Hivi punde tu, PIUS Msekwa amependekezwa na Kamati Kuu ya CCM kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti, CCM. Hii ni kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika ndani ya CCM.
===
HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM), imepitisha jina la aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Pius Msekwa, kurithi mikoba ya John Malecela kwa kumteuwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara.
Pius MsekwaHALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM), imepitisha jina la aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Pius Msekwa, kurithi mikoba ya John Malecela kwa kumteuwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara.
Pius Msekwa ameteuliwa baada ya Malecela kuamua kwa ridhaa yake kustaafu nafasi hiyo ambako katiba ya CCM humpatia nguvu Mwenyekiti wa Chama hicho humpendekeza mtu na kisha jina lake hupelekwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Kamati Kuu kwa ajili ya kupitishwa.
Baada ya Malecela kuamua kuachia nafasi hiyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtunuku heshima ya kuwa mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu na NEC kwa kutambua na kuenzi mchango wake katika chama.
Wengine walioteuliwa na NEC ni pamoja na Hadija Faraja, ambaye amekuwa Katibu wa CCM, kwa upande wa Unguja Kaskazini.
Mbali ya Msekwa kuwa kiongozi wa muda wa TANU na CCM, pia alishirikiana na aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya ASP, marehemu Thabit Kombo wa Zanzibar kuandaa Katiba ya CCM ambayo ilizaliwa mwaka 1977 baada ya TANU na ASP kuungana.
Msekwa ndiye Katibu Mtendaji wa kwanza wa CCM na kisha alikuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mbali ya kuwa Mbunge wa Ukerewe.
===
HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM), imepitisha jina la aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Pius Msekwa, kurithi mikoba ya John Malecela kwa kumteuwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara.
Pius MsekwaHALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM), imepitisha jina la aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Pius Msekwa, kurithi mikoba ya John Malecela kwa kumteuwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara.
Pius Msekwa ameteuliwa baada ya Malecela kuamua kwa ridhaa yake kustaafu nafasi hiyo ambako katiba ya CCM humpatia nguvu Mwenyekiti wa Chama hicho humpendekeza mtu na kisha jina lake hupelekwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na Kamati Kuu kwa ajili ya kupitishwa.
Baada ya Malecela kuamua kuachia nafasi hiyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtunuku heshima ya kuwa mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu na NEC kwa kutambua na kuenzi mchango wake katika chama.
Wengine walioteuliwa na NEC ni pamoja na Hadija Faraja, ambaye amekuwa Katibu wa CCM, kwa upande wa Unguja Kaskazini.
Mbali ya Msekwa kuwa kiongozi wa muda wa TANU na CCM, pia alishirikiana na aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya ASP, marehemu Thabit Kombo wa Zanzibar kuandaa Katiba ya CCM ambayo ilizaliwa mwaka 1977 baada ya TANU na ASP kuungana.
Msekwa ndiye Katibu Mtendaji wa kwanza wa CCM na kisha alikuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mbali ya kuwa Mbunge wa Ukerewe.