Ablessed
JF-Expert Member
- Mar 19, 2013
- 4,616
- 3,499
Hii mada ilikua nzuri. Niliona mzee alikua anampa kichapo sana step mother wetu . Kuna siku yule mama alipigwa vibaya sana akaamua kuondoka kwao . Cha kushangaza baada ya siku 2 akarudi nikaamuuliza kwanini umerudi huyu atakuja kukuua je huoni umeumia sana. Alinijibu nakaa kwa muda nitaondoka. Mama yule hakuondoka mpaka leo lkn niliapa sintakuja kuvumilia kipigo toka kwa mume wangu kwa namna yoyote. Namshukuru Mungu alinipa mtu mwema na mwenye hekima.
Hali hii ukiikemea toka day one basi haiwezi kuendelea kwani nafikiri wanaume wengine hujaribu akiona umepokea kipigo na umekaa kimya basi hurudia tena na tena halafu inakua mazoea lkn dada/mama ukikigomea kipigo toka siku ya kwanza huyo mtu hatorudia kukupiga tena.
Hali hii ukiikemea toka day one basi haiwezi kuendelea kwani nafikiri wanaume wengine hujaribu akiona umepokea kipigo na umekaa kimya basi hurudia tena na tena halafu inakua mazoea lkn dada/mama ukikigomea kipigo toka siku ya kwanza huyo mtu hatorudia kukupiga tena.