So far hakuna aliyewazuia, JK kisha wapongeza na wengine wako kimya. Kinachoendelea JF ni mawazo binafsi may be tusubiri tuone kama CCM wataweza kuicheza hii ngoma safari hii!!
1. Sure! Yetu ni maoni tu ndugu! Mtu mwingine asije akazuia watu wengine kufikiria na kutoa maoni huku akijua kwamba Ibara ya 18 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 (pia Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977) inaruhusu watu kutoa maoni! Ibara hiyo ya 18 Katiba ya Zanzibar, 1984 inasomeka hivi: "Bila ya kuathiri sheria za nchi, KILA MTU yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na kutafuta kupokea na kutoa habari na dhana kupitia chombo chochote, bila kujali mipaka ya nchi na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati."
2. Kuhusu uhuru huo huo wa kutoa maoni Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho na Sheria Na. 1 ya mwaka 2005, inasema: "Kila mtu- (a) anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake; (b) anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi; (c) anao uhuru wa kufanya mawasiliano na haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake; na (d) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii."
3. Hapa tunatekeleza tu uhuru wa Kikatiba na hakuna mtu wa kutuzuia. Haya mambo ya mtu kuogopa kivuli chake ndio yanayotoa nafasi ya watu kuanza kutoa maoni na ndivyo tunavyofanya!
 
Unaeleweka sana Ndugu yangu. SMT kinarani ni JK. Katika hotuba zao mbali mbali wote Karume na Maalim wamemshukuru JK kwa kuonesha kuwaunga mkono na wamemuomba (Kiheshima-lakini ni wajibu wake) msaada wake wa dhati katika kufanikisha dhamira zao. Wanaoingilia ni watu kama Msekwa na Makamba.


Makamba na Msekwa hawajawaingilia Wazanzibari kwa lolote, kwani kesho Baraza la Wawakilishi wakikaa na kupitisha Sheria kwamba Karume ataongoza Zanzibar mpaka BWANA atakapomtwaa hakuna cha Makamba wala Msekwa atakayekuwa na usemi! Wao walichofanya ni kutumia uhuru wao wa Kikatiba wa kutoa maoni!
 
inferiority complex
Nafikiri hujuwi unalolizungumza, kuna Freedom of expression na Abuse of the freedom.

Sasa huwezi kukaa mbele za watu na kucheza komedy kama wazanzibari wote ni gay, halafu ukaratajia jamii iendelee kufurahi.

Sasa na sisi huku Zanzibar tukianza kuact film za kuwa wamasai ni gay, kwa kisingizio mmasai mmoja alibakwa na mtaliano?Utasema nini kwenye film kama hii?

Acha pumba get your points straight!Huwezi kutoa mfano wa ndoa ukafananisha na muungano, halafu ikawa kila ukifanya hivyo mifano yako Zanzibar ndio jike.Halafu ukasema ati hiyo ni inferiority complex tuu...lakini huu mfano ni sawa.Mbona hutowi mfano wa ndoa ya kigay?

Acha mizengwe ndugu yangu, huu muungano mie nashauri uvunjwe tuu.Ni vurugu zisizo na tija yoyote!Yalikuwa ni mawazo ya Nyerere, ameshatangulia kaburini sasa ni maamuzi ya walio hai.Vunja au rekebisha kila mtu awe anajulikana boundaries zake ni zipi.
 
Naona watu wana vichwa vitukutu kweli, na hili limefanywa kwa makusudi kufifisha mipaka baina ya Tanganyika na SMT.

Tukumbuke jamani tumeungana, lakini Zanzibar haikupoteza mamlaka yake na serekali yake.Sasa wewe unapolazimisha lazima maoni yako yasikilizwe na kufuatwa, bado yatakuwa maoni kweli?Mie naona kulazimisha maoni yako yasikilizwe ni kuamrisha na sio maoni.

Sasa Bunge tukufu la Zanzibar kesho linaingia uwanjani, na haya yote yatajulikana kama Karume ataendelea au atabaki.Na pia tutapata kujua kama SMZ ni koloni la mtanganyika au ni nchi yenye mamlaka yake yenyewe.

Sasa tusiandikie mate na kalamu ipo, subirini mchezo kuanzia kesho.
umenena kweli tupu,zenj inawenyewe na wenyewe mtawaona kuanzia kesho 20/1/2010 ktk baraza la wawakilishi wataamua mambo yao wenyewe,tusiwaingilie,makamba domo kaya kila mtu anajua,
 
Nafikiri hujuwi unalolizungumza, kuna Freedom of expression na Abuse of the freedom.

Sasa huwezi kukaa mbele za watu na kucheza komedy kama wazanzibari wote ni gay, halafu ukaratajia jamii iendelee kufurahi.

Sasa na sisi huku Zanzibar tukianza kuact film za kuwa wamasai ni gay, kwa kisingizio mmasai mmoja alibakwa na mtaliano?Utasema nini kwenye film kama hii?

Acha pumba get your points straight!Huwezi kutoa mfano wa ndoa ukafananisha na muungano, halafu ikawa kila ukifanya hivyo mifano yako Zanzibar ndio jike.Halafu ukasema ati hiyo ni inferiority complex tuu...lakini huu mfano ni sawa.

Hapa kuna mambo mawili: Nia ya mtoa mfano na watafsiri wa huo mfano. Nimewahi kusikia kuwa Muungano unafananishwa na NDOA, tena siku hiyo Mh. Juma Duni Haji alikasirika mpaka wanapanelist wote kwenye kipindi cha TBC1 cha "This Week in Perspective" walimshangaa! Mtoa mfano alikuwa na nia njema, kwa mawazo yangu, lakini Juma Duni Haji, kwa maoni yangu, ali-over react, nafikiri mawazo yake yalihamia kwenye Tanzania Bara kuwa Dume na Zanzibar kuwa Jike. Kwa hiyo basi wewe unaona mfano bora ni upi? Ndoa-Huku Tanzania Bara ikiwa DUME na Zanzibar ikiwa DUME vile vile? Huo mfano ni mzuri? Huko kuhamisha mawazo ndio inferiority complex. Na hao ZeComedy hawajawahi kuigiza mambo ya u-gay, kama yapo elezea ilikuwa ni lini na ilikuwaje!
 
umenena kweli tupu,zenj inawenyewe na wenyewe mtawaona kuanzia kesho 20/1/2010 ktk baraza la wawakilishi wataamua mambo yao wenyewe,tusiwaingilie,makamba domo kaya kila mtu anajua,

Kauli hizi (in red) ni za chuki na ubaguzi!
 
Hapa kuna mambo mawili: Nia ya mtoa mfano na watafsiri wa huo mfano. Nimewahi kusikia kuwa Muungano unafananishwa na NDOA, tena siku hiyo Mh. Juma Duni Haji alikasirika mpaka wanapanelist wote kwenye kipindi cha TBC1 cha "This Week in Perspective" walimshangaa! Mtoa mfano alikuwa na nia njema, kwa mawazo yangu, lakini Juma Duni Haji, kwa maoni yangu, ali-over react, nafikiri mawazo yake yalihamia kwenye Tanzania Bara kuwa Dume na Zanzibar kuwa Jike. Kwa hiyo basi wewe unaona mfano bora ni upi? Ndoa-Huku Tanzania Bara ikiwa DUME na Zanzibar ikiwa DUME vile vile? Huo mfano ni mzuri? Huko kuhamisha mawazo ndio inferiority complex. Na hao ZeComedy hawajawahi kuigiza mambo ya u-gay, kama yapo elezea ilikuwa ni lini na ilikuwaje!
Huwezi kufananisha muungano na ndoa, tafuta mfano mwengine au kaa kimya.
Hao ZeComedy ni watovu wa nidhamu, wanafananisha askari wa Zanzibar kuwa ameregea.Sasa nani atakubali hili?Au anazungumza kama mwanamke...sasa nini maana yake?Au unataka mpaka waanze kuact porno ndio uanze kukemea?

Wewe naona kama ni muflis wa hoja.Hujajibu ungelisema vipi kama nasi Zanzibar tukianza kuact film za kimasai na wataliano huko mahotelini...umeiruka hii, najua sio bahati mbaya umefanya kwa makusudi.
 
Mambo ya Zanzibar hatuwezi kuwaachie tu wenyewe as if Zanzibar siyo sehemu ya Muungano. Wanaongea tu sasa hivi lakini ngoja kutokee tatizo huko tuone kama SMT haitaombwa msaada. Tatizo kuna baadhi ya watu ni wanafiki na wanaogopa kusema ukweli. Bottom line is as long as Zanzibar ni part ya muungano hakuwezi kikaendelea chochote kule tukasema tuwaachie tu wenyewe. Kinacho tokea Bara kina affect Zanzibar na kinacho tokea Zanzibar kina affect muungano. Be honest people.
hivi mbona tukiuwana huwa hamuinngilii? badili yake mnaongeza majeshi na polisi wazidi kuuwa (kumbuka enzi za mkapa na maandamano), mambo ya zanzibar mnayaingilia mkiona tunapatana tu?. tuachieni tu! kwavile hata tukiuwana huwa hamna msaada wowote!
 
Hii thread inanikumbusha ule usemi wa mtoto akililia moto, apewe - atajifunza tu pale atakapochomwa na kuuonja uchungu, hataulilia tena moto. Pia akililia wembe mpe umkate pale pale, atakoma kulilia vitu vya hatari.

Wasioijua vizuri historia ya mapinduzi ya Zanzibar nawatahadhrisha tu muwe makini na kila king'aacho, si lazima kiwe dhahabu. Mtoto aweza kuwa ana tabia ya kuchezea kinyeshi, dawa ni kumpa ugali wa moto, atakoma.
 
Hii thread inanikumbusha ule usemi wa mtoto akililia moto, apewe - atajifunza tu pale atakapochomwa na kuuonja uchungu, hataulilia tena moto. Pia akililia wembe mpe umkate pale pale, atakoma kulilia vitu vya hatari.

Wasioijua vizuri historia ya mapinduzi ya Zanzibar nawatahadhrisha tu muwe makini na kila king'aacho, si lazima kiwe dhahabu. Mtoto aweza kuwa ana tabia ya kuchezea kinyeshi, dawa ni kumpa ugali wa moto, atakoma.

Wala humtishi mtu, Zanzibar ni kongwe zaidi ya Tanganyika.Kwa maana hiyo limeishi likiwa kama taifa la Zanzibar kwa miaka mingi, wakati Tanganyika hata haijazaliwa.

Sasa hapa kuleta story za wembe na mtoto sijuwi unataka kumtisha nani?Wazanzibari?....naona bora uelekeze makombora huko Tanganyika ndio ambao wana woga wa kuvunjika muungano.

Huku visiwani tutasherehekea sana ukivunjika.
 
Huwezi kufananisha muungano na ndoa, tafuta mfano mwengine au kaa kimya.
Hao ZeComedy ni watovu wa nidhamu, wanafananisha askari wa Zanzibar kuwa ameregea.Sasa nani atakubali hili?Au anazungumza kama mwanamke...sasa nini maana yake?Au unataka mpaka waanze kuact porno ndio uanze kukemea?

Wewe naona kama ni muflis wa hoja.Hujajibu ungelisema vipi kama nasi Zanzibar tukianza kuact film za kimasai na wataliano huko mahotelini...umeiruka hii, najua sio bahati mbaya umefanya kwa makusudi.

Tatizo halipo kwenye mfano bali mtoa mfano anakusudia nini! Hata hivyo wazenj kwa kuwa mnajisikia vibaya sidhani kama kuna mtu ataendelea kutumia mifano hii! Hata ZeComedy walishaona huko hakusomeki, walishaiona njia! Hawabonyezi tena "kizenj, bonyeee!"
 
Tatizo halipo kwenye mfano bali mtoa mfano anakusudia nini! Hata hivyo wazenj kwa kuwa mnajisikia vibaya sidhani kama kuna mtu ataendelea kutumia mifano hii! Hata ZeComedy walishaona huko hakusomeki, walishaiona njia! Hawabonyezi tena "kizenj, bonyeee!"
Hata zenji ziko komedy za kuonesha wamasai wanavyoweka mikuki pembeni ...na wataliana wakifanya mambo yao yale ya kaumu Luti :D
 
Kwani hao Wazanzibari tumewashika vinywa vyao mpaka mseme tunawaingilia? Yetu ni maoni tu, wao ndio wenye final say! Huko kwenye Baraza la Wawakilishi watakaa wenyewe Wazanzibari! Seif aache woga usiokuwa na maana! Woga wake ndio unaowafanya watu waulize maswali mengi zaidi, that man is too defensive! Kwani haya ni mambo ya misahafu ambayo hakuna kuuliza maswali? Na hivi Karume akifariki (hatuombei anyway) ina maana hicho "kizuri" alichokianzisha kitakufa vilevile? Na kama hicho "kizuri" kinamtegemea Karume na Seif pekee, hakitadumu, labda Seif na Karume waishi milele!
Sorry huwa sipendi sana kuongea ili ambalo nalindika NA kwa kweli nasikitika kuongea hivi ila ni ukweli usiopingika kwamba watu wa bara(WANYAMWEZI au WATANGANYIKA)kawaida yenu huwa hamuna maoni mazuri juu ya ZNZ sababu mnazijua wenyewe na mtazikwa nazo.mimi ninavojua mnaroho mbaya na niwachoyo sana na ni mafisadi.kawaida mkitoa maoni iwe radioni aumtandaoni kama hivi mnaona wazanzibari kama hawana akili na mnaona sijui kwa nini wakushindeni nyinyi ki ukweli wazanzibari hamuwashindi kwa chochote na kwa lolote wako juu kwa kila kitu tatizo lao walikosea na wameamua kujirudi wameshaamua kuelewana acheni chokochoko zenu na nakuhakikishieni HATURUDINYUMA.
 
Wala humtishi mtu, Zanzibar ni kongwe zaidi ya Tanganyika.Kwa maana hiyo limeishi likiwa kama taifa la Zanzibar kwa miaka mingi, wakati Tanganyika hata haijazaliwa.

Sasa hapa kuleta story za wembe na mtoto sijuwi unataka kumtisha nani?Wazanzibari?....naona bora uelekeze makombora huko Tanganyika ndio ambao wana woga wa kuvunjika muungano.

Huku visiwani tutasherehekea sana ukivunjika.


Wakati mkisherehekea msiende Morogoro na Kyela kutafuta mchele wa pilau na kutumalizia chakula chetu kama mfanyavyo kila mwezi Julai.
 
Mambo ya Zanzibar hatuwezi kuwaachie tu wenyewe as if Zanzibar siyo sehemu ya Muungano. Wanaongea tu sasa hivi lakini ngoja kutokee tatizo huko tuone kama SMT haitaombwa msaada. Tatizo kuna baadhi ya watu ni wanafiki na wanaogopa kusema ukweli. Bottom line is as long as Zanzibar ni part ya muungano hakuwezi kikaendelea chochote kule tukasema tuwaachie tu wenyewe. Kinacho tokea Bara kina affect Zanzibar na kinacho tokea Zanzibar kina affect muungano. Be honest people.

Ni kweli kuwa Zanzibar in sehemu ya Muungano lakini tutapotosha ukweli kama tutailinganisha Zanzibar na sehemu nyingine za Muungano kama Mwanza, Mafia, Dar es salaam na mikoa mingine.

Zanzibar ni sehemu ya Muungano kama mbia (partner) sawa wa Tanganyika na ndio maana wana Serikali yao wenyewe, Rais wao, Waziri Kiongozi, Baraza la wawakilishi na vyombo vingine vya dola ambavyo huwezi kuvipata sehemu nyingine yoyote ya Muungano kama nilizozitaja hapo juu. Wana haki ya kuamua mustakabali wa nchi yao kwa uhuru bila kuingiliwa hata kama utakuwa na maana ya kujitoa katika Muungano au kuubadilisha muundo wa Muungano.

Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ni haki ya wazanzibari wenyewe na sio sehemu ya masuala ya Muungano. Na kwa kuwa Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar unawahusu wazanzibari wenyewe (Mtanganyika hana haki na wala huwezi kupiga kura kumchagua Rais wa Zanzibar) ni vyema wakaachiwa waamue watamchagua kwa staili gani. Hata kama wataamua wawe na Rais wa maisha kwa Zanzibar kama (kama ilivyo Muamar Ghadafi kwa Libya) hiyo ni haki yao.

Kama kuongeza muda wa Rais Karume kutasaidia kuleta uchaguzi huru na wa haki kwa Wanzanzibari wote na kuondokana na migogoro, chuki, mauaji na mambo yanayofanana na hayo, mimi nawaunga mkono kwa asilimia 100%. Ila ni vyema makubaliano yao yakawekwa hadharani ili wazanzibari wajue ni mambo yapi yamekubaliwa.

Naungalia muafaka wa Rais Karume na Maalim Seif Sharif kama fursa mzuri wa Wazanzibari kuangalia upya Katiba yao, sheria za uchaguzi na mfumo mzima wa kuendesha chaguzi zao ili waunde mfumo mzuri zaidi wa kupata watetezi wa maslahi ya nchi yao.

Wanaweza kuachana na huu usanii wa kisiasa unaoendelezwa Tanzania kwa jina la Demokrasia ya Vyama vingi ambapo chama pekee chenye uhuru na haki ya kuchaguliwa ni CCM.
 
Kwani hivyo vijikura viwili kutoka Zanzibar vinaweza kubadili matokeo JK asishinde?


Subiri kesho tarehe 20, sikiza mambo ya bunge la Zanzibar.Hizo hoja za mseto pamoja na futa zitajadiliwa upya.Kama bado una mawazo mgando ya kutishana, bai naona kama uanze kukaa mkao mpya wa kutega sikio.

Jumbe na Salmin hawa watu wote hawakuwa na support ya wazanzibar.Hii issue ya Karume kuongezwa muda inahitaji 2/3 ya BLW.




Sasa ndugu yangu unajua kama Zanzibar ni taifa kongwe zaidi ya hiyo Tanganyika?Maana unafananisha Mafia na Zanzibar, uko makini lakini?
Hilo la serekali moja lilimshinda huyo Nyerere ambae alikuwa anamkaribia Adolf Hiltler kwa ukatili na udikteta.Jee ataweza JK?Kwanza hebu naanze na kufukuza kazi hao wahusika na mafisadi, halafu ndio tutaweza kusema muna rais mwenye msimamo.

Mie personally, taifa langu likipotea na kufanywa mkoa basi niko tayari kujifunga bomu na kujiripua sehemu yoyote ya Dar :D


Hoja zako tangu mwanzo kwa mwenye akili zake alifahamu nini kilichoko kichwani mwako. Zanzibar ikifanywa mkoa utajifungia bomu ukajilipue Dar. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano, Zanzibar ni sehemu ya Muungano. Maana ya sehemu ni kama MKOA au Wilaya. Kilimanjaro, Tanga, Arusha, Kigoma, Tabora na n.k. ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano, kwa hiyo Zanzibar nayo kama sehemu ya Jamuhuri ya Muungano ni Mkoa kwenye JMR ya Muungano kama ilivyo mikoa mingine SASA NJOO HAPA DAR LEO HII UJILIPUE
 
Hoja zako tangu mwanzo kwa mwenye akili zake alifahamu nini kilichoko kichwani mwako. Zanzibar ikifanywa mkoa utajifungia bomu ukajilipue Dar. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano, Zanzibar ni sehemu ya Muungano. Maana ya sehemu ni kama MKOA au Wilaya. Kilimanjaro, Tanga, Arusha, Kigoma, Tabora na n.k. ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano, kwa hiyo Zanzibar nayo kama sehemu ya Jamuhuri ya Muungano ni Mkoa kwenye JMR ya Muungano kama ilivyo mikoa mingine SASA NJOO HAPA DAR LEO HII UJILIPUE
Kwani 98 hatukufanya hivyo?Pili hiyo kusema ati Zanzibar ni mkoa, hiyo itakuwa ni ndoto zako tuu.Sifikirii kama Tanga kuna serekali ya Tanga, lakini Zanzibar tuna serekali yetu na sisemi mambo yote lakini yapo mambo mengi tuu ikiwemo mafuta tunaweka mkwala...na hamufanyi chochote.

Juzi tuu Karume alimwambia JK kama mafuta ni ya Zanzibar...sherehe za mapinduzi, na leo tayari serekali yetu adhimu inajadili formula na mikakati ya mafuta.

Na nyie endeleeli na choko-choko zenu...lakini hizo hazimfanyi mwenye nyumba asipate usingizi.
 
[/COLOR]

Wakati mkisherehekea msiende Morogoro na Kyela kutafuta mchele wa pilau na kutumalizia chakula chetu kama mfanyavyo kila mwezi Julai.

Tanzania (98% Tanganyika) sioni cha kujivunia...mtu mzima umekuja na hoja ya mchele.:rolleyes:

Europe watu wanakula mchele daily, na wala hautoki Tanganyika.Sijawahi kuenda supermark yoyote duniani, nikaona product made in Tanzania...sorry bout that.

Lakini kusema ndio muungano uvunjike mususe kuuza mchele wenu au umeme wenu huko visiwani, sijuwi nani ataathirika?...keep in mind Zanzibar is a client with money to buy those products!!
 
Kwani hao Wazanzibari tumewashika vinywa vyao mpaka mseme tunawaingilia? Yetu ni maoni tu, wao ndio wenye final say! Huko kwenye Baraza la Wawakilishi watakaa wenyewe Wazanzibari! Seif aache woga usiokuwa na maana! Woga wake ndio unaowafanya watu waulize maswali mengi zaidi, that man is too defensive! Kwani haya ni mambo ya misahafu ambayo hakuna kuuliza maswali? Na hivi Karume akifariki (hatuombei anyway) ina maana hicho "kizuri" alichokianzisha kitakufa vilevile? Na kama hicho "kizuri" kinamtegemea Karume na Seif pekee, hakitadumu, labda Seif na Karume waishi milele!
Definately you are right.kila mwisho wa mwaka Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania anawashukuru watanzania kwa kudumisha amani na Utulivu.jirani zetu wanatusifu watanzania kwa Undugu.kwaiyo amani ya wazanzibar inaletwa na wananchi wa zanzibar na siyo karume na Seif.kwani zanzibar nzima wasomi au wenyeuwezo wa kuongoza ni wawili tu?. Mimi nafikiri kujadili karume aendelee nikupoteza muda tu.Hizo ni mawazo mgando. Juzi juzi tu rais wa Niger amepindua katiba kajiongezea muda eti anamaliza miradi aliyoanzisha. miradi yenyewe ni makampuni ya China kumalizia kuchimba gesi.serikali ya China ilikuwa na wasiwasi ni mrithi wake kwa sababu wanahisi atabadilisha mikata yao ya kinyonyaji.Yoweri naye kaanza bado kagame . huku ni kujiinua kuliko wengine. ambalo ni kosa. kwanza seif amegombea tayari mara tatu apishe wengine. Nafikiri cuf ni muhimu kuliko seif.Au tuseme bila seif na karume hakuna cuf na CCm zanzibar
 
Ndugu zangu kama mlikuwa hamjui sasa mjue hili. Kuna mkono wa Marekani katika muafaka kati ya Seif and Amani. Hii ni kutokana na ukweli kuwa baadhi ya Wazanzibar waliokimbilia Somalia kuna baadhi ambao hawajarudi na wamejiunga na Alshabab na wamefundishwa mambo ya kushambulia kwa mabomu na wangetekeleza mauaji makubwa sana wakati wa uchaguzi. Sas ingetumika kigezo kuwa ni watu wa CUF kumbe sio, sasa ukishakuwa na watu wa CUF na CCM wanaelewana ni rahisi kugundua hawa Alshabab. Inahisiwa hata nyumba zilizochomwa walihusika....
 
Back
Top Bottom