Mtoto wangu wa miaka 8 anaogopa somo la hisabati kama ukoma!

Mkuu hapo kwenye Red, mama yake na wewe wote ni wazazi tu, kama wewe ulishindwa kama mzazi basi hata mama kama sio mwalimu wa primary hataweza, labda kama angekuwa mwalimu. Mimi mwenyewe mama na siwezi kufundisha wanangu, huwa tunaishiana kufinyana na kumwambia akalale hata kama katoka kuamka. maana sometimes nahisi kama hataki kusoma ili akacheze, kwa hiyo adhabu huwa kama hutaki kusoma basi na kucheza hakuna. kwa kweli inaumiza sana mtoto asipofanya vizuri, na hasa kama unaamini angeweza kufanya vizuri akiongeza juhudi.

Nimekupata mama. Binafsi naamini anaweza kufanya vizuri zaidi ya hapo. Yaani hajaweka nguvu zote hadi ile chembe ya kwenye mkia ili tubwage manyanga. Ushauri wako tutaufanyia kazi.

hii inategemea ww baba ulikuwaje enzi hizo kwenye Hisabati!
Kama ulikuwa unakuna kona vipindi vya hesabu basi umemwambukiza hata mke wako nae jaribu kuulizia kama alikuwa fit kwenye hisabati labda kachukua kipaji cha mama yake.

Naogopa kuingia kwenye mitego ya kujimwagia misifa hapa jamvini. Labda niseme tu kuwa wote (mimi na mama yake) tunaweza kwa kiwango cha kawaidia kufanya hesabu especially zile za primary

Mwambie "troublesome, crack headed halfcast from Harare" will come get him if he doesn't do his homework...lol!!

Hapo si ndo tutamharibu kabisa?

kabla sijatoa ushauri wangu niambie mwanao anajua kuhesabu hadi ngapi?

nikutahadharishe kuwa watoto ni saikolojia tupu......... hata unapoongea naye kuna vitu huwa anakuambia unashindwa kusikia kwa sababu ya kushindwa kumsoma saikolojia yake...........

naanza kwa kukupa kitu kimoja unachoweza kuona cha kipuuzi lakini kizingatie, halafu ukinielewa, uende kumwelekeza na mwanao, kama umeanza kumkaririsha tebo tafadhari sitisha kwanza hadi tutakapokuwa tumeelewana namna ya kumuelekeza kujifunza hesabu..........

step 1:
nakushauru usome avatar ya fixed points, halafu ujaribu kufumba macho na ujaribu kuweka namba mbalimbali kufuatana na mtiririko wa kuhesabu kwenye mistari ya mchoro wa ile avata bila kuitazama............. kisha fungua macho uone jinsi ulivyoweka namba zako na umbile linalojitokeza ukiziunganisha hizo namba kwa mstari............. hesabu idadi ya pembe/kona zinazotokea, angalia kama umbo liko katika sura inayoeleweka ama la.......... usijaribu kulazimisha umbo lako lifanane na lile la avatar ya fixed point na wala usisahihishe ukigundua halifanani na wala usichungulie avatar wakati ukiandika namba zako hadi umemaliza kuziandka......... na ukimaliza, kazi a avatar inakuwa imekwisha............. tuanaingia hatua nyingine...........

ukimaliza hilo zoezi, kabla hujaongea na mtoto niPM nitakupa hatua inayofuata yaani step 2..............

Mkuu hiyo homework imenishinda. Kichwa kime-jam. Kama una ushauri mwaga tu. Tutakushukuru mkuu.
 
Kwa umri wake wa miaka8 bado ni mapema kufikiri analiogopa somo la hisabati. Unawezaje kumfundisha au nawe ni mwalimu? je unatumia muda gani kumfundisha? mimi wangua ana 6yrs yuko std 2, niliwah kujaribu kumfundisha hesabu nikakuta ndio kwanza anazidi kufeli maana mi nilitmia njia hii na mwalimu ile so tukawa tunamchanganya tu nikaamua kuwaachia walimu wafanye kazi yao sasa anapanda kutoka 60 mpaka 80 hata 95. nafikiri ujaribu kumwacha afundishwe na walimu wake akija na swali limemshinda katika homework yake muulize shule kafundishwaje fanya nae kwa kufuata njia aliyofundishwa shule.

By the way mi nilisoma shule za kawaida nieanza kujua hesabu secondary kabla ya hapo nilikua nachukulia kama somo la wale wanaofaulu wanajua wao wamefanyeje!
 
hesabu ni somo gumu kulielewa kwa mtoto kwa sababu halina maandishi ................lina namba tu

nafikiri ungeweza kumfundisha theory behind hizo hesabu ingemsaidia mtoto ......

unaweza kuchukua lessons kwenye internet (zipo nzuri with colourful picts and animations) ambazo mtoto anaweza kufahamu kwa urahisi zaidi.

mfano unapomfundisha mtoto Volume of a cylinder ( his mug for tea as an example) ..........hakikisha unamfundisha kwa nini ikawa hivyo visualy. (labda utengeneze cylinder la karatasi then unalifungua na kugeuka rectangle and ................)

am sure he will enjoy

all the best
 
hesabu ni somo gumu kulielewa kwa mtoto kwa sababu halina maandishi ................lina namba tu

nafikiri ungeweza kumfundisha theory behind hizo hesabu ingemsaidia mtoto ......

unaweza kuchukua lessons kwenye internet (zipo nzuri with colourful picts and animations) ambazo mtoto anaweza kufahamu kwa urahisi zaidi.

mfano unapomfundisha mtoto Volume of a cylinder ( his mug for tea as an example) ..........hakikisha unamfundisha kwa nini ikawa hivyo visualy. (labda utengeneze cylinder la karatasi then unalifungua na kugeuka rectangle and ................)

am sure he will enjoy

all the best

Ahsante mkuu. Naomba msaada, utubandikie hiyo link. Ningefurahi kurudia hiyo shule kwani sasa inakuwa practical zaidi.
 
hiyo link kwa kweli kukutafutia nitashindwa kwa sasa ......besides inategemea na mwanao sasa anasoma topic gani....
 
Kwa umri wake wa miaka8 bado ni mapema kufikiri analiogopa somo la hisabati. Unawezaje kumfundisha au nawe ni mwalimu? je unatumia muda gani kumfundisha? mimi wangua ana 6yrs yuko std 2, niliwah kujaribu kumfundisha hesabu nikakuta ndio kwanza anazidi kufeli maana mi nilitmia njia hii na mwalimu ile so tukawa tunamchanganya tu nikaamua kuwaachia walimu wafanye kazi yao sasa anapanda kutoka 60 mpaka 80 hata 95. nafikiri ujaribu kumwacha afundishwe na walimu wake akija na swali limemshinda katika homework yake muulize shule kafundishwaje fanya nae kwa kufuata njia aliyofundishwa shule.

By the way mi nilisoma shule za kawaida nieanza kujua hesabu secondary kabla ya hapo nilikua nachukulia kama somo la wale wanaofaulu wanajua wao wamefanyeje!


pia nadhani angeongea na walimu wa mtoto ili wampe ushirikiano wa karibu akiwa shuleni
 
hiyo link kwa kweli kukutafutia nitashindwa kwa sasa ......besides inategemea na mwanao sasa anasoma topic gani....


Poa mkuu. Mimi nilidhani unaijua hiyo link na kwa hiyo ungenisaidia kuokoa muda wa kuanza kuitafuta. Hata hivyo nitajaribu.

Kuhusu topic nimesema toka mwanzo kwamba yuko darasa la tatu na tatizo ni hesabu zote kwa ujumla. Topic ambazo naona amepata shida zaidi ni kuzidisha (namba mbili hadi tatu kwa namba mbili, mfano 562 x 18 au 78 x60), kugawanya na nyingine pia.
 
pia nadhani angeongea na walimu wa mtoto ili wampe ushirikiano wa karibu akiwa shuleni

Tutajaribu kuongea na mwalimu wake wa shuleni. Tatizo kubwa ni kuwa shule hairuhusu tuition na pia mimi binafsi sipend tuition hata kidogo. Tutajaribu kuona kama mwalimu wake anaweza kutupatia ushirikiano ili mtoto apate attention zaidi ikiwa ni pamoja na kumfuatilia kwa karibu. Sipendi kumtafutia mwalimu mwingine kwani naogopa kumchanganya zaidi.
 
Dark City,

Watoto (watu) wapo tofauti na namna ya kufundisha inatakiwa kuwa balanced ili watoto wa makundi yote waweze kuelewa kinachofundishwa. Kuna wengine wanaelewa zaidi lugha ya picha/vitendo, wengine maneno/maandishi/namba pekee inatosha. Jaribu kufuatilia namna anavyofundishwa hesabu shuleni na linaganisha na wewe unavyomfundisha. Kuna uwezekano mkubwa jinsi anavyofundishwa shuleni ndo na wewe unafanya hivyohivyo hivyo mtoto haelewi anachofundishwa.

Hatua ya kwanza jaribu kung'amua mtoto wako yupoje (hasa katika hayo makundi mawili). Kisha msaada wako uulekeze zaidi kwa kuzingatia kundi lake.
 
Poa mkuu. Mimi nilidhani unaijua hiyo link na kwa hiyo ungenisaidia kuokoa muda wa kuanza kuitafuta. Hata hivyo nitajaribu.

Kuhusu topic nimesema toka mwanzo kwamba yuko darasa la tatu na tatizo ni hesabu zote kwa ujumla. Topic ambazo naona amepata shida zaidi ni kuzidisha (namba mbili hadi tatu kwa namba mbili, mfano 562 x 18 au 78 x60), kugawanya na nyingine pia.

Firstlady1 one hesabu zilinishinda ndo maana sasa nafundisha la kwanza mpaka la nne na vipindi vya watoto tu sitaki kuumiza kichwa changu mie
 
Firstlady1 one hesabu zilinishinda ndo maana sasa nafundisha la kwanza mpaka la nne na vipindi vya watoto tu sitaki kuumiza kichwa changu mie


Pole sana dada. Si ajabu uliangukia katika mikono mibaya na hukuwa na mtu wa kukusaidia. Kuna watu wengi ambao walishindwa hisabati kwa sababu ya kufundishwa vibaya.

Kuna kijana wangu ambaye nilimtoa kijijini baada ya kumaliza darasa la saba. Alipoanza form 1, ikagundulika kuwa hawezi kabisa kumudu masoma kwani uwezo wake ulikuwa sawa na mtoto wa darasa la nne. Niliomba washikaji zangu (walimu) wakampiga msasa (crush program) hadi akaweza kufikia kiwango cha darasa la 7 ndani ya miezi kama 8. Alisoma sekondari na kumaliza kidato cha nne akiwa na B ya hisabati. Kwa sasa yuko chuoni. Kwa hiyo mimi naamini kwamba mwalimu anao mchango mkubwa sana katika kufeli au kufaulu somo lolote.
 
hesabu bana hata mimi ilikiuwa mama mke yaani we acha

nilikuwa nagonga hizo hizo40-50, nikijitahid sana 65.
nilipoenda form one (seminary) ilikuwa hakuna ubishi lazima usome na kufauli hesabu vinginevyo unatimuliwa.ilinibidi kuweka mkazo sana na hesabu na nilijikuta naipenda tu.mpaka leo niko fiti na chuo nimesomea fani ya telecom
tatizo la mwanao nahisi haya

wewe mwenyewe hujui mbinu za kumfundisha(lugha ya ukali)
mwalimu wake ni mkali sana na anachpa bakora
unamrundikia vitu kibao kwa wakati mmoja( anza taratibu kana ni hesabu za kutoa ni za kutoa tu kuwa siku na unaacha maswali mawili mpka matano)
msome mwanao vizuri kuna kitu anapenda( huwa anapenda kuchora picha picha mda mwingi)
ana vitabu vya ziada na kiada(mnunulie kama hana)
muwekee ratibaya kusoma na kucheza

bado mwanao ana nafasi nzuri ya kupenda hisabati, mjengee mazingira mazuri mkuu
 
Jitahidi mkuu, taratibu tu ataelewa maana naona hatari ya mwanao kuwa kama yule mwalimu wa kwenye tangazo la haki elimu anayefundisha square root.
....Ah!mkuu una maana hata yule naye alianza kuogopa hesabu tangu mwaka 47?? Maana yule teacher anachanganyikiwa kabisa anapoambiwa akafundishe hesabu...
 
Ok. Kwa nini usijaribu kufanya somo la hisabati kuwa kama mchezo fulani kwa kumnunulia vitabu vya hesabu vyenye picha kibao za kupendeza rangi na michezo michezo ya hisabati, math learning software games kwenye dvd/cd-rom, au hata nintendo ds pamoja na math games
 
Ok. Kwa nini usijaribu kufanya somo la hisabati kuwa kama mchezo fulani kwa kumnunulia vitabu vya hesabu vyenye picha kibao za kupendeza rangi na michezo michezo ya hisabati, math learning software games kwenye dvd/cd-rom, au hata nintendo ds pamoja na math games


Ahsante sana mkuu kwa mawazo yako mazuri. Vitabu anavyo vya kutosha. Hata hivyo napata taabu kupata visual teaching aid ambazo zingemsaidia. Mimi niko Tz na nimejaribu maeneo mengi ya Dar na hata Arusha lakini nimeshindwa kupata DVD/VCDs za kufundishia watoto. Kama kuna sehemu unaijua basi nistue.
 
...wewe mwenyewe hujui mbinu za kumfundisha(lugha ya ukali) mwalimu wake ni mkali sana na anachpa bakora unamrundikia vitu kibao kwa wakati mmoja( anza taratibu kana ni hesabu za kutoa ni za kutoa tu kuwa siku na unaacha maswali mawili mpka matano) msome mwanao vizuri kuna kitu anapenda( huwa anapenda kuchora picha picha mda mwingi) ana vitabu vya ziada na kiada(mnunulie kama hana) muwekee ratibaya kusoma na kucheza

Hapo mkuu umenena. Huyu mtoto anapenda sana kuchora na anaweza. Ukimkuta sehemu basi atakuwa anachora. Najitahidi kumpangia ratiba ili afanye masomo yote ila kwa kweli anapenda sana kuchora chora.
 
Mimi nafikiri hukumjenga alipokuwa mdogo sana kama kumnunulia toys na hisabati lkn isikupe homa matajiri wengi duniani hawajui hesabu mpaka calculator. Nakushauri umwekee mwalimu nyumbani kwani kila kitu ni fani na ww huwezi mfundisha utakuwa na qhadhabu wkt mwingine. Good luck
 
Back
Top Bottom