Mtei awashauri viongozi CCJ wahamie CHADEMA

Ukitaka kuunganisha vyama kuna sababu mia za kufanya hivyo na ukitaka kuto unganisha pia zipo mia za kutofanya hivyo. Kinachotakiwa ni common ground ambayo ipo wazi kabisa mengine ni chuki binafsi za waanzilishi!

NIlishauliza nipeni tano ambazo haziwezi kufanywa na chama kimoja..
 
Kama CHADEMA wanataka muungano wa Wapinzani, wakumbatiane kwanza na CUF, NCCR, TLP, DP na wengineo waliowatangulia CCJ.

Lakini kwa upande mwingine, je ni kilio cha kubembeleza mvuto kwa kuwa CHADEMA imeshapoteza mvuto na dira?

Nitafurahi siku ambayo utaonesha kuwa una mawazo yako binasfi na siyo painted mwanakijiji every where!
 
Kwa namna yoyote hatima ya CCJ isihusianishwe na kushiriki au kutoshiriki uchaguzi ujao.

Litakuwa ni kosa kubwa sana kukiua hiki chama kwa ajili tu ya kushiriki uchaguzi ujao, ata kama hakitafanikiwa kushiriki uchaguzi ujao bado kina nafasi ya kujenga upinzani wa maana kuelekea 2015.
Butola you have a point wengi wanaiangalia Ccj kwa mtazamo wa leo si wa kesho wanataka isajiliwe haraka haraka ili ishiriki uchaguzi ina maana ikishindwa uchaguzi mwaka huu wanaiambia Ccj kwaheri, yale yale ya Mrema kuletwa na kuvuma karibu na uchaguzi baada ya hapo wakamwachilia mbali. Tunatakiwa tuipe muda kama miaka miwili au mitatu iende kwa wananchi ijieleze inataka kutufanyia nini na viongozi wao ni akina nani kwa leo tunawajua viongozi wawili tu na tanzania ni kubwa hatutaki sera nzuri za vitabuni za copy and paste Ccj wasituuzie mbuzi kwenye gunia, ni bora kukipigia chama ambacho tumekiona angalau kinajaribu kuliko chama kisicho hata na uongozi unaojulikana.
 
mkiwa wengi wa kufanya nini; mbona CCM wako wengi bungeni EBO!!! WINGI NDIO UBORA?

Wingi siyo ubora, mbona chadema wamefanya mambo makubwa sana bungeni na uchache wao? tatizo ni kwenye kupitisha haya mambo yenye ubora yanaitaji muwe wengi hii ni kanuni. Pia unaona tatizo la kuwa wachache maana mnashindwa hata kuhakiki kazi. Si umeona viongozi wako wameshindwa hata kufanya basics na kumpa tendwa ujiko wa bure, wameshindwa hata kuhakikisha majina yao yako vizuri?
 
Nitafurahi siku ambayo utaonesha kuwa una mawazo yako binasfi na siyo painted mwanakijiji every where!

huku ni kushindwa hoja; ina maana na wewe una mawazo ya Luteni ? unaogopa kukubaliana na mtu mwingine kwa sababu utaonekana una mawazo yake? Maswali yaliyopo ni ya msingi... kwanini Chadema ising'ang'anie kuungana na hivyo vyama vingine? Mtei hakutoa ushauri kwa CUF au TLP anauotoa kwa CCJ ambacho tulishaambiwa hakina mpango?
 
Wingi siyo ubora, mbona chadema wamefanya mambo makubwa sana bungeni na uchache wao? tatizo ni kwenye kupitisha haya mambo yenye ubora yanaitaji muwe wengi hii ni kanuni. Pia unaona tatizo la kuwa wachache maana mnashindwa hata kuhakiki kazi. Si umeona viongozi wako wameshindwa hata kufanya basics na kumpa tendwa ujiko wa bure, wameshindwa hata kuhakikisha majina yao yako vizuri?


mambo yapi hayo? help me out ambayo hayakufanywa na watu wengine nje ya bunge na uchache wao?
 
Mkuu Mwanakijiji Punguza Hasira, navyotambua Hasira si Tabia yako. Mtei ameshauri kama CCJ IKIKOSA usajili wa Kudumu inakaribishwa kwenye chama ambacho yeye yumo kwa maana anaamini malengo ya CCJ yanafanana na malengo ya Chama ambacho yeye yumo ina maana kama CCJ ikipata Usajili wa Kudumu Basi Kila la kheri
 
Luteni.. nyinyi sijui kwanini hamtaki kunisoma.. nimeshauliza huko nyuma mara nyingi.

a. Waungane kiwe nini?
b. Muungano uwe kwa msingi gani?
c. Baada ya kuungana kinakuwa nini?

Tumeimba mara nyingi.. 'wapinzani waungane' sijui "muungano wa upinzani' mara "waungane kuwa na nguvu bungeni" lakini hakuna anayejibu maswali hayo. Wanasema waungane ili "waiangushe CCM" nikiwauliza ili 'kiwe nini' wanasema "i don't care, tunataka CCM ing'oke".. huu siyo muungano.
MMKJ

Ukianza kuchambua sana na kwa nini zikizidi siku zote matokeo yake huwa si mazuri hata humo ndani ya Ccj mtaanza kuulizana kwanini huyu kwa nini Mpendazoe kwanini Kiyabo tuu mwisho watakugeukia na wewe kwanini Mwanakijiji hivi yeye ni nani na mambo kama hayo.
 
Mimi ninaamini kuwa CCJ wameanzisha chama kwa ajili ya madhumuni na malengo yanayofanya kuwepo kwa chama cha siasa. Lengo kuu likiwa ni kukamata madaraka ya nchi, hivyo si vizuri sana kuwafanya CCJ kuwa tawi la chama chochote kingine; waachwe waunde chama chao na kujiimarisha kwa ajili yamadhumni na malengo yao. Walishaviona vyama vingine vilikuwepo na havijakidhi matarajio ya wao na wananchi wa nchi hii hivyo wanataka kuleta mawazo mapya yenye kuleta mabadiliko katika siasa za nchi hii. Ni vizuri tuwaache CCJ wasajili chama chao, na sisi wapiga kura tutachuja maji na taka.
 
NIlishauliza nipeni tano ambazo haziwezi kufanywa na chama kimoja..

Hakuna kitu ambacho hakiwezi kufanywa na chama kimoja mradi tu wakubaliane wenye chama. Ila kuna limitation nyingi kwenye vyama vingi na kubwa zaidi ni kugawana kula
 
Mwanakijiji yaonekana unakielewa vema chama cha CCJ. naomba majibu bya maswali yafuatayo.
1. Kwa nini mwangwi wake wa kuanzishwaa umeleta hofu zaidi kwa CCM?

2. Je vigogo walio nyuma ya CCJ (kama Mpendazoe) wasijitokezee hadharani na kuonyesha kwa dhati dhamira yao ya kuipinga CCM na kuchukua nchi?

3. Taarifa ya Tendwa kuwa uhakiki wa Dar kwa CCJ ni wanachama 13 tuu na hakionekani kuwa makini katika oganaizesheni yake???

4. Ni kweli tabia za watanzania wengi (hasa vigogo walio nyuma ya CCJ) ni wanafiki, waoga na wenye kujijali binafsi zaidi???
 
CCJ wapunguze high expectation na kutambua hii ni Afrika na muda pia ni rasilimali muhimu katika maendeleo. Mawazo ya Mzee Mtei ni mazuri lakini hayawezi kufanya kazi hata yeye mwenyewe ameshindwa kuyatekeleza.

Wanasiasa wapunguze kidogo kujikubali wao na kutambua michango tofauti ya watu wengine, manake tatizo hilo lipo CCM na ushauri wa Mtei pia Chadema lipo na CUF.

Tukumbuke tu kila uchaguzi wa vyama vingi ulileta mpinzani mpya kutoka chama tofauti, Lyatonga na NCCR 1995, Lipumba na CUF 2000 na Chadema 2005 ijapokuwa Lipumba alifuatia. Changamoto kubwa kwa upinzani ni kumentain kwanza kile walichokipata kutoka chaguzi zilizopita ili kwenda mbele zaidi. Kuitoa CCM kwa mdomo na kujaza thread hakutoshi bila mikakati endelevu na vitendo kwa hatua kwa hatua, hizi short cut ni kujichelewesha zaidi.
 
MMKJ

Ukianza kuchambua sana na kwa nini zikizidi siku zote matokeo yake huwa si mazuri hata humo ndani ya Ccj mtaanza kuulizana kwanini huyu kwa nini Mpendazoe kwanini Kiyabo tuu mwisho watakugeukia na wewe kwanini Mwanakijiji hivi yeye ni nani na mambo kama hayo.

utaona kuwa katika maswali yote hapo juu hayahusiani na "nani".. that is where ur wrong. Ukianza kuhamisha maswali kwa watu.. ina maana unaanza kushindwa hoja.
 
Mkuu Mwanakijiji Punguza Hasira, navyotambua Hasira si Tabia yako. Mtei ameshauri kama CCJ IKIKOSA usajili wa Kudumu inakaribishwa kwenye chama ambacho yeye yumo kwa maana anaamini malengo ya CCJ yanafanana na malengo ya Chama ambacho yeye yumo ina maana kama CCJ ikipata Usajili wa Kudumu Basi Kila la kheri

sina hasira at all.. ni upuuzi wa watu wenye kujidhania wanazungumzia na watoto wadogo na kutumia maneno kama "ebo"! Kama mtu hana hoja anyamaze au aitete lakini siyo kuwafanya watu wengine duni au wapuuzi kwa sababu hukubaliani nao.
 
Mwanakijiji leo umechemka! Kwanza hoja hazivutii alafu unaonekana kuwa na hasira wakati si kawaida yako!
Naomba punguza Hasira mheshimiwa, unajua mzee Mtei kushauri CCJ si kosa maana ameona CCJ wana malengo fulani yanafanana na Chadema. Pili anaye sema mbona CHADEMA haitaki kuungana na vyama kama TLP n.k ; kwanza ajiulize TLP msimamo wao ni nini? Nani asiye muona jinsi Mrema alivyokumbatia CCM? Je huyu anaweza kuwa mpinzani wa kweli?. Sasa wandugu tusikurupuke tu kuonge na kuchangia bila kufanya uchambuzi yakinifu! Halafu watu wanao sema kama wapinzani wanataka madaraka waungane..Hebu tujiulize mbona utitiri wa vyama unazidi...Kwa hili chama Makini hakiwezi kukurupuka na kuungana tu bila kuchambua! kwanza kuna vyama mluki vinaanzishwa kuua upinzani!
 
Kama CCJ mna uhakika wa Kusimama peke yenu na kupata at least 50% ya viti vya Bunge ambavyo vitawawezesha kurekekisha sheria mbalimbali na hata katiba then hamna sababu ya kufanya any kind of Coalition au Ushirikiano na Chama chochote kile. For that nasema Go CCJ go CCJ

Ila kama Ujio wenu na Mipango yenu ya kuwa peke yenu itasababisha hata kile kidogo kilichokuwepo bungeni kisiwepo tena, namaanisha kama mbinu zenu zitapelekea kwa kippindi cha 2010/15 bunge letu liwe 100% CCM basi kizazi cha wana wa nchi ya Tanzania Hakitakaa kiwasamehe Milele
 
sina hasira at all.. ni upuuzi wa watu wenye kujidhania wanazungumzia na watoto wadogo na kutumia maneno kama "ebo"! Kama mtu hana hoja anyamaze au aitete lakini siyo kuwafanya watu wengine duni au wapuuzi kwa sababu hukubaliani nao.

Du hapa kama nimekukwaza naomba msamaha ili neno "ebo" nimelizoea tu na halina maana yoyote kwangu ni kichombezo tu ingawa najua lina maana. narudia tena samahani!
 
sina hasira at all.. ni upuuzi wa watu wenye kujidhania wanazungumzia na watoto wadogo na kutumia maneno kama "ebo"! Kama mtu hana hoja anyamaze au aitete lakini siyo kuwafanya watu wengine duni au wapuuzi kwa sababu hukubaliani nao.

Du hapa kama nimekukwaza naomba msamaha ili neno "ebo" nimelizoea tu na halina maana yoyote kwangu ni kichombezo tu ingawa najua lina maana. narudia tena samahani!
 
Back
Top Bottom