Huyu mzee yupo very committed ktk chama nadhani ndio sifa kubwa alokuwa nayo toka enzi za Nyerere. Ni sifa ambayo inaendana na nafasi zote ailizowahi kushika kwani ana mapenzi na chama kuliko hata familia yake acha mbali Utanzania.
Kwa hiyo yawezekana kuwa ni chaguo zuri sana kwa CCM isipokuwa tu sifahamu kama ataiweza kazi ya Malecela mahala ambapo utengano wa Chukua Chako Mapema umekuwa donga kubwa kichama.
Akifahamu chanzo cha mgawanyiko ndani ya chama kuwa ni Ulaji na sio maslahi ya nchi ama Sera za chama nadhani atakuja gundua kazi yake ni nzito sana kuliko alivyotegemea. Kila kiongozi ndani ya chama CCM wanataka nafasi yao ktk uhujumu uchumi - that is a fact. hakuna anayesikitika kuhusu Uhujumu uchumi ila mgawanyo wa mali ya Taifa na ndio maana kila mtu anagombea NEC. Ukishindwa NEC ndio kushindwa maslahi ya tumbo. Influence inatumika sana kama kigezo cha uchaguzi huu na sio utekelezaji wa mhusika.
Ana kazi nzito sana!
Mkuu ukitulia huwa unamwaga vitu vya nguvu ila basi tu...