Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,897
- 941
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduz (MNEC) na Mfanyabiashara wa Makampuni ya ASAS, Salim Abri Asas amechangia zaidi ya Tsh. milioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa bweni la Wanafunzi wa Chuko Kikuu cha Iringa lenye uwezo wa kuchukua Wanafunzi zaidi ya 40 kama sehemu ya kuunga mkono shughuli za elimu katika Mkoa wa Iringa .
Akisoma risala mbele ya Mgeni rasmi Salim Abri Asas, Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Iringa Asunta Nombo amesema Chuo hicho kinakabiliwa na changamoto ya malazi ikiwemo ukosefu wa mabweni ya kutosha “Chuo kinapokea Wanafunzi wengi na tayari ujenzi wa bweni umeanza na umaliziaji unagharimu zaidi ya Tsh. milioni 35 na bweni likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua Wanafunzi wengi”
Akiongea wakati wa sherehe hizo za ukaribisho wa Wanafunzi wapya waliojiunga na Chuo hicho katika kozi mbalimbali, Asas amesema Serikali kwa upande wake inafanya kazi kubwa katika Sekta ya Elimu jambo ambalo linatia moyo kwa Taasisi mbalimbali na Watu binafsi kuunga mkono juhudi hizo.
“Kwenye ujenzi wa bweni hili kwanza nitahakikisha litakamilika kwa viwango vizuri kwasababu najua bweni hili limepewa jina la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hivyo nitahakikisha linakamilika na hata kuanza kuweka vitu vinavyostahili ndani ya bweni hilo kama vitanda, viti, meza n.k hivyo nitahakikisha kwa kushirikiana jengo hilo litakamilika ili kusiwe na shida hii tena”
Akisoma risala mbele ya Mgeni rasmi Salim Abri Asas, Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Iringa Asunta Nombo amesema Chuo hicho kinakabiliwa na changamoto ya malazi ikiwemo ukosefu wa mabweni ya kutosha “Chuo kinapokea Wanafunzi wengi na tayari ujenzi wa bweni umeanza na umaliziaji unagharimu zaidi ya Tsh. milioni 35 na bweni likikamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua Wanafunzi wengi”
Akiongea wakati wa sherehe hizo za ukaribisho wa Wanafunzi wapya waliojiunga na Chuo hicho katika kozi mbalimbali, Asas amesema Serikali kwa upande wake inafanya kazi kubwa katika Sekta ya Elimu jambo ambalo linatia moyo kwa Taasisi mbalimbali na Watu binafsi kuunga mkono juhudi hizo.
“Kwenye ujenzi wa bweni hili kwanza nitahakikisha litakamilika kwa viwango vizuri kwasababu najua bweni hili limepewa jina la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hivyo nitahakikisha linakamilika na hata kuanza kuweka vitu vinavyostahili ndani ya bweni hilo kama vitanda, viti, meza n.k hivyo nitahakikisha kwa kushirikiana jengo hilo litakamilika ili kusiwe na shida hii tena”