Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
MWANASIASA muasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edwin Mtei, amewataka viongozi wa Chama cha Jamii (CCJ), kuhamia Chadema, ili wawe katika nafasi mzuri ya kuendeleza upinzani wa kweli hasa kama chama hicho hakitapata usajili wa kudumu ndani ya mwaka huu.
Mtei alitoa rai hiyo jana alipokuwa akizungumza na Gazeti la Mwananchi huku kukiwa na habari za msajili wa vyama vya siasa nchini, kuhaidi kuanza kuhakiki wanachama wake wa CCJ jijini Dar es Salaam.
Mtei alisema anawashauri viongozi wa chama hicho kuhamia Chadema ili kuimarisha upinzani wa kweli.
"Mimi nawashauri hao watu wa CCJ waje kwetu Chadema kama watakosa usajili wa kudumu ili kwa pamoja, tuimarishe upinzani wa kweli,"alisema Mtei.
Alisema angependa kuona siku moja viongozi wa chama hicho akiwemo Fred Mpendazoe, wanahamia Chadema, chama chenye watu waliodharimia kuleta mabadiliko ya kweli.
"Waje ili kwa pamoja, tuunganishe nguvu zetu ili twende bungeni tukaimarishe upinzani wa kweli,"alisiisitiza Mtei
Alisema amekuwa akisikitika kuona viongozi wa CCJ wakihaha siku hadi siku kusaka usajili wa kudumu wa chama hicho.
Alisema viongozoi hao wanaweza kuhamia Chadema hasa kwa kuzingatia kuwa sera za vyama hivyo viwili zinafanana.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Mtei alitoa rai hiyo jana alipokuwa akizungumza na Gazeti la Mwananchi huku kukiwa na habari za msajili wa vyama vya siasa nchini, kuhaidi kuanza kuhakiki wanachama wake wa CCJ jijini Dar es Salaam.
Mtei alisema anawashauri viongozi wa chama hicho kuhamia Chadema ili kuimarisha upinzani wa kweli.
"Mimi nawashauri hao watu wa CCJ waje kwetu Chadema kama watakosa usajili wa kudumu ili kwa pamoja, tuimarishe upinzani wa kweli,"alisema Mtei.
Alisema angependa kuona siku moja viongozi wa chama hicho akiwemo Fred Mpendazoe, wanahamia Chadema, chama chenye watu waliodharimia kuleta mabadiliko ya kweli.
"Waje ili kwa pamoja, tuunganishe nguvu zetu ili twende bungeni tukaimarishe upinzani wa kweli,"alisiisitiza Mtei
Alisema amekuwa akisikitika kuona viongozi wa CCJ wakihaha siku hadi siku kusaka usajili wa kudumu wa chama hicho.
Alisema viongozoi hao wanaweza kuhamia Chadema hasa kwa kuzingatia kuwa sera za vyama hivyo viwili zinafanana.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi