Dr Willibrod Slaa
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 675
- 1,523
Kama kweli ni kama unavyoelekea kusema ningependa kusema tu vuta subira usiwe na uwoga. Mimi niliisha kutishiwa kupelekwa mahakamani. Uwoga wetu wakati mwingine haujengi. Nchi hii naona sasa itakombolewa tu na watu serious wanaotafuta ukweli bila itikadi, wasio na uwoga wa kupelekwa mahakamani palipo na ukweli. Kama mtu ni mchafu ni dhahiri utaogopa kupelekwa mahakamani au hata kunyooshewa kidole. Kama kuna hoja inatumiwa kuiua Chadema ni hii ya msiba ni kwa msingi huo nimeona nisikae kimya bila kuingilia wakati ninaona dhahiri nina mchango wa kutoa. Utafiti uliofanyika kuhusu kilichoandikwa kwenye magezeti 8 yakiendelea kuachiwa ni uhai wenyewe wa Chadema unatishiwa. Tukisubiri wakati nyumba imebomoka hatuwatendei haki wanachadema wa kweli wala ukweli wala Taifa. Mara kadhaa nafasi ya Mnyika imeulizwa kwenye JF. Cheo alichomia Mnyika wakati anaandika Barua kwa IGP ni Kaimu Katibu Mkuu hakutumia Naibu Katibu Mkuu. Ni muhimu kuwa makini katika kusoma kabla ya kutoa hoja hizi zinazoweza kuchanganya. Kaimu Katibu Mkuu ni mtu anayeachiwa Ofisi wakati Mhusika Mkuu wa Ofisi yaani (Substantive Officer) yuko nje ya Ofisi kwa muda wa kutosha. Pamoja na hilo Chadema kwa kawaida anakaimu nafasi ya Kaimu Katibu Mkuu Mhe. Victor Kimesera, ambaye kwa wakati huo alikuwa Kiteto kwa shughuli nyingine za Chama. La muhimu ni kuwa Katibu Mkuu katika hatua zote anakuwa Consulted na kwa mambo makubwa na hasa yenye sura ya kisheria anatoa Tamko la aina hiyo mwenyewe. Isitoshe, Chadema inaongozwa 'collegially" kwa kutumia vikao vya Sekretariat. Kwa kawaida, isipokuwa katika dharura ya ajabu kama ipo Sekretariat inakuwa imepitia maamuzi yote ya kichama yanayotolewa chini ya muhuri wa Chama na hivyo kwa jina la chadema. utaratibu huu ukieleweka natumaini tutazungumza lugha moja tunayoelewana wote.Mnyika, naomba ajue hasira zake zaweza kutuulia chama, ni kwa nini ampe adui nafasi? sasa ajiandae mahakamani atapelekwa na huyu jamaa, na sifa ya chama inazidi kuharibika,