Muhimbili: Madaktari wadai posho, wao si kituo kupitishia vigogo kwenda India

Yaani huu ni kama utani kabisaaa...mimi niliacha kazi Muhimbili mwanzoni mwa mwaka 2006, wakati huo tulikuwa tukilipwa posho hii ya Tshs 10,000 kwa siku unapokuwa zamu. Na zamu ni kuwa unaanza saa 2 kamili asubuhi mpaka kesho yake saa 2 kamili asubuhi (24 hrs)...leo hii mwishoni mwa mwaka 2011 (5 yrs later), pamoja na mabadiliko yoote ya gharama za kimaisha bado daktari analipwa posho ya mwaka 2006! Jamani, si utani huu!!?
Tupe shavu mkubwa.
 
Ni sawa kundi la afya ni dogo sana na yet mhimu sana waongezewe pia posho.
Ni rahisi kupandisha posho/mshahara wa kundi dogo la watumishi kuliko kundi kubwa e.g waalimu.
Hii ni kwa kuzingatia kuwa unapokuwa umepandisha ni irreversible, mtumishi hawezi kukuelewa katika mazingira ya kawaida kumwambia kuwa umeshusha rate ya pay aina yoyote ile.
Haiingii akilini kumlipa mbunge posho ya siku laki mbili..(200,000), hali mshahara wake ni mamilioni, bado posho ya usafiri sijui itaongezwa hadi laki ngapi plus millioni zaidi ya tano/mwezi inayobadikwa jina eti "posho ya jimbo".
Yote hayo mwalimu mashahara wake kwa siku 30 ni pungufu ya 200,000 ambayo mbunge anapata kama masalia mengine kwa siku moja.
Nchi ni yetu sote, lazma kuwe na uwiano wa kuyafaidi matunda ya nchi.
 
Daktari ni daktari tu hakuna cha ubingwa katika madaktari tunaowaona kila siku. Wote wamevaa pima joto shingoni kama kila daktari anavyofanya.

Bingwa ni yule anayepambanishwa na wengine na kisha kuibuka kuwazidi wenzake na hivyo kuwa bingwa kama timu za mpira zinavyochezwa katika ligi kupata bingwa. Sasa hawa madaktari kujiita mabingwa ni kwa itikadi gani? Na walimu wajiite mabingwa kwa vile ndio waliwafundisha somo la sayansi lililowapatia udaktari? Kila mmoja sasa atajiita bingwa kama wanasiasa wanavyojipachika hadhi ya Dr .....
Neno Bingwa limeletwa na TUKI wakimrefer daktari mwenye shahada ya uzamili au zaidi.
 
Kwakuwa wanafikia MoI,if i were a dr ningekua napendekeza wakatwe miguu tu!
Sidhani kama ethics zao zinawaruhusu kufanya hivyo.
Lakini pia kama unahasira nao binafsi unaweza wafanyia chochote unachotaka hata kuwaua ukijisikia sidhani kama wabunge wana ulinzi. tunakunywa nao hata baa za uswazi.
End justfiy the means
 
Madaktari wetu nawaunga mkono lakini kwa hili la kupeleka watu India nawapinga,wengi wa madaktari wetu hawako serious na kazi,hawafanyi kazi kwa weledi na kusababisha mauti kwa wagonjwa wengi nchini.

kiongozi kama waziri ni kiongozi wa kitaifa lazima apate huduma ya uhakika ili kulitumikia taifa, angalia kipindi wamempasua kichwa mgonjwa wa mguu na wakichwa hali kadhalika,utasema una madaktari serious na kazi,tuache unafiki taifa limejaa wataalamu wasiojituma wanalilia hela tuu, hatuna uzalendo kwa watu wetu na kazi tunaona kama upuuzi fulani.

kuna wakati moja ya mtu wa karibu alifanyiwa upasuaji wa mguu. Mguu ukapinda akawa hawezi kutembea baada ya kupelekwa India wahindi wakamtibu wakagundua madaktari wetu walishindwa kuunga mfupa sawasawa na kumsababishia ulemavu, hawa wa India wakamtibu na hadi sasa anadunda kama kawaida, hawana utaalamu hilo walikubali, Moi wamepewa nyenzo zote lakini hakuna kitu pale.


Aliyekuambia India hawana ajali hospitalini alikudanganya. JK hata akifa bado nchi hii itapata raisi mwingine, sana nashangaa kwa nini uone uhai wako si mali kitu kuliko wa RAISI ama Waziri ama mbunge yeyote awaye. Uhai wako una umuhimu sawa na hao unaowaita viongozi wa kitaifa, na pengine uhai wako ni bora zaidi kwa kua hao viongozi ndio wenye wajibu wa kuendeleza tiba nchini.

Viongozi wa kitaifa wakifa bado tutapata viongozi wengine, hivyo viongozi waliopo na raia wengine wote tutibiwe ndani ya nchi ili na waganga wetu wapate uzoefu zaidi na zaidi. Kwa anayependa kujilipia binafsi, kutibiwa popote ruksa.
 

NAIBU WAZIRI: NIMEWASIKIA
“Nimewasikia ndugu zangu wafanyakazi, kuna baadhi ya mambo itabidi niyapeleke kwa wakubwa zangu na mengine nitayajibu hapa,” alisema Dk. Nkya.


Dk. Nkya aliwataka wafanyakazi hao kufanya kazi kwa kujituma wakati Serikali inaendelea kutatua matatizo yao kwa awamu kulingana na uwezo wake wa kifedha.
Shida ya viongozi wote wa Tanzania hawajui maan ya nafasi walizo nazo.
Anakuja kuongea na wananchi hali yeye mwenyewe hajui nini cha kufanya.
Nafikiri kwanza hawa madaktari walipoteza muda wao kumsikiliza huyu mama aliyebandikwa kwenye hicho kiti. Na yeye baada ya kutoka hapo Muhimbili alienda kusaini allowance ya malaki kadhaa huku aikwaacha madokta na miayo.
 
Shida ya viongozi wote wa Tanzania hawajui maan ya nafasi walizo nazo.
Anakuja kuongea na wananchi hali yeye mwenyewe hajui nini cha kufanya.
Nafikiri kwanza hawa madaktari walipoteza muda wao kumsikiliza huyu mama aliyebandikwa kwenye hicho kiti. Na yeye baada ya kutoka hapo Muhimbili alienda kusaini allowance ya malaki kadhaa huku aikwaacha madokta na miayo.

Umefunua ukweli wa yote sina cha nyongeza hapa.
 
"Nimewasikia lakini mimi sio mwamuzi, nitapeleka yote kwa Waziri au kwa Waziri Mkuu atafute ufumbuzi, haya yote mlioniambia," alisema Dk. Nkya.
Hana majibu.. kwanini waziri wake hakuja?.
Naye hangekuwa na majibu.
Basi angekuja na Waziri Mkuu Aliyemtaja kuja kutafuta ufumbuzi.
Tunavyojua Pinda hajawahi kuwa na uamuzi.
Naye angeomba bosi wake aje kutafuta ufumbuzi.
Kikwete naye hana majibu kwani hata hajui kwanini nchi yake ni maskini.
WATANZANIA NCHI YETU TANZANIA HAINA TOFAUTI NA SOMALIA. HATUNA UONGOZI WA NCHI. SI LAZIMA TURUSHIANE RISASI NDO TUJUE TUMEFIKA PABAYA.
It is high time to topple the filthy corrupt and irresponsible regime!!!!!
Period.
 
Sewa-Haji-Ward.jpg
 
Sewa-Haji-Ward.jpg
3940383859_73f48abf02.jpg
DK.JPG


Miaka 50 ya Uhuru Tanganyika hali ndio hiyo wakati Wabunge wanafikiria kujiliwaza na vimwana kule dodoma ambapo vijana wetu wanaosoma vyuo vya Dodoma wakiwa wahanga wa kuwafariji wabunge, papo hapo wabunge kwa ubinafsi mkubwa walio nao kujiongezea posho kwa kiwango cha kutisha na kusikitisha na kuacha hali hii ya wagonjwa wakiteseka na wauguzi kukosa hata pesa stahiki ya kujikimu.

Matokeo ya wabunge kujiongezea posho ni kuendelea kutanua wakiwa Dodoma usiku kucha na wanapoingia bungeni ni kutia sahihi kwenye vitabu vya mahudhuria kisha kuanza kuchapa usingizi na kusubiria kupata malaki ya pesa jioni wanaporudi kwenye starehe zao.
 
3940383859_73f48abf02.jpg


Hata vyandarua hakuna maana yake licha ya matatizo yaliyowapeleka hospitalini watakumbwa na ugonjwa wa kuambukizwa malaria kutokana kukosa kinga ya mbu.
 
Hawa madaktari wana haki ya kudai malipo bora lakini jambo ambalo limekuwa linanipa shida kuelewa ni matumizi ya neno 'bingwa'. Kama wao ni madaktari bingwa kwa nini wagonjwa (kiongozi mgonjwa ni mgonjwa tu) wanapelekwa India? Ubingwa wao ni kwenye nini hasa? Tanzania tumezidi tamaa ya kutaka vyeo vya mng'aro. Daktari bingwa?

Bingwa ni kinywaji kikali sana
 
3940383859_73f48abf02.jpg


Hata vyandarua hakuna maana yake licha ya matatizo yaliyowapeleka hospitalini watakumbwa na ugonjwa wa kuambukizwa malaria kutokana kukosa kinga ya mbu.
Hali kama hiyo na kitanda kama hicho chenye wagonjwa wawiliwawili chandarua itakaaje?
Na hii inaonekana ni wodi ya watoto, wazazi wa watoto hawa wanalalaje hapa?
Si tu malaria ya kuogopa, si watapewa mseto!!! wanaweza ambukizana magonjwa hatari kabisa ambayo dawa zake bado hazijatoka kwenye labs.
 
NAIBU WAZIRI: NIMEWASIKIA
“Nimewasikia ndugu zangu wafanyakazi, kuna baadhi ya mambo itabidi niyapeleke kwa wakubwa zangu na mengine nitayajibu hapa,” alisema Dk. Nkya.


Hapo ndipo kwenye Tatizo kubwa..... Nchi hii Hakuna mwenye maamuzi

Naibu Waziri anamsubiri Waziri , Waziri anamsubiri Waziri Mkuu .... Wote wanalalika

Waziri Mkuu atsubiri JK atoke alikoenda kizurula Naye JK atalalamika na akiziidiwa Ataunda tume....

Tume itatafuna mamilioni na kuleta mapendekezo .,, nayo itaichia serikali kutekeleza na huo itakuwa ndio mwishoni....biashara imeisha.... Du
 
NAIBU WAZIRI: NIMEWASIKIA
"Nimewasikia ndugu zangu wafanyakazi, kuna baadhi ya mambo itabidi niyapeleke kwa wakubwa zangu na mengine nitayajibu hapa," alisema Dk. Nkya.


Hapo ndipo kwenye Tatizo kubwa..... Nchi hii Hakuna mwenye maamuzi

Naibu Waziri anamsubiri Waziri , Waziri anamsubiri Waziri Mkuu .... Wote wanalalika

Waziri Mkuu atsubiri JK atoke alikoenda kizurula Naye JK atalalamika na akiziidiwa Ataunda tume....

Tume itatafuna mamilioni na kuleta mapendekezo .,, nayo itaichia serikali kutekeleza na huo itakuwa ndio mwishoni....biashara imeisha.... Du
Vicious_Cycle_Logo.jpg
 
Back
Top Bottom