Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #261
Nakubaliana na wewe Mwanakijiji lakini tusisahau, kuwa pamoja na kushindwa, kuna mafanikio makubwa Chadema imeweza kuyapata katika hizo chaguzi.
Hili halina mjadala lakini haya mafanikio yanasaidia vipi CDM zaidi ya kuongeza matumaini kuwa siku moja mkono wa mwanadamu utaanguka? Kwa mfano, Nassari akipata 20,000 zaidi ya 17,000 alizopata lakini bado akashindwa na mgombea wa CCM ambaye atapata 24,000 (less 10,000 za alizopata Jeremiah Sumari) tunaweza kusema kuwa CDM imefanikiwa?
BInafsi naamini tuanze kupima mafanikio kwa kuanglaia kushinda uchaguzi kwanza vitu vingine vyovyote ni secondary. I mean kama chama ni maarufu, kina wanachama wengi, na kinapendwa lakini hakishindi uchaguzi kinafaa nini kwenye kuleta mabadiliko? NI kweli kinagusa nyoyo za watu, kinawapa watu matumaini, kinafichua mafisadi lakini hata kwenye majimbo ya mafisadi wenyewe chama hakishindi bado tunaweza kusema ni mafanikio?