mangikule
JF-Expert Member
- Jun 11, 2012
- 6,054
- 5,432
Mkuu spanner; mazoba/wachumia tumbo walikuwepo kote kuanzia utawala wa Hitler, hadi Rwanda. Ni waganga njaa!! tu wala usijali mambo yakiwa mambo utayaona yanachafua nguo za ndani tu!Ninyi mliopewa fedha na usalama wa taifa ili muwatetee ondoeni ujinga wenu humu.
Hawa watu ni wauaji na kutetea wauji ni kushiriki uuwaji. Acheni kutetea wauaji. Kama maofisa wa TISS walihusika na wizi wa fedha za umma kwenye BoT, watashindwa vipi kupanga njama za kuuwa wanaokosa serikali.
Stori ya leo ya Mwanahalisi imesheheni taarifa. Tatizo lako umesoma hii iliyopo hapa JF na ukatoa hukumu. Hii ni sehemu tu ya stori. Stori kamili imechukua kurasa mbili. Imesheheni taarifa. Imejaa uchunguzi. Imefuata maadili. Achana na Mwanahalisi.
Kama Kikwete na Zoka wanakana kuhusu hili linalosemwa, basi njia ni rahisi. Waunde tume huru kuchunguza waliomvamia Ulimboka. Kukana pekee yake hakutoshi.
Rostam Aziz alikana kumiliki Dowans. Kikwete alikana kuifahamu Dowans. Lowassa alikana kuingilia mchakato za zabuni na kuipendelea Richmond.
Lakini mwisho wa siku Lowassa akajiuzulu, mahakama ikathibitisha kuwa Rostam ndiye mmiliki halali wa Dowans na Lowassa akasema Kikwete alikuwa anafahamu kila kilichokuwa kinatendeka – kwa maana ya kwamba alikuwa anafahamu Dowans ni mali ya Rostam Aziz.