Mkuu Mdondoaji huyo Sultani ali kujaje kumiliki eneno la ukanda wa Pwani? Je aliipata kihalali au nae ali tumia ubabe? Kumbuka kuna kipindi kwenye historia ya dunia nchi zote ziliundwa kutokana na conquests na vita. Tukifuata mawazo yako ina maana ramani ya dunia nzima yote lazima ichorwe upya. Wazanzibar wadai hilo eneo tuone wata fika wapi, hawaja katazwa. Si hata muungano wamepeleka madai ya kuupinga UN mpaka leo hamna kitu.
Mkuu Sultani alinunua hiyo ardhi kutoka kwa machifu na zipo articles zinasema hilo na nyingi zinapatikana hata kwenye vitabu vyetu vya historia. Sasa kununua ardhi sijui kama ni kosa kuliko kuichukua kiubabe. Ramani ya Duniani inaenda ikibadilika mkuu Kabla ya wakoloni kulikuwa na ramani ya tofauti, 1884-1885 kukawa na ramani nyengine (Berlin Conference), after the first world war ikabadilika, after the second world war ikabadilika, after the end of cold war imebadilika hasa kufuatia kuanguka kwa Urusi, Hivyo ramani inaenda ikibadilika to me that is not the point.
My point is je Tanganyika legitimacy ya kusema ukanda wa pwani ni wetu tumeitoa wapi??? Na nani ana makubaliano ya mauzo baina ya Sultani na Mjerumani? Naona narudia kitu kile kile ni vema nikaishia hapo naomba kujitoa katika hii thread inatosha nilikuwapo.