kopo la blue band. lakin miye hapana kwanza huko mbona hufiki arifuu uwiii heeeeeeeeeeeee!
 
Last edited by a moderator:
Kujitetea dhidi ya vipigo toka kwa mume/boyfriend ni muhimu sana. Mtambuzi halafu si kila aliyeona Baba akimpa vipigo mama huwa anarithi tabia hiyo mbaya naye kuitumia katika mahusiano yake. Katika mazungumzo na rafiki zangu wa karibu kuhusu swala hili wengi ambao walishuhudia vipigo dhidi ya mama zao hawajawahi kumgusa GF/Wife au hata kwa kibao kimoja au hata kumfinya. Nawadharau sana wanaume ambao hushindwa kumaliza tofauti zao na maGF/wake zao kwa njia za amani na kuamua kutumia vipigo.

Mkuu BAK, nilichokisema ni hiki hapa..........
Uzoefu unaonesha kwamba baadhi ya wanaume au wanawake hutumia kile walichokiona kutoka kwa wazazi wao katika ndoa zao. Tabia za wazazi huakisi sana maisha ya watoto wao hususan katika maisha yao ya ndoa, labda kama watajitambua na kujivua gamba, lakini vinginevyo watakuwa wanatumia kile walichokiona na kujifunza kutoka kwa wazazi wao. Kwa mfano mwanamke anayeishi na mwanaume mnyanyasaji na mpigani, ni dhahiri kama wana mtoto wa kiume anakuwa na uwezekanao mara saba zaidi kuja kuwa mnyanyasaji kwa mkewe atakapokuwa mkubwa. Na kama ni binti ana uwezekanao mara tatu zaidi kuja kuwa mtu wa kupata vipigo atakapokuwa ameolewa. Hapa wa kulaumiwa ni wazazi, kwa sababu wao ndio wamewafanya wawe hivyo. Kwa kuwa wazazi ndio mashujaa wa watoto wao, huakisi tabia halisi za wazazi wao.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom