Mkuu wa Shule ya Sekondari Nyiendo wilayani Bunda jitafakari kama kiti kinakutosha

Mjukuu wa kigogo

JF-Expert Member
Sep 19, 2023
201
437
God is Good ndio salamu yako maarufu unayoitumia wakati wa kufungua vikao vya shule utafikiri ulizaliwa altareni!Dalili zako za kufeli zilianza mapema sana na bado unaendelea tu kufeli japo uongozi wa juu pengine unakuonea huruma.

1. Baada ya taarifa za awali kuonyesha mwalimu wa kiume anayefundisha somo la kiswahili kutolewa mtandaoni kwamba huwa hafundishi ulimuita haraka na kumweleza asaini daftari la mahudhurio kwa siku zote ambazo hakuwepo(compensations)ili hata wakifika wakaguzi apate kunusurika.Na Kwa uhakika lengo lenu lilifanikiwa!Mwalimu huyu amekuwa na kawaida ya kukaa nje ya kituo Kwa muda mrefu kwa visingizio vingi.Mwalimu huyu amekuwa na kawaida ya kila akifika huwa ana kawaida ya kukupoza.Baadhi ni kama kununua mbuzi na soda ili walimu wakae pamoja.Pia ni mzuri sana wa kujenga hoja vikaoni. Kwa wanaomjua huyu mtu ni kama panya kuuma na kupuliza!Fanyeni utafiti kuthibitisha hili.

2. Unakumbuka mwalimu huyu huyu alichangia sana kuondoka kwa mwalimu ibrahimu mwakio aliyekuwa anajitolea shuleni.Ilibainika mwl husika alikuwa kamtengenezea Mwakio mtego wa kutembea na Mwanafunzi ili ashikwe fumanizi.Bahati nzuri mwalimu alistukia huo mtego baada ya kuelezwa each&everything na mwanafunzi husika. Ofisi yako ilishughulika na hili japo walimu husika waliishi kwa uadui kwa muda mrefu.

3. Mkuu wa shule jumatano mlikaa kikao lakini mmoja wapo wa wanamtandao wako ambaye ndie katibu wa kikao bila aibu alitamka hadharani "Mimi siyo tu chawa wa Mkuu mimi ni chawa pro max".Aliongea hayo huku unamtazama tu!Kilichoshangaza ni pale alipokuomba uanze kuwalipa pesa za zawadi walimu wenye madai!Sasa hatujui yeye ni nani mpaka akuelekeze!

4. Wakati unaanzisha wazo la hostel ulishirikisha walimu kwenye kikao ila kwenye usimamizi ulisimamia kila kitu,hatimaye mpango wa hostel ukawa umejifia kifo cha mende rasmi.Na Kuna mwalimu mmoja (Kwa sasa ni mkuu wa shule)ambaye alikuwa na utaratibu wa kufundisha JUMAMOSI aliwahi kulalamika anasumbuliwa sana na wanafunzi wa hostel kumuomba mia tano mia tano za sukari toka Kwa hao wanafunzi wa hostel mpaka ikawa kero akaona isiwe shida akaacha kufundisha weekend.Kwani uongo?Sasa kama bajeti ilipigwa ilikuwaje watoto waishi maisha magumu mpaka kuwa omba omba na wengine kurudi makwao?

5. Mwl mmoja kutoka idara ya taaluma ni mchapakazi sana ila ukiingia nae mgogoro au kumkosoa tu, shule itakuwa chungu sana kwako.Nitatoa Mfano.Miaka kadhaa iliyopita alikuwa na tuhuma ya kutembea na mwalimu mmoja waliyekuwa ofisi moja.(Mwalimu kashahamia butiama)Mme wa huyu madame aliwahi kufika shuleni akiwa na sime,ni Mungu tu alisaidia yasitokee ya kutokea.Sasa huyo mme wa mtu alisoma na walimu wawili wanaofundisha Nyiendo,hali hii ilipelekea mtaaluma kuwachukia sana zaidi ya sana kwamba ndio wanaopeleka taarifa hizo.(Walikuwa hawasalimiani)Suala hili liligharimu vikao viwili au zaidi.Kuisha kwa suala hili ni pale tu mwenye mke alipomuuliza mkewe unabaki bunda au unaenda butiama?No Butiama,no Ndoa!Mke akasalimu amri. Leo kulikuwa na kikao cha kupiga kura kubaini mhusika lakini tangu awali ilishajulikana atatajwa nani kuhusika na kuleta taarifa JF (Mtajwa ni wale open minded vikaoni) wa .Hii wiki nzima idara ya taaluma wameunganisha nguvu na wapambe wa mama ili kumkomesha!Ilikuwa ni mkakati maalum ambao uliratibiwa vizuri!

6. Huyo mliyempigia kura inaeleweka wazi ataishi maisha magumu sana ikiwemo kupelekwa bush kama alivyodai mtaaluma kikaoni Majuzi,kwamba atapelekwa chingulubila.Kiufupi atapitia kwenye tanuru la moto!Hii pia iwe funzo Kwa mnaokosoa viongozi badala kukubali tu au kukaa kimya kikaoni na kusubiri kupiga makofi!

7. Kikao cha Majuzi pia ulitumia muda mwingi kumkejeli mtangulizi wako Mr.Erasto Arende kama vile hakuitengeneza shule,Arende kwa Nyiendo ni kama Nyerere na Uhuru wa Tanganyika!Hata cheti cha pongezi,Certicate of recognition shule ilikipata chini ya utawala wake!Please mpe heshima yake!

8. Mwalimu wako mmoja alipata tatizo la kuhukumiwa jela.Familia yake ikayumba na kuamua kwenda kuishi ukweni.Mtoto wake wa kike ambaye alikuwa "A-material" aliwalilia sana viongozi wa shule mmsaidie ili abaki asome Nyiendo ahitimu vizuri mkamkataa!Unaishi pale pale shuleni ulishindwa hata kuishi nae?Kama mkuu wa kituo ukaruhusu kupoteza division one nzuri ya binti kizembe kabisa!Kweli God is Good!Huyu Binti akiyumba si atawalilia pia nyie?

Hakuna anayehitaji nafasi yako ila nakushauri yafuatayo kabla jahazi halijazama.....!

1. Kuna mwalimu smart sana hapo shuleni anaitwa Bazalaki Biseko(japo pia hapo awali wewe na ofisi ya taaluma mlikwaruzana nae sana japo mlikaa mkayamaliza).Mfanye huyu mama awe mshauri wako mkuu.Huyu mama ni dhahabu japo hamjastuka!Hana makando kando.Huyu ni Mcha Mungu,acha kuzungukwa na wavaa pensi mtaani!Unamuacha mtu wa maadili unaruhusu kuzungukwa na waenda club watakushauri nini zaidi ya kukufarakanisha na walimu wako?Huyu atakusaidia sana!

2. Mara Moja Moja kwenye posho Yako ya mwezi unatoa hata 100,000 kuwasapoti part time teachers!Wanahangaika sana na kudhalilika!Wanaishi tu Kwa kudra za Mungu hawana wa kuwapambania!Pia punguza kuwa unasifu sifu kundi lako kwenye vikao ili kuwananga wengine!

It's me mjukuu wa kigogo....
Stay tuned for next episode next time
 
Kwa hiyo unadhani ukileta huku ndio utapata suluhu wewe mwalimu? Kama huendani na itikadi za mkuu wako wa shule si uhame au uache kazi?
 
Hii itasaidia nini? kwamba utapanda daraja kutoka 2014 umepanda mara 1 tu, maisha ni magumu kwa walimu kwakweli, naomba serikali kuwaingiza wenza wa walimu pia kwenye orodha ya wanufaika wastaafu hii itasaidia mwalimu kupiga kazi kwa bidii na kupunguza umbea mahala pakazi
 
Hapa kuna mawili, inawezekana unayosema ni kweli na pili inawezekana ni majungu kama kawaida ya wafanyakazi huko maofisini.

Ili kuweka mambo sawa, wewe na huyo mwalimu mkutanishwe na mamlaka husika.
 
Katika sehemu ya kazi ni kawaida kutofautiana sbb kila mtu ana mitazamo yake ni vizuri huu ujumbe ungeufikisha kwa muhusika (mkuu wa shule) kupitia hvyo vikao vya staff au utafute mtu labda mzee mwenzake mkuu wa shule mwenye hekima ili amfikishie ujumbe huu
 
safi sana wapi? mkuda tu huyu.. na wewe ni mwalimu eti?
Mkuda nini?? Ukuda kuongea ukweli wake??

Uongozi makini huanzia ngazi za chini, mtu akifichua uovu ngazi ya chini mnakopata ulaji nyie mkuda, mtu akifichua uovu ngazi za juu serikalini ni shujaa, shenztype.
 
God is Good ndio salamu yako maarufu unayoitumia wakati wa kufungua vikao vya shule utafikiri ulizaliwa altareni!Dalili zako za kufeli zilianza mapema sana na bado unaendelea tu kufeli japo uongozi wa juu pengine unakuonea huruma.

1. Baada ya taarifa za awali kuonyesha mwalimu wa kiume anayefundisha somo la kiswahili kutolewa mtandaoni kwamba huwa hafundishi ulimuita haraka na kumweleza asaini daftari la mahudhurio kwa siku zote ambazo hakuwepo(compensations)ili hata wakifika wakaguzi apate kunusurika.Na Kwa uhakika lengo lenu lilifanikiwa!Mwalimu huyu amekuwa na kawaida ya kukaa nje ya kituo Kwa muda mrefu kwa visingizio vingi.Mwalimu huyu amekuwa na kawaida ya kila akifika huwa ana kawaida ya kukupoza.Baadhi ni kama kununua mbuzi na soda ili walimu wakae pamoja.Pia ni mzuri sana wa kujenga hoja vikaoni. Kwa wanaomjua huyu mtu ni kama panya kuuma na kupuliza!Fanyeni utafiti kuthibitisha hili.

2. Unakumbuka mwalimu huyu huyu alichangia sana kuondoka kwa mwalimu ibrahimu mwakio aliyekuwa anajitolea shuleni.Ilibainika mwl husika alikuwa kamtengenezea Mwakio mtego wa kutembea na Mwanafunzi ili ashikwe fumanizi.Bahati nzuri mwalimu alistukia huo mtego baada ya kuelezwa each&everything na mwanafunzi husika. Ofisi yako ilishughulika na hili japo walimu husika waliishi kwa uadui kwa muda mrefu.

3. Mkuu wa shule jumatano mlikaa kikao lakini mmoja wapo wa wanamtandao wako ambaye ndie katibu wa kikao bila aibu alitamka hadharani "Mimi siyo tu chawa wa Mkuu mimi ni chawa pro max".Aliongea hayo huku unamtazama tu!Kilichoshangaza ni pale alipokuomba uanze kuwalipa pesa za zawadi walimu wenye madai!Sasa hatujui yeye ni nani mpaka akuelekeze!

4. Wakati unaanzisha wazo la hostel ulishirikisha walimu kwenye kikao ila kwenye usimamizi ulisimamia kila kitu,hatimaye mpango wa hostel ukawa umejifia kifo cha mende rasmi.Na Kuna mwalimu mmoja (Kwa sasa ni mkuu wa shule)ambaye alikuwa na utaratibu wa kufundisha JUMAMOSI aliwahi kulalamika anasumbuliwa sana na wanafunzi wa hostel kumuomba mia tano mia tano za sukari toka Kwa hao wanafunzi wa hostel mpaka ikawa kero akaona isiwe shida akaacha kufundisha weekend.Kwani uongo?Sasa kama bajeti ilipigwa ilikuwaje watoto waishi maisha magumu mpaka kuwa omba omba na wengine kurudi makwao?

5. Mwl mmoja kutoka idara ya taaluma ni mchapakazi sana ila ukiingia nae mgogoro au kumkosoa tu, shule itakuwa chungu sana kwako.Nitatoa Mfano.Miaka kadhaa iliyopita alikuwa na tuhuma ya kutembea na mwalimu mmoja waliyekuwa ofisi moja.(Mwalimu kashahamia butiama)Mme wa huyu madame aliwahi kufika shuleni akiwa na sime,ni Mungu tu alisaidia yasitokee ya kutokea.Sasa huyo mme wa mtu alisoma na walimu wawili wanaofundisha Nyiendo,hali hii ilipelekea mtaaluma kuwachukia sana zaidi ya sana kwamba ndio wanaopeleka taarifa hizo.(Walikuwa hawasalimiani)Suala hili liligharimu vikao viwili au zaidi.Kuisha kwa suala hili ni pale tu mwenye mke alipomuuliza mkewe unabaki bunda au unaenda butiama?No Butiama,no Ndoa!Mke akasalimu amri. Leo kulikuwa na kikao cha kupiga kura kubaini mhusika lakini tangu awali ilishajulikana atatajwa nani kuhusika na kuleta taarifa JF (Mtajwa ni wale open minded vikaoni) wa .Hii wiki nzima idara ya taaluma wameunganisha nguvu na wapambe wa mama ili kumkomesha!Ilikuwa ni mkakati maalum ambao uliratibiwa vizuri!

6. Huyo mliyempigia kura inaeleweka wazi ataishi maisha magumu sana ikiwemo kupelekwa bush kama alivyodai mtaaluma kikaoni Majuzi,kwamba atapelekwa chingulubila.Kiufupi atapitia kwenye tanuru la moto!Hii pia iwe funzo Kwa mnaokosoa viongozi badala kukubali tu au kukaa kimya kikaoni na kusubiri kupiga makofi!

7. Kikao cha Majuzi pia ulitumia muda mwingi kumkejeli mtangulizi wako Mr.Erasto Arende kama vile hakuitengeneza shule,Arende kwa Nyiendo ni kama Nyerere na Uhuru wa Tanganyika!Hata cheti cha pongezi,Certicate of recognition shule ilikipata chini ya utawala wake!Please mpe heshima yake!

8. Mwalimu wako mmoja alipata tatizo la kuhukumiwa jela.Familia yake ikayumba na kuamua kwenda kuishi ukweni.Mtoto wake wa kike ambaye alikuwa "A-material" aliwalilia sana viongozi wa shule mmsaidie ili abaki asome Nyiendo ahitimu vizuri mkamkataa!Unaishi pale pale shuleni ulishindwa hata kuishi nae?Kama mkuu wa kituo ukaruhusu kupoteza division one nzuri ya binti kizembe kabisa!Kweli God is Good!Huyu Binti akiyumba si atawalilia pia nyie?

Hakuna anayehitaji nafasi yako ila nakushauri yafuatayo kabla jahazi halijazama.....!

1. Kuna mwalimu smart sana hapo shuleni anaitwa Bazalaki Biseko(japo pia hapo awali wewe na ofisi ya taaluma mlikwaruzana nae sana japo mlikaa mkayamaliza).Mfanye huyu mama awe mshauri wako mkuu.Huyu mama ni dhahabu japo hamjastuka!Hana makando kando.Huyu ni Mcha Mungu,acha kuzungukwa na wavaa pensi mtaani!Unamuacha mtu wa maadili unaruhusu kuzungukwa na waenda club watakushauri nini zaidi ya kukufarakanisha na walimu wako?Huyu atakusaidia sana!

2. Mara Moja Moja kwenye posho Yako ya mwezi unatoa hata 100,000 kuwasapoti part time teachers!Wanahangaika sana na kudhalilika!Wanaishi tu Kwa kudra za Mungu hawana wa kuwapambania!Pia punguza kuwa unasifu sifu kundi lako kwenye vikao ili kuwananga wengine!

It's me mjukuu wa kigogo....
Stay tuned for next episode next time
Walimu wachache wenye akili kama hizi za kwako, ndiyo mnaosababisha walimu wengine wadharauliwe.
 
Back
Top Bottom