Mjukuu wa kigogo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2023
- 201
- 439
Awali wakati tunaanza kulalamikia mambo kadhaa kadhaa hapo shuleni, baadhi waliamini ni chuki binafsi, vita ya kugombania madaraka, watu kukosa fursa, n.k. Lengo letu halikuwa baya. Kwa wafuatiliaji wa mitandao, tumefanya haya kukosoa na kupongeza taasisi mbalimbali nchini, mfano St. Mathew, Elohim, Bugando, Teofilo Kisanji, n.k., kwa hiyo hatujaanza leo!
Tukirudi kwenye hoja ya msingi, tunapenda kuutumia uzi huu kukupongeza kwa dhati kabisa! Tangu tumeripoti changamoto kwenye kituo chako, umebadilika sana! Tunamaanisha mabadiliko chanya! Hata yule bwanyenye aliyekuwa anaonekana shuleni kama kakakuona kaanza kuhudhuria! Makundi shuleni yameanza kufa! Ari ya kufanya kazi iliyopotea imeanza kurudi!
Sasa kuna hili hapa linafuka moshi! Kuna taarifa za wanafunzi wa kike kunyanyaswa kimapenzi na baadhi ya walimu wa kiume! Na wamewataja kwenye vikao vyao! Suala hili tunaomba lifanyiwe kazi haraka lisiachwe maana hapa kuna mambo makuu mawili, inaweza kuwa mbinu ya wanafunzi husika kuwachafua na kuwavunja moyo walimu husika wasiweze kutimiza majukumu yao ipasavyo (hili pia ni kawaida kutokea kwenye taasisi mbalimbali duniani). Ikibainika wanafunzi wananyanyaswa, wahusika wachukuliwe hatua kali, na endapo ni mbinu za wanafunzi, pia wanatakiwa kupewa adhabu kali sana itakayoambatana na kumtambua aliye nyuma yao anayeendesha hii hujuma!
Sasa linaloendana na hilo, ambalo sasa ndio limeleta huu uzi, kuna mwalimu wako mmoja wa kike ambaye inasemekana ana mahusiano na mmoja wa walimu wako wa kiume. Huyu sasa kalikoroga kweli kweli. Kuna mazingira yanaonyesha huyo mwalimu wa kiume anatembea na mwalimu wa kike pamoja na mwanafunzi (anawachanganya). Sasa hili sijui tuliiteje, sijui kughafirika au kupitiwa!
Hivi inaingia akilini mwalimu wa kike kumuita mwanafunzi husika chumba na kumchamba kisa kupambania penzi! Mbaya zaidi wakiwa watatu (mwalimu wa kike, mwalimu wa kiume, na mwanafunzi husika). Zaidi ya masaa matatu walimu mnareconcile conflict ya kimapenzi na mwanafunzi? Hii ni hatari na inashusha hadhi ya mwalimu! Bahati nzuri mwanafunzi mnamjua, na hao walimu wanajulikana! Sasa hivi hii issue ndio story ya wanafunzi! Mkuu waite walimu husika uongee nao!
Jingine ni hili la mwalimu wako mmoja kumnyima maji mwalimu mwenzake mgonjwa ambaye alikuwa anahitaji maji ya kumezea dawa! Kutoa chupa moja ya nusu lita angepungukiwa nini kwenye katoni tatu zilizokuwepo? Wakumbushe walimu wako waache roho mbaya! Haya yafanyie kazi!
Lengo letu ni kujenga na si kubomoa!
Tukirudi kwenye hoja ya msingi, tunapenda kuutumia uzi huu kukupongeza kwa dhati kabisa! Tangu tumeripoti changamoto kwenye kituo chako, umebadilika sana! Tunamaanisha mabadiliko chanya! Hata yule bwanyenye aliyekuwa anaonekana shuleni kama kakakuona kaanza kuhudhuria! Makundi shuleni yameanza kufa! Ari ya kufanya kazi iliyopotea imeanza kurudi!
Sasa kuna hili hapa linafuka moshi! Kuna taarifa za wanafunzi wa kike kunyanyaswa kimapenzi na baadhi ya walimu wa kiume! Na wamewataja kwenye vikao vyao! Suala hili tunaomba lifanyiwe kazi haraka lisiachwe maana hapa kuna mambo makuu mawili, inaweza kuwa mbinu ya wanafunzi husika kuwachafua na kuwavunja moyo walimu husika wasiweze kutimiza majukumu yao ipasavyo (hili pia ni kawaida kutokea kwenye taasisi mbalimbali duniani). Ikibainika wanafunzi wananyanyaswa, wahusika wachukuliwe hatua kali, na endapo ni mbinu za wanafunzi, pia wanatakiwa kupewa adhabu kali sana itakayoambatana na kumtambua aliye nyuma yao anayeendesha hii hujuma!
Sasa linaloendana na hilo, ambalo sasa ndio limeleta huu uzi, kuna mwalimu wako mmoja wa kike ambaye inasemekana ana mahusiano na mmoja wa walimu wako wa kiume. Huyu sasa kalikoroga kweli kweli. Kuna mazingira yanaonyesha huyo mwalimu wa kiume anatembea na mwalimu wa kike pamoja na mwanafunzi (anawachanganya). Sasa hili sijui tuliiteje, sijui kughafirika au kupitiwa!
Hivi inaingia akilini mwalimu wa kike kumuita mwanafunzi husika chumba na kumchamba kisa kupambania penzi! Mbaya zaidi wakiwa watatu (mwalimu wa kike, mwalimu wa kiume, na mwanafunzi husika). Zaidi ya masaa matatu walimu mnareconcile conflict ya kimapenzi na mwanafunzi? Hii ni hatari na inashusha hadhi ya mwalimu! Bahati nzuri mwanafunzi mnamjua, na hao walimu wanajulikana! Sasa hivi hii issue ndio story ya wanafunzi! Mkuu waite walimu husika uongee nao!
Jingine ni hili la mwalimu wako mmoja kumnyima maji mwalimu mwenzake mgonjwa ambaye alikuwa anahitaji maji ya kumezea dawa! Kutoa chupa moja ya nusu lita angepungukiwa nini kwenye katoni tatu zilizokuwepo? Wakumbushe walimu wako waache roho mbaya! Haya yafanyie kazi!
Lengo letu ni kujenga na si kubomoa!