JEMBA NIMEFURAHISHWA SANA NA MAENDELEO YALIYOFANYIKA..LAKINI UNAJUA PESA ZA KULETA HAYO MAENDELEO ZILITOKA KWENYE UTUMWA ,MASHAMBA YA WAARABU YA KARAFUU YALIYOLIMWA NA WATWANA WEUSI,KODI YA MELI/VYOMBO VILIVYOPITA UNGUJA,na pia tukumbuke himaya ya zanzibar ilikuwa pamoja na OMAN,kwa hiyo bila shaka pesa nyingi pia ilitoka oman.
lakini unapojivunia umeme na majumba ya sultan ukumbuke kando tu maeneo ya michenzani kwenda mbele miaka hiyo zilisheheni MBAVU ZA MBWA za kina KABWELA!
LAKINI napata wazo...kuna watu wanafikiri pamoja na dhuluma zote zile ,bora SULTANI,sasa hiyo ina maana serikali ya mapinduzi zanzibar haijafikia matarajio ya wengi?


mkuu PM tukubaliene kuwa watawala wa wakati ule walijitahdi kuleta maendeleo zanzibar na kutokana na idadi ya watu wake kwa wakati ule maendeleo yalukuwa makubwa ukichukua kwa ratio ile ile na leo.

mie ni mmoja ninaeiamini na kuipenda sana ASP, lengo la awali la ASP ilikuwa ni kunyanyua hali za wazanzibari na hasa sisi waafrika.

kama utarejea maendeleo ya lioletwa na ASP yalikuwa ni mwendelezo mwema wa kuleta maendeleo kwa zanzibar, lakini kila siku zilipokuwa zikisonga mbele ndipo hali ilipochafuka, na hapo ndipo tunapodai huu muungano ulisaidia vipi kurekebisha hali ya zanzibar zaidi ya kuibana na kuupora uchumi wake.

nnaweza kusema baada ya rais wa kwanza wa mapinduzi hadi leo zanzibar ilianza kurudi nyuma kwa speed ile ile iliokuwa ikisonga mbele.


omani na zanzibar zilikuwa ni nchi mbili mbali mbali kwa kuruni, rejea historia mwalimu mikaeli.

na utumwa uliisha zamani , waliirithi afroshirazi zanzibar ilioneemani, ila twaamini muungano ulisaidia kuifikisha zanzibar hapa tulipo leo. imezalisha watu wasio na uchungu na nchi, na ikitokea wenye uchungu au kutaka kurekebisha walipokosea walikiona cha moto kwa mkono wa muungano.

nnawapa sana pole marais wetu Idriss Abdul wakil(mchango wako hatutousahau na mola akulipe mazuri huko uliko)

pia Mheshimiwa ABoud Jumbe(mola atakusamehe kwa ulioteleza na tunakupongeza kwa yale mema uliolifanyia taifa lako)

pamoja na Dr Salmini amour na Wewe mh Amani karume
 
Kuna watu wanataka tuamini kuwa "utumwa ulikuwa mzuri kwa Zanzibar" na mabwana wale walikuwa watu wema kweli... Wanaolilia "ile Zanzibar" ya kale.. wanakumbuka jinsi walivyokuwa wakitetemekewa kila wakipita.! Uchungu wa mapinduzi ya Zanzibar ni mtumwa kawa mfalme!!!

Si mnaona seneta Obama hapa anapewa ulinzi sasa baada ya KKK kuchukizwa na uwezekano wa jamaa kuwa Rais wa kwanza mweusi (hata kama amechangia)! Huko Zanzibar kuna watu ambao hadi leo hawaamini kuwa watu weusi wanaongoza visiwa hivyo!! Kumbukeni pia kuwa ukichanganya damu ya kiarabu na wewe mwarabu...!
 
mkjj
nnakuheshimu sana, na nnaamini ni mtu usiyeongozwa na hoja za kiza, ila sasa nnaona umeanza kupotea.

hivi utumwa uliisha lini kule zanzibar? 1964? jeee baada ya utumwa wapi zanzibar walifikia kimaendeleo? halafu jee unajua kuwa karibu nusu ya wafalme wa zanzibar ni watoto wa watumwa? kama hulijui hilo nnaomba uendelee kufanya utafiti.

suala si uarabu kama ni uarabu ndio suala basi mwarabu sasa yuko ikulu zanzibar au hujui kuwa mama yake karume ni mwarabu ? bi Fatma karume.

nyie kwa nini hasa mnapenda kukumbushia utumwa tunapotaja kuwa muungano ulitukandamiza.?

zanzibar tattizo la utumwa liliisha tokea karne ya kumi nane na unalijua ila unataka kubabaisha tu. hoja yetu iko pale pale kuwa muungano umeiimiza zanzibar sana tu.

maana baada ya muungano hali ya zanzibar imeendelea na kuendelea kuwa mbaya. kiasi ambacho lazima tukubali malengo ya mapinduzi hayakufikiwa, na hapa tulipo ni pabaya zaidi kuliko alipotuacha mkoloni. sasa kosa liko wapi? tungalipenda kuwa ktk hali ilio bora kuliko wakati ule.

kuna kipindi rais wetu wa kwanza aliweza kusema tuna kiasi gani akiba ya pesa za kigeni na hatudaiwi leo jeuri hiyo hatuna, tulikusaidieni hata nyie ndugu zetu wa mrima leo uwezo huo hatuna.

hili ndilo linalotufanya tuamini lazima tukae tuzungumze maana wazanzibari tumetolewa kwenye mstari wa kuwahudumia wananchi wetu.

hatuna budi kukaa na kuangalia upya huu mmungunyuano, na hasa katika maeneo tulioyaeleza huko juu.
 
Communal%20Labor%20helps%20build%20apartments%20c197x.jpg
 
haya ni machache ambayo ASP iliweza kufanya mwanzoni, leo hii SMZ hyaina jeuri hiii, acha kabla ya ASP
 
Topic ulizoainisha hapo juu zitaunganishwa, lakini kwa wakati huu endelea kuchangia kama zilivyo.
 
Dr who
nnaunga mkono hoja, ziunganishwe ili mchangiaji aweze kuwa na mtiririko mziri wa mawazo.

Mh. Ole nahisi wazo ni zuri, maana hata mKjj atapata kuelewa kuwa, hapa watu hawazungumzii utumwa na biashara ya pembe za ndovu yeshapita yale, tunaangalia kizazi hiki na kinapopelekwa na muungano huu
 
jamani mimi nakubaliana na Mwanakijiji kwamba hiyo HIMAYA ya ZNZ iliyokuwa imepiga hatua kubwa ya maendeleo ilijengwa kwa jasho na damu ya WATUMWA kutoka TANGANYIKA.

Yuko aliyedai kwamba kuna baadhi ya watawala wa ZNZ walikuwa wa mzao wa watumwa. Mimi naomba kuelekezwa SULTANI mmoja tu wa ZNZ ambaye BABA yake alikuwa MTUMWA.

Wakati tunaungana wote Tanganyika na ZNZ tulikuwa na hali nzuri ya kiuchumi. Sote kwasababu moja au nyingine tumeanguka kiuchumi. Itakuwa jambo la msingi kama tutajichunguza wenyewe, na kutafuta sababu za ndani, kwanini, Tanganyika, au ZNZ, imeanguka kiuchumi, na kudorora kimaendeleo.

Tumekuwa tukisikia habari za ZNZ kuilalamikia TRA kwamba ndiyo "mchawi" aliyeua uchumi wa ZNZ. Lakini hii TRA imeanza kazi mwaka 1995/96. Sote tunaelewa kwamba hata kabla TRA kuanzishwa hali haikuwa nzuri ZNZ. Kinachoshangaza hakuna anayehoji suala hilo.

Wazanzibari wajichunguze wenyewe, badala ya kulalamikia kwamba kila tatizo walilonalo limetokana na muungano na Watanganyika.
 
mkjj
nnakuheshimu sana, na nnaamini ni mtu usiyeongozwa na hoja za kiza, ila sasa nnaona umeanza kupotea.

hivi utumwa uliisha lini kule zanzibar? 1964? jeee baada ya utumwa wapi zanzibar walifikia kimaendeleo? halafu jee unajua kuwa karibu nusu ya wafalme wa zanzibar ni watoto wa watumwa? kama hulijui hilo nnaomba uendelee kufanya utafiti.

suala si uarabu kama ni uarabu ndio suala basi mwarabu sasa yuko ikulu zanzibar au hujui kuwa mama yake karume ni mwarabu ? bi Fatma karume.

nyie kwa nini hasa mnapenda kukumbushia utumwa tunapotaja kuwa muungano ulitukandamiza.?

zanzibar tattizo la utumwa liliisha tokea karne ya kumi nane na unalijua ila unataka kubabaisha tu. hoja yetu iko pale pale kuwa muungano umeiimiza zanzibar sana tu.

maana baada ya muungano hali ya zanzibar imeendelea na kuendelea kuwa mbaya. kiasi ambacho lazima tukubali malengo ya mapinduzi hayakufikiwa, na hapa tulipo ni pabaya zaidi kuliko alipotuacha mkoloni. sasa kosa liko wapi? tungalipenda kuwa ktk hali ilio bora kuliko wakati ule.

kuna kipindi rais wetu wa kwanza aliweza kusema tuna kiasi gani akiba ya pesa za kigeni na hatudaiwi leo jeuri hiyo hatuna, tulikusaidieni hata nyie ndugu zetu wa mrima leo uwezo huo hatuna.

hili ndilo linalotufanya tuamini lazima tukae tuzungumze maana wazanzibari tumetolewa kwenye mstari wa kuwahudumia wananchi wetu.

hatuna budi kukaa na kuangalia upya huu mmungunyuano, na hasa katika maeneo tulioyaeleza huko juu.

Je, kuporomoka kwa bei ya karafuu katika soko la dunia, zao pekee la biashara lililokuwa likiingizia Zanzibar pato haina mchango wowote katika kurudisha uchumi wa Zanzibar nyuma?

Wasukuma wa Shinyanga na Mwanza walima pamba mashuhuri enzi zile wakati bei ya pamba ilipokuwa dhahabu nyeupe ukiwauliza leo watakwambia kwamba walikuwa na maendeleo mazuri sana wakati huo. Ni hivyo hivyo, wakerewe watakwambia kuwa uvuvi wa samaki ulikuwa wa maana sana hata kuweza kuwasomesha watoto wengi walioweza kwenda mbele zaidi, na kusemwa kuwa ni kwa sababu ya kula vichwa vya 'furu' (smaki mdogo). Sehemu za nchini kote kulikokuwa kunalimwa kahawa, watu walikuwa wanayo maisha mazuri tu kuliko leo. Sasa kwa hayo yote, leo tusingizie sababu ya muungano ndio uliorudisha maendeleo nyuma?

Hata hivyo, mimi nitakubaliana na mtu yeyote atakayependekeza kura ya maoni pande zote za muungano kuhusu kuendelea kwa huu muungano.

Wanaopendekeza serikali tatu hebu fikiria gharama za uendeshaji huu:
1. Serikali ya Muungano
2. Serikali ya Tanganyika
3. Serikali ya Unguja
4. Serikali ya Pemba (why not?)
5. Serikali ya Afrika Mashariki (inakuja)

kusema kweli hailete picha nzuri hata kidogo kwa kuendelea kung'ang'ania muungano bila ya kujali malalamishi ya sehemu moja ya muungano huu. Mwishowe watu wataamini kwamba kweli kuna sababu inayonufaisha sehemu ya bara zaidi.
 
source :
http://www.zanzinet.org/zanzibar/economy/sekta.html

Major Economic Sectors

--------------------------------------------------------------------------------


Agriculture
Zanzibar enjoys a cool tropical climate favourable for the production of many warm-climate crops but clove trees have largely filled its landscape, particularly on the island of Pemba. For many years, it was the leading producer of cloves in the world but the age of clove trees, diseases, agronomic- and a number of human-related factors have caused a steep decline in the annual production levels. Clove trees thrives best in deep soils on western sides of both islands. Other major cash crops are coconuts, chillies, and recently seaweed. There are also other crops such as black pepper, cinnamon and vanilla but due at the moment they are not produced in quantities that could warrant export to outer world.

Farming for food production is also a major activity for the majority of Zanzibaris. Major food crops include rice, cassava, sweet potatoes, bananas, plantains, yams and cocoyams. The staple food of Zanzibar is rice and due to high demand much of it is imported. Like cloves, agricultural production in Zanzibar is concentrated more on the deep soil areas whereas the coral rag is popular for root crops and other drought tolerant or seasonal crops. Fruits such as mangoes, pineapples, oranges, dorians, jackfruits, and many more are available but due to seasonal shortages and high demand they are imported from the mainland. Vegetables are mostly imported from the mainland but a number of green leafy vegetables are produced locally.

Production of livestock products to feed the local market in Zanzibar has increased markedly in recent years. With the exception of beef supplies for the Zanzibar urban market, production of milk, eggs, and poultry meat almost meet the demand. Due to high demand, particularly in Zanzibar town, cattle are imported from mainland of Tanzania, quaranteened and tested for diseases at a government centre of Kisakasaka before being slaughtered for public consumption. Mutton and goat meat are available in local markets but they are less popular and their supplies are not closely monitored. Pemba is almost self-sufficient in livestock products compared to Unguja. Livestock hides and skins are either processed locally into sandals (Makubadhi) or exported.


Trade and Industries
Much of Zanzibar's involvement in trade has been presented earlier due to its central role in the history of the archipelago. Briefly, Zanzibar prospered in the past due to maritime trade involving slaves, spices, ivory and gold. These items, were the glory of the past and no longer applicable to today's Zanzibar. Slavery is history and the interior that used to supply ivory and gold is no longer under her control.The Revolutionary Government of Zanzibar (RGZ) initially closed doors for its citizens wishing to pursue trading opportunities to external world. It instead championed a move of launching a number of factories producing consumer goods such as shoes, cigarettes, soaps and oils, household items, sugar, perfumery and spirits. None of these survived the economic downturns and the government has to bear the burden of keeping thousands of people who once worked for these factories. It also established two public corporations, BIZANJE for importing consumer commodities into the isles and Zanzibar State Trading Corporation (ZSTC) for marketing cloves and other cash crops to the world markets. BIZANJE is now defunct and during the Ali Hassan Mwinyi's period as president of Zanzibar, a program of trade liberilization allowed private entrepreneurs to get involved with the business of importing consumer commodities into the country. ZSTC is still operating but recently there were reports that the government is about to yield into pressures to either completely close its business or transform it into a mere facilitating agency.

Trade liberalization is a welcome policy for Zanzibar businessmen but there is a lot to be done if trade is to deliver the expected benefits for people of Zanzibar. During the early days of its operation, this policy gave businessmen a big boost in revenue mainly by utilizing the large market in mainland Tanzania. Nevertheless, when the union government also followed suit and liberalized its economy, Zanzibar faced an upward hurdle. It became more serious when Zanzibar was forced to harmonize its tax and tarrifs in accordance with those set forth by the Tanzania Revenue Authority (TRA). Therefore, the relaxation of trade restrictions seems to be having little impact to the economy of Zanzibar. Furthermore, there are also concerns on the way the whole sector is organized and the chances of trade replacing the clove industry are very slim.
 
haya ni baadhi ya maneno ya wabunge wetu huko zanzibar wakiwa bungeni.

huyu ni mbunge wa DOLE
source:http://www.parliament.go.tz/bunge/ContrLst.asp?Menu=Contr&PTerm=2005-2010&vpkey=1205&page=2

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kidogo kuhusu uchumi hasa uchumi wa Zanzibar. Kabla sijasema, ninataka nimnukuu Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano alipokuja katika Bunge. Alisema hivi: “Nitaangalia upya mchango wa Serikali ya Muungano katika maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii ya Zanzibar bila kuathiri haki na mamlaka kamili ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mambo ambayo siyo ya Muungano.”

Sasa hili nimeliangalia humu, nimekuta ule mgawanyo tu wa misaada kutoka nje, sasa hivi Zanzibar inapata mtihani mmoja, mtihani mmoja uko kwenye Muungano. Lazima unapokuwa katika Muungano, uridhie na mambo ya mwenzio hata kama hayo siyo wewe yanayokufaidisha. Lakini, keshokutwa tunaingia katika Afrika Mashariki. Tunazungumza Afrika Mashariki na kila kitu. Tunasema, Mwalimu alisema kwamba kuna hatari nchi ndogo ikamezwa na kubwa. Lazima tuambiane ukweli, nchi ndogo ikamezwa na kubwa.

Zanzibar hivi sasa hali yake ya uchumi siyo nzuri tukubaliane ndugu zangu. Siyo nzuri, pengine kwa sababu hakuna namna ya kutoka pale, maana kodi zinazowekwa hapa na Jamhuri ya Muungano, ndiyo kodi zinazotumika Zanzibar. Hivi tunaulizana, wananchi wa Zanzibar tuseme wako milioni moja. Kama kuna tajiri anaamua kuleta televisheni milioni moja, basi ina maana kila mmoja lazima anunue moja moja mpaka mchange, zitakazobakia kama milioni mbili atanunua nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lazima tukubali kwamba wananchi wa Zanzibar kwa vyovyote vile uandaliwe mkakati, soko lao liwe Tanzania Bara. Tukubaliane hivyo. La sivyo, viwango vya kodi vya Zanzibar viwekwe vya tofauti, na kama siyo hivyo ujengwe mkakati maalum wa kusaidia. Kwa mfano, Afrika Mashariki kuna mambo mengi hivi sasa yanakuja na yatasadia Jumuiya ya Afrika Mashariki na yatasaidia hao wananchi milioni 30. Lakini hao watu milioni moja ambao wako pale Zanzibar wanasaidiwa vipi? Wanafaidika vipi na Muungano? Maana wananchi wa kawaida hawataki Uwaziri Mkuu hawataki Ubunge, hawataki Uwaziri, wao wanataka kufaidika na maisha yao vizuri. Hali za wale Wazanzibari wale sio nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, njia ya kwanza ambayo ningeomba, Bandari ya Zanzibar iwe bandari huru katika Afrika Mashariki na Afrika Mashariki ikibali kwamba Bandari ya Zanzibar ni Bandari huru ili ifanye kazi ya kupokea mizigo yote ya Afrika Mashariki na baadaye isambae katika Afrika Mashariki. Wazanzibari wale watapata kazi na suala la uchumi litakua na Serikali itajiendesha na mgogoro utakuwa hakuna. Si tunagawana! Wewe, kilimo wewe ardhi yako nzuri, wewe na nini, wewe na soko, lakini na wale nao watapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili sijui limefikia wapi! Nilitaka hilo na lenyewe niliweke hapa ili pengine Serikali itakapofanyia kazi, lifanyiwe kazi. Sio lazima lipatiwe jibu. Mnaweza mkalifanyia kazi huko baadaye, sio lazima mseme msimamie. Semeni nyie ndiyo mliosema. Kwa sababu wadogo hawaambiwi hili kasema fulani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo ninataka niliseme ni suala la Utawala Bora. Suala la Mihimili Mitatu:- Mhimili Bunge, Mhimili Mahakama, Mhimili Serikali. Kwa muda wa miaka 40 Bunge, Mahakama, vimetiwa mfukoni na Serikali.

Sasa, Mheshimiwa Rais ana maneno mazuri alisema hapa na nilikuwa namsikiliza na nafuatilia sana. Katika ukurasa wa 22 wa hotuba yake, alisema hivi: “Serikali nitakayoiongoza itazingatia na kuendeshwa kwa msingi wa utawala bora, uwazi na uwajibikaji. Tutaheshimu utawala wa sheria na tutazingatia na kuheshimu mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili mikuu ya dola yaani Utawala, Bunge na Mahakama. Tutaheshimu uhuru wa Mahakama na Bunge na tutatimiza ipasavyo wajibu wetu na tutawezesha.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ukitizama wenzetu wa Serikali na Bunge na Mahakama, kweli tuko sawa sawa! Tukubaliane! Wenzetu wa Serikali wanakusanya kodi na kupanga mikakati. Maana yake mpaka hili Baraza la Mipango na kila kitu wanakubaliana huko, sisi tunaletewa hapa tupitishe Bajeti. Lakini vipaumbele wamepitisha wao. Wanatutia mfukoni wenzetu. Sasa hilo ni jambo ambalo linatakiwa kusawazishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine, Bunge na Mahakama sio chombo cha kuipigia magoti Serikalini katika kuomba Bajeti yake. Kama mwenzio ana uwezo mkubwa na wewe huna uwezo, uhuru huna. Kama yeye anakusanya kodi na halafu wewe unapiga magoti, maana yake Ofisi ya Spika, Bajeti yake iko chini ya Mkurugenzi ambaye yuko Ofisi ya Waziri Mkuu. Sasa, mtaendeshaje mambo yenu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
 
JEMBA NIMEFURAHISHWA SANA NA MAENDELEO YALIYOFANYIKA..LAKINI UNAJUA PESA ZA KULETA HAYO MAENDELEO ZILITOKA KWENYE UTUMWA ,MASHAMBA YA WAARABU YA KARAFUU YALIYOLIMWA NA WATWANA WEUSI,KODI YA MELI/VYOMBO VILIVYOPITA UNGUJA,na pia tukumbuke himaya ya zanzibar ilikuwa pamoja na OMAN,kwa hiyo bila shaka pesa nyingi pia ilitoka oman.
lakini unapojivunia umeme na majumba ya sultan ukumbuke kando tu maeneo ya michenzani kwenda mbele miaka hiyo zilisheheni MBAVU ZA MBWA za kina KABWELA!
LAKINI napata wazo...kuna watu wanafikiri pamoja na dhuluma zote zile ,bora SULTANI,sasa hiyo ina maana serikali ya mapinduzi zanzibar haijafikia matarajio ya wengi?

PM,

duh!! mzee PM hilo mbona liko wazi sana wala halihitaji kurunzi, coz lengo la ASP na serikali yake ilikuwa ni kumkomboa mtu mweusi na kumpa maisha bora zaidi. Kwa hiyo ni wazi kuwa malengo hayo hata theluthi moja haijafikiwa kwani tunaona maisha yalivyokuwa magumu maradufu na vile vile huko kukombolewa hakuko kwani sasa hivi Zanzibar ipo chini ya mkoloni Muungano imebanwa haifurukuti.

Unasema street lights zilikuwa zipo Mji Mkongwe tu?inaonyesha unamakengeza hebu rudia tena kusoma previous post ambayo nimeiweka ndio utaelewa zaidi

Tunafahamu kuwa wakoloni walikuwa wabaya lakini waliweza kuijenga Zanzibar kwa hali na mali mpaka likawa Taifa lenye nguvu barani Africa kwa nini sasa basi chini ya Muungano hilo lishindikane??? na waliweza hata kuleta pesa kutoka Omani kwa lengo la kuijenga Zanzibar
 
Jemba Jemba...

mkuu kama unayo original documents za MUUNGANO wa TZ na ZNZ hebu nitumie ktk PM.

Mtumwitu....

unatisha utafikiri maradhi ya KIFAFA mkuu kwa info zako,heshima mbele tuendelee kukata issue.
 
Jemba Jemba...

mkuu kama unayo original documents za MUUNGANO wa TZ na ZNZ hebu nitumie ktk PM.

Mtumwitu....

unatisha utafikiri maradhi ya KIFAFA mkuu kwa info zako,heshima mbele tuendelee kukata issue.

Engineer,

duh!!! hizo original documents hata Serikali ya Zanzibar haina, mimi nitazipata wapi ???
 
Muungano ni kitu muhimu sana kwa wanadamu wowote wale , wengine wanaungana ni marafiki , wachumba na kadhalika nchi zinaungana na kuwa taifa moja kama Tanganyika ilivyoungana na Zanzibar kutengeneza tanzania , kwahiyo tunatanzania bara na visiwani

Muungano wetu umekuwa kwa muda mrefu lakini wengi wao hawaelewi tumeungana kwa sababu gani haswa , na wengi pia hawaoni sababu za muungano huu kuendelea kuwepo , watu katika mitandao wamepiga kura kutaka kuvunja muungano na kuandika vitu kibao wanachoelewa kuhusu muungano na kadhalika .

Je hawa jamaa waliojitutumua kutengeneza huu muungano walikubaliana nini ? na mbona katika historia ya muungano karume anaonekana kufichwa sana na hata hatajwi sana kama anavyotajwa Nyerere na watu wengine wachache kuna nini kwa karume na jamaa zake wengine wa pemba ?

Hii nayo ni changamoto ya wapemba wenyewe wajieleze kwanini karume hawamtaji sana katika historia hii tata ya muungano , hata wananchi wengi wa unguja wanamwona karume kama msaliti na hata alivyouwawa ile ni sahihi kabisa

Wengine wanafikia hatua ya kusema yeye sio mzanzibari , kwahiyo hakuwa na uhalali wowote wa kukubaliana chochote na nyerere , kama alikuwa anataka ulinzi basi angeomba jeshi liende kumlianda kwa mkataba maalumu sio kuruhusu muungano .

Pia kuna wanaodai karume alishaona kuna kila dalili ya yeye kuuwawa kwa sababu ya visasi vya watu wa visiwani , kwahiyo alihitaji sana muungano kwa ajili ya kuendelea kutawala zaidi yeye na familia yake , hiyo inaeleweka aliuwawa na sasa hivi ni motto wake ndio ameshika hatamu

Kwahiyo katika muungano tusiongelee mambo ya uchumi peke yake au mambo madogo lazima tujue huu muungano ulikwua kwa sababu gani kama ni ulinzi si unaona wakati wa uchaguzi kuna kuwa na jeshi kule visiwani kulinda amani ulinzi tunawapa ? kama masuala ya uchumi , sisi tunaagiza mali nyingi sana kutoka visiwani .

Vitu kama umeme wa kuzalishia viwandani mwao wanautoa Tanzania bara , nasikia kabla ya muunngano znz walikuwa wanauza maji nchi za asia baada ya muungano uchumi umeshuka hawauzi tena maji na bidhaa nyingi katika nchi za asia huu ni uzembe wao wenyewe watu wa sisiwani .

Mtu wa kisiwani anajiona mjanja akienda uingereza kubeba mabox na kuwaletea wajomba zake computer used waje kuuza badala ya kuwekeza katika elimu kwa manufaa ya wakujuu zao wakati ujao na ndio maana sasa hivi wameishiwa hawana mpya na hawana hoja wala ukijenga hoja wanashindwa kuzipangua .
 
Back
Top Bottom