MORE PRESSURE: CDM Wasiposhinda Arumeru East Uongozi mzima wa Taifa LAZIMA Ujiuzulu

Mzee Mwanakijiji nimependa uchambuzi wako lakini ujue kwamba CDM bado ni taasisi inayotegemea nguvu za watu bado haijawa na rasilimali zake za kukifanya kijiendeshe chenyewe.

Kumbuka kuwa hata ruzuku wanayoipata haitoshi kuendesha chama nchi nzima hivyo ukisema uongozi ujiuzulu kwa kushindwa uchaguzi mdogo huoni kama utakuwa unabariki kufa kwa chama sababu ya kushindwa katika uchaguzi mdogo? Nakumbuka humu ndani kuna mtu alishawahi kusema watu wanarundikiwa vyeo wakati ni wabunge badala ya kuwaajili vijana ambao wako katika chama na hawana kazi za kufanya, wakatokea viongozi wa CDM wakatoa ufafanuzi na kutuambia uongozi ndani ya CDM ni wa kujitolea na chama hakina vyanzo vya fedha zinazoweza kuajili watu na kuwalipa mishahara.

Mfano unasema wakishajiuzulu ufanyike uchaguzi na atakayeta kugombea kama ni mbunge aachie ubunge wake ndiyo apewe uongozi, hapo MM unakutaka kuwaonea bure kwani huo ubunge kuupata mbele ya CCM sio kazi rahisi sasa leo aache ubunge ili atumikie chama wakati wameshasema hawana vyanzo vya kupata pesa.

Kuna mengi umeshauri lakini ushauri wako umewahi sio wa 2012 ni labda wa 2017 maana bado wako katika kukijenga chama na tusiwapuuze kuna kila jitihada wanazifanya ikiwemo kuwa tayari hata kugharimu maisha yao kwa ajili ya kukitetea chama.

Kwa ushauri wa kuwafikia wnanchi wa mikoa ambayo bado haina mwako hilo naliunga mkono kwani mikoa kama Lindi, Mtwara, Tanga mingine ambayo mwako ni mdogo inabidi wawekeze nguvu zaidi.

Zaidi inabidi tuendelee kuwaunga mkono hawa jamaa kwani wanajitahidi sana sana kupenya katika mishipa iliyobana katika jitu linaloitwa CCM
 
MM, mbona na wewe umeanza kutoa maoni yako na NEC ikiwa ile ile? kwa hivyo hakuna kilichobadika. Kutokwenda kwenye uchaguzi kutamgharimu nani kati ya chama (CDM) na mwananchi? Hapo naona kama huna hoja vile.

Utaona kuwa sijali sana NEC wanafanya nini ndio maana sijaandika lolote kuhusu wao; ninajua vizuri wao ni nani na wanafanyaje kazi. I care less what they do.
 
Thread inapokwa ya hisia binafsi za mtu na si mtazamo wa wapiga kura wenyewe inakuwa haina maana tena. Hivi unategemea MBOWE, SLAA wa-step down kisa eti Wwameshindwa Arumeru Mashariki? watamwambia nini Mzee mtei eti mkwe wake kakosa nini mpaka awajibishwe? Tume ya Uchaguzi pateni somo kutokana na thread hii, ni mbinu gani CDM wanashauriwa kuzitumia ili kujipatia ushindi huko Arumeru Mashariki? wale wasiyo na shahada za kutopigia kura wahakikishe wanakua nazo, wazitoe wapi?

Hivi unajuwa kweli ulichokiandika hapa au na wewe unataka uonekane ni miongoni mwa political analyst? Tendwa ndiye msajili wa vyama vya siasa na CHADEMA ni miongoni mwa chama kilicho chini ya ofisi yake, sasa Kilaza kama wewe unakuja kujaza page nzima kuongea nonsence topic? hapa ndipo huwa napinga watu wanaposema binadamu wote ni sawa!......mimi nakataa siwezi kuwa sawa na mtu mwenye akili zenye matege kama hizi.
 
Off course huwezi kufanya analysis ukiwa unakula Burruto la Chipotle ndani ya Obamaland halafu unataka uzungumzie current affairs za Arumeru,......hapa mkuu MMM amepotoka, nilidhani angekuwa mjanja angejiuliza ni kwa nini Meneja kampeni wa CHADEMA ni mchungaji Natse na ni kwa nini kule hakuna kelele za Bakwata bali chokochoko za Washiri? hizi siasa za kwenye Mtandao hazipo Applicable katika kila nchi, huwezi kujuwa hali halisi ya Arumeru kwa online politics bali lazima uwepo kwenye Battle ground.

Labda unaunderstimate uwezo wangu wa kujua kinachoendelea "on the ground". I probably know more kuliko unavyofikiria believe me I do wakati mwingine zaidi sana ya wale wanaozunguka on the ground na kujipa ujiko wa kuwa wako on the ground wakifikiria wao ndio Watanzania zaidi wenye haki zaidi ya kuzungumzia mambo ya Tanzania.
 
Hakika umeyaangalia mambo kwa mapana sana na kama Wakuu wa CDM watapata kuipitia lipo jambo la kujifunza kwao lenye mlengo ulio chanya kwao! Yafaa yazingatiwe yale uliyopata kuyazungumzia kwa namna ya pekee kabisa kwa ukuaji zaidi wa chama husika! Bravo Kaka!
 
Well said big Man, but still hopping the chance is ours although is true that we need more zeal to reach this nice dream!
 
Labda unaunderstimate uwezo wangu wa kujua kinachoendelea "on the ground". I probably know more kuliko unavyofikiria believe me I do wakati mwingine zaidi sana ya wale wanaozunguka on the ground na kujipa ujiko wa kuwa wako on the ground wakifikiria wao ndio Watanzania zaidi wenye haki zaidi ya kuzungumzia mambo ya Tanzania.
Mkuu sijaku underestimate na sintofanya hivyo kamwe kwa sababu nafahamu mchango wako kwa Taifa hili, na nikiri kuna baadhi ya Taarifa huwa nazipata kutoka kwako kupitia source zako mbalimbali kabla hata waliopo Nyumbani hawajazipata taarifa hizo.
Kuhusu haki ya kuzungumzia mambo ya nyumbani hiyo ni haki yako ya kuzaliwa & no body can take it away,.....kuhusu hawa waliopo kwenye Battle ground si wote kwamba ni wapiganaji bali wapo kiposho zaidi, unaweza ukakijenga chama zaidi online au kupitia vijarida na makala mbalimbali kuliko hawa wapinaji uchwara ambao wakikosa pesa kwenye chama basi hapa thread za ufisadi CHADEMA hazikauki.
Nakuamini sana mkuu wangu na wewe ni sehemu muhimu sana ya JF.
 

Watanzania tuendelee kuwaunga mkono watanzania ambao sasa wazinduka na kugundua kuwa CHADEMA si chama cha SIASA bali kikundi ambacho kinalalama siku zote kwa kutaka tu damu ya watanzania utadhani ni majni.


Ndugu yangu unatoa povu bure lakini hoja yako haina mantiki kabisa. "Watanzania tuendelee kuwawaunga mkono watanzania...". Hapo nani ni nani? Ni Mtanzania yupi anaye... Mtanzania?

Kimsingi CDM ni chama kilichosajiliwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania kwa maslahi ya Watanzania. Watanzania wanakiunga mkono na ndiyo maana kina viongozi wengi toka CDM wanaowaongoza Watanzania wenzao. kama ni kikundi kinachotaka kumwaga damu ya Watanzania basi hawana tofauti na majambazi. Kwa hilo la kumwaga damu nakushauri kwamba upeleke suala hilo polisi na kwa kuwa tunaiamini serikali basi nadhani utapata msaada. Kinyume na hapo umekuja humu jamvini kwa kukariri ulichoelezwa bila kujua unachokisema
 
Hakika Mwanakiji hapo umenena maneno manono sana kwani wakati fulani kuna mambo yanayoonekana dhahiri lakini hayafanyiwi kazi kiasi kwamba hapo baadaye yatatengenezwa kama visingizio vya kushindwa kwa CDM.Hakika nimeupenda uchambuzi wako nadhani hawataamini mpaka waone hayo unayosema.Maneno matamu na makali kwa serikali hayasaidii zaidi ya ushindi.Wafanye uhakikisho wa watu wao wanakwenda kupiga kura.Mkuu umeongea vema ingawa wakati fulani watu wengi hawapendi ukweli."SIRI WANASEMA BAYANA WANAFICHA"
 
Mwanakijiji hoja yako ni nzuri sana, na umeijenga vizuri sana na yenye nia njema kwa mustakabali wa Chadema; lakini nina maswali matatu/manne:

Changamoto kubwa ya Chadema pamoja na kuwa na ruzuku ya zaidi ya mil 200 bado ni rasilimali fedha. Fedha tulizo nazo zimekwisha gawanywa ktk maeneo mbali mbali ya kibajeti. Wabunge wote ambao wana nafasi za uongozi hawapewi mishahara wala posho.Zaidi sana wanapaswa kuchangia Chama pale inakuwa na hitaji la ghafla lisolokuwa budgeted kama chaguzi ndogo.

Mantiki ya kuwapa wabunge nafasi nyingi za uongozi kwa Chadema ambayo haiwezi kupata upendeleo Serikalini kama ccm ni kupunguza matumizi kwa kuwa na viongozi wote wasiolipwa mshahara pale inapowezekana. Pale inaposhindikana tunafanya hivyo kama ilivyo kwa Dr Slaa na waajiri wengine wengi wa makao makuu.

Je, Leo tukiamua kuwa na M/kiti, makamu 2, manaibu katibu wakuu 2, mwenezi, nk ambao si wabunge tukaamua kuwalipa, tutawalipa sh ngapi? Je, hiyo fedha tunazo? Ikumbukwe kuwa kiongozi wa Chadema wa ngazi ya Taifa Lazima awe msomi atakayelazimika kulipwa fidha za kutosha.

Pili, Hoja ya kushinikiza wajiuzulu kwa kuwa wameshindwa chaguzi ndogo nyingi nayo ina maswali;

Hivi, kama tuna uhakika kuwa Chaguzi hizo zilizopita ambazo walishindwa, walishindwa kutokana na rafu za ccm, Je suala ni kuwataka wajiuzulu au ni kuwashauri wasusie chaguzi zingine zinazofuata hadi tuwe na tume huru ya Uchaguzi? Kwa ushauri wangu, siyo kwamba nawatetea maana hata mimi napenda ushindi, ila nadhani tujikite zaidi kama Chadema kwenye nini kifanyike? Pengine turudi nyuma kwenye drawing board ya Chaguzi ndogo na kuu ili tuje na suluhisho endelevu badala ya more pressure ya kutaka wajiuzulu kwa ushauri wangu.

Tatu, Hiki Chama kimeanza kuongozwa na hao viongozi uliowataja ktk kipindi cha chini ya miaka 10 iliyopita. Tukilinganisha mafanikio yao na vyama vingine ktk mazingira haya magumu ya ukandamizaji wa dola Tanzania Chadema imefanikiwa sana. Je ni haki kusema kwamba wameshindwa? Chini ya Uongozi wa viongozi wote wote wa kitaifa uliowataja (Mbowe, Said, Mohamedi, Slaa, Zitto, Mnyika, nk). Ndo Chama kilichoiondoa CUF Kutoka kuwa Chama kikuu cha upinzani, ndo ktk kipindi hiki idadi ya wabunge, madiwani na kura imeongezeka kwa kasi ya kutisha kuliko vyama vyote vya siasa. Ndo kwa mara ya kwanza inakuwa Chama cha pili uzini zanzibar. Je, haya siyo mafanikio ya kuwataka viongozi wote hao waendelee na Uongozi badala ya kuwataka wajiuzulu? Narudia ni haki kuwaambia wajiuzulu. Inawezekana wewe hujaridhika na mafanikio yao lakini je, hao wengine ambao watajaza nafasi hizo una uhakika kuwa watafanya vizuri kuliko hawa waliopo? Je, kama jibu ni ndiyo, mbona hawajaonesha uwezo huo ktk majimbo na mikoa wanayoyaongoza? Maana nafasi za kuonesha uwezo ziko nyingi, siyo ktk ngazi za taifa peke yake.

Nne, japokuwa tunajitahidi kujenga Chama kama taasisi bado kuna uwezekano mkubwa sana kwamba wanachama wengi wanajiunga na Chadema kutokana na mvuto binafis wa viongozi hao kwa sasa. Sisemi kwamba ni jambo zuri watu kumfuata mtu badala ya taasisi husika, wala sisemi kwamba hicho ndiocho ambaocho kinaendekezwa na Chadema. Hapana. Hivyo ndivyo hali halisi ilivyo, japokuwa sivyo inavyotakiwa kuwa, get me right. Swali ni je, tukiwaondoa hawa ktk nafasi zao ambayo ndiyo jukwaa lao la kuwasiliana na wananchi, haitaathiri Chadema. Wengi wao ni wabunge hivyo watatumia Bunge, lakini watatu kati yao katibu mkuu, makamu m/kiti Zanzibar na naibu katibu mkuu Zanzibar hawatakuwa na Jukwaa lingine. Je si ndo watakuwa hawasikiki kabisa kutokana na kukosa jukwaa na hivyo kurudisha nyuma ukuaji wa Chama?

Mwanakijiji naomba mwongozo wako ktk maswali haya manne.
 
Mtaji wa benki ni CASH.
Mtaji wa mkulima ni MBEGU.
Mtaji wa mwenye bar ni MAKRETI YALIYOJAA BIA.
Mtaji wa shushaina ni KOPO LA KIWI.
MTAJI WA MWANASIASA NI WATU.......YOU LOSE THE SUPPORT OF THE MASSES YOU LOSE POWER.....period!
By the way MMJ ushawahi kujiuliza huko Korogwe kwa nini Maji Marefu (P4) alimshinda Dr Edmund Mndolwa (Phd,FCCA)?
 
CDM walipata umaarufu kwenye Bunge la Sitta.
Makinda ndiye anaewabania CDM sasa hivi, ukijumlisha na ukosefu wa coalition ya upinzani bungeni.Kama mnadhani hii ndiyo CDM ya 2010 mnajidanganya.
Kuhusu suala la Arumeru kuwa ngome, hapo umekosea, wasome historia yao wameru. It's very complicated, very complicated.
 
Angalizo, kama huna sababu ya msingi ya kureply with quote thread hii ya MMM please usifanye hivyo mnawatesa wenzetu ambao wanatumia simu kwa sababu hii thread ni ndefu.

Leo umeongea kitu cha maana sana. Nadhani umetumia kichwa kufikiri bila shaka?
 
Mkuu Mwanakijiji, naona kijijini bado umeme haujafika, bado giza totoro!
Na naliona giza hilo hawa viongozi wa kitaifa wakijiuzulu, endapo watashindwa Arumeru.
In the meantime wenzenu CCM wamekaa mkao wa kula, refa yule yule, magoli yale yale na wala mpira haujabadilishwa!
CDM watashindaje?
 
CCJ vipi? hawajaingia kutafuta kura?

Wewe kalia ufataani, hauna zaidi na CCM inashinda.
 
CHADEMA HAIWEZI KUSHINDA ARUMERU MASHARIKI!

Mimi ni mwanachama hai wa CDM ninayekubali kukosoa na kukosolewa na kutafuta suluhisho la kudumu. Mimi nipo tofauti sana na wale ambao wanaipenda CDM mpaka hawataki kusikiliza changamoto maana ukileta tu changamoto wewe ni CCM! MZEE M.M mimi nakukubali sana na nakubaliana na analysis yako. Hizi ndizo sababu zangu kwa nini CDM haitashinda Arumeru:

1. ARUMERU KUNA VIJIJI VINGI SANA
Nilishawahi kusema huko nyuma kwamba Ngome ya CDM ni kusini mwa barabara ya Moshi - Arusha ambako kuna mchanganyiko wa makabila. Lakini kwa Kaskazini huko ni CCM tu. CDM haijawahi kujiimarisha vijijini. Na kwa tanzania vijijini ambako hawana umeme, maji na chakula cha kutosha hawajawahi kuona faida ya kuiacha CCM. Je? haya mahaba ya CCM na wakazi wa vijijini (ambao ndio wengi nchini) yanaletwa na nini? Utagundua kumbe vijiji vingi havina wawakilishi.naomba muwaulize washabiki wengi wa CDM kama wanajua ofisi zao za mkoa na wilaya zilipo!

2. VIONGOZI WOTE WA CDM NI WABUNGE
- Mfumo wa kuajiri makatibu wa CCM ni wakuigwa.Mtu akiwa na shida na chama anajua wapi pa kukipata. hata ile dhana ya wao kuwajibika kiutendaji mpaka wanaweza kuhamishwa vituo vya kazi kulingana na uhitaji ina maana katika kujenga chama. Leo viongozi wote wa CDM watagawa vipi majukumu ya chama na jimbo? kwa nini asiwepo mtu anayewajibika kwa shughuli za kilasiku za chama tu?

3. HAKUNA MTANDAO
Hebu fikiria wilaya ya Kondoa (km 160 tu kutoka dodoma!) haina mtandao wa CDM! hebu jiulize kuna vijiji vingapi vikubwa! sasa leo Arumeru kuna vijiji vingapi? CCM wanamtandao hadi wa nyumba kumi lakini CDM hatuna hata wa nyumba 100! CCM wanashinda kwa sababu ufisadi wao wanaueneza mpaka level ya familia wakati sisi wema wetu tuashindwa kuueneza hadi level ya kata!

TUNAWEZA KUSHINDA ARUMERU MASHARIKI LAKINI NI KAMA MUNGU WA MBINGUNI ATARIDHIA TUSHINDE LAKINI KWA SASA MATUMAINI HAKUNA!
 
Kwangu hilo la pili silijali sana kwa sababu tayari liko presumed. Hilo la vijana ni suala la mikakati tu. Kwanini CDM inaenda kushiriki chaguzi abazo inajua ngome yake - vijana - hawana kadi za kupigia kura? Uchaguzi huu unafanyika zaidi ya mwaka mmoja baada ya uchaguzi mkuu kwanini hakukuwa na zoezi la kuandikisha wapiga kura wapya? Well.. "You go to war with the army you got" alisema Rumsfeld.

Hapo kwenye red: Njia mbadala ni nini? Ikiacha kushiriki wafanye nini? Ninachojua ni kuwa uchaguzi ni wa Watanzania na kwa ajili ya Watanzania. Hili swali lilipaswa kuulizwa hivi, "kwanini Watanzania wanaenda kwenye uchaguzi wakati vijana hawana kadi za kura?". Haki ya kupiga kura ni ya Watanzania (vijana kwa maana yetu) na hiyo haki ndiyo wanaonyimwa. Haijalishi kwamba vijana ni ngome ya CDM au la. katika hili hata kama CDM wapige kelele namna gani, lakini katika hili CDM watakuwa wakipambana na serikali ambapo katika muktadha wa mambo ya vyama hawastahili kupambana kwa sababu hawako katika ngazi sawa za utendaji. Hivi MM wewe hili unalionaje?
 
Mkuu, watu wamekubali kwenda kwenye uchaguzi wakijua NEC ni ile ile - basi hiyo inakuwa assumed kwenye equation. Hakuna chochote kilichobadilika kati ya uchaguzi wa Igunda, Uvini na huu wa Arumeru.

Mimi sikubaliani nawe kabisa katika hili. CDM ni lazima iingie kwenye uchaguzi hata kama ilijua kuwa uwezekano wa kushindwa tena vibaya kama Uzizi ni mkubwa. Utakubalina nami kuwa hii ni mbinu ya kujiimarisha na kufahamika zaidi. Ukumbuke ni hawa viongozi wa CDM wanaopigania kubadilishwa kwa katiba na tume ya uchaguzi. Kwangu mimi nitakuwa wa kwanza kuwataka wajiuzulu baada ya uchaguzi 2015, kwanza kama watakubali kuingia kwenye uchaguzi chini ya katiba hii na tume hii ya uchaguzi, hilo halitakubalika.

Mimi natamani sana kuona CDM inashinda Arumeru lakini kuna factors nyingine ambazo lazima tuzitilie maanani, mfumo tuliomo. CCM wana uwezo wa kufanya chochote na chochote. 2010 CDM ilifanikiwa kushinda hayo majimbo machache si kwa sababu nyingine isipokuwa nguvu ya umma ya kuudai ushindi wao kwa nguvu, vinginevyo wasingeambulia kitu. Pia 2010 CCM wasingeweza kuunganisha nguvu zao kwani majimbo ni mengi na kila mtu anapigana kivyake.

No! hapana itakuwa ni mapema mno kuwahukumu viongozi wetu. 2015 CDM isiposhika dola hapo sasa tutawaomba wapumzike ili ziingie fikra mpya.
 
CHADEMA itashinda vipi wakati tunasoma kuwa akaunti ya uchaguzi ni 0, yes zero! fedha imekopeshwa kwa Slaa kujengea nyumba yake Kunduchi! na nyingine inalipiwa posho za Josephine na hausigeli wao kwa ajili ya Junior apate malezi mema, na nyingine zinalipa walinzi wa Kanisa analokwenda Josephine. Aliyepewa fedha za kufanya "study" ya uchaguzi Arumeru alikuwa South Africa ambapo hakuna mawasiliano, huku kampeni zinaendelea! Kwi kwi kwi teh teh teh!

Kuna kuwashinda CCM hapo? hapo kuna mchezo wa kuigiza tu.
 
Back
Top Bottom