Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Wadau naombeni msaada wenu,
Mwanangu wa miaka 8 (yuko darasa la 3) anataka kunipa kichaa. Nimejaribu sana kumsaidia aweze kufanya vizuri kwenye masomo yote na amejitahidi ila siyo hisabati.
Nimekuwa nikimfundisha lakini naona siku zinavyoenda ninakuwa kama natangaza uadui naye au vita. Anaonekana kukata tamaa na hisabati hadi napata wasi wasi.
Hata ukimwomba kuona madaftari yake, wakati mwingine anaficha daftari la hisabati (na kudai kuwa liko kwa mwalimu) au analiweka chini kabisa ya madaftari mengine. Nadhani angependa nisilione kamwe.
Kwenye mitahani anafanya vizuri masomo yote isipokuwa hisabati. Anaweza kupata A kidogo, B+ na B lakini hesabu ni kuanzia 40-50%. Mbaya zaidi hata ukimfundisha kitu akaelewa na kufanya mazoezi vizuri, kesho yake hakumbuki zaidi ya nusu ya vitu. Ndugu zangu nifanyeje?
Nasikitika sana kwani sikuwahi kuona kama hisabati ni somo la kusumbua kiasi hicho na hasa hasa katika hatua za awali. Lakini kubwa kabisa ni kwamba ninsingependa kumwona mwanangu anakata tamaa na somo lolote mapema namna hii.
Naombeni maoni au ushauri.
Mwanangu wa miaka 8 (yuko darasa la 3) anataka kunipa kichaa. Nimejaribu sana kumsaidia aweze kufanya vizuri kwenye masomo yote na amejitahidi ila siyo hisabati.
Nimekuwa nikimfundisha lakini naona siku zinavyoenda ninakuwa kama natangaza uadui naye au vita. Anaonekana kukata tamaa na hisabati hadi napata wasi wasi.
Hata ukimwomba kuona madaftari yake, wakati mwingine anaficha daftari la hisabati (na kudai kuwa liko kwa mwalimu) au analiweka chini kabisa ya madaftari mengine. Nadhani angependa nisilione kamwe.
Kwenye mitahani anafanya vizuri masomo yote isipokuwa hisabati. Anaweza kupata A kidogo, B+ na B lakini hesabu ni kuanzia 40-50%. Mbaya zaidi hata ukimfundisha kitu akaelewa na kufanya mazoezi vizuri, kesho yake hakumbuki zaidi ya nusu ya vitu. Ndugu zangu nifanyeje?
Nasikitika sana kwani sikuwahi kuona kama hisabati ni somo la kusumbua kiasi hicho na hasa hasa katika hatua za awali. Lakini kubwa kabisa ni kwamba ninsingependa kumwona mwanangu anakata tamaa na somo lolote mapema namna hii.
Naombeni maoni au ushauri.