Wafanyakazi mnaogopa hata kugoma au kuandamana hata siku moja mnategemea nini?Kamwe aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Pamoja na sifa na tambo zote walizofanya serikali kuhusu kuongeza mishahara wameishia kuongeza elfu 20,000?
Ikiwa ni muda mchache toka bank ya NMB kunipa notification ya mshahara kuingia na kufanikiwa kuona kilichoongezeka. Nimepigwa butwaa kuona tambo zote zile increment haizidi 20K!
Nadhani Sasa ni muda wa watumishi wa umma kujitambua na kuacha kushoboka na serikali. Serikali ime-inflate gharama za maisha kwa kiwango kikubwa but then haina efforts za kuboresha maslahi.
Maamuzi ya namna hii yanapunguza morali ya kazi na kushusha uadilifu. Tutegemee uzembe makazini na kuongezeka ubadhirifu.
Serikali imeshindwa kusimamia utumishi wa umma hususani kwenye suala la maslahi.