mtanzania1989
JF-Expert Member
- May 20, 2010
- 4,064
- 6,733
Jamii ya Somalia Kenya inaonekana imeteseka na kuonewa na GoK kwa muda mrefu, hii jamii kwa vyovyote baadhi yao watashirikiana na Al Shabab, ni muda muafaka sasa kwa GoK kwenda kuondoa sintofahamu yao na hii jamii, lakini ubaguzi hautapungua Kenya basi wajue tu Al Shabab watapata sympathizers wa kutosha kutoka jamii ya kisomalia.Kwanza nawapa pole sana ndugu zetu wa Kenya kutokana na kitendo cha ukatiri uliyo pitiliza mipaka, tunawaombea walio poteza maisha Mungu alaze roho zao mahali pema peponi - AMEN.
Mkuu, tukija kwenye documentary ya Al Jazeera, hata mimi miaka kama miwili hivi iliyopita niliwahi kuona Documentary nyingine ya Al-Jazeera, ilikuwa inazungumzia kuhusu Wakenya wa Garrisa wenye asili ya Somalia; mtangazaji alikuwa Msomali mzaliwa wa Garrisa ameajiliwa Al Jazeera - mazungumzo niliyo sikia kwenye documentary hiyo yalinishangaza sana - sikuamini masikio yangu!! Kwanza, Msomali huyo alisema alikimbia Kenya miaka mingi iliyopita kutokana na mateso aliyo wahi kupata akiwa mikononi mwa Polisi, jamaa na ndugu zake hawakuwahi kusalimika kutokana na matendo ya ukatili na baadhi yao kuuwawa na Polisi bila sababu za msingi! Aliongezea kwamba, wakati mwingine wanajeshi walikuwa wanavamia nyumba zao usiku wa manane wanavunja milango na kuwafanyia vitendo vya kuwadhalilisha, wakati mwingine Wanajeshi wanafanya summary excution!! Mark you - mtangazaji alisema ukatili huo ulikuwa unafanyika kwa muda mrefu kabla hata ya kikundi cha Al-Shabaab hakija hibuka/hundwa huko Somalia.
Mtangazaji huyo na Camera crew wa Al Jazeera alirudi Garrisa kinyemela, aliwahoji Wasomali wenzake kinacho endelea kwenye Mji wa Garrisa na Vitongoji vyake tangu ahame kwenda Ulaya - wenyeji wenye asili ya Kisomali walilalamika sana kwamba wanasumbuliwa na kudhalilishwa kwa miaka mingi sana, walimwambia mambo mengi sana kutokana na kumuamini Kijana huyo mzaliwa wa Garrisa.
Baada ya kusikiliza Documentary hiyo ambayo ilichukua muda mrefu kidogo ndio nikagundua kwamba Somali Community in Northern Kenya wanajihisi wanabaguliwa sana na Taifa lao la Kenya, binafsi ningeshauri Viongozi wa Kenya wajaribu kukaa chini na watu hawa na kuwahakikishia kwamba hawatafanyiwa vitendo vya kutowajali/kudhalilisha - mkipuuzia ushauri wangu basi Wasomali wa Garrisa na wa sehemu nyingine za Kenya watashawishika kuwapa hifadhi Al-Shaabab - tukajikuta Africa Mashariki tunapata zahama za Africa Magharibi na BOKO ARAM, inaelekea Al Shaabab wameanza kutumia mbinu za BOKO ARAM - tuwe macho.
Labda nimalizie kwa kusema kwamba Viongozi wa Kenya wasijingize sana kwenye masuala ya Somalia, adhabu mlio wapa Al Shaabab inatosha ondoeni majeshi yenu Somalia hakuna atakae wacheka - wahacheni Wasomali wayamalize matatizo yao wenyewe - kama wanataka Taifa lao liwe Islamic Republic- shauri yao mbona Taifa lao limewahi kuishi zaidi ya miaka ishirini bila ya kuwa Serikali, mizigo ya Regime chage wahachie wa Merikani wahangaheki nalo lakini na wao utafika wakati watachoka kukimbizana na Al-Shaabab.