Mke wa mtu ndio anaingia ndani sasa hivi (saa 9:16 usiku)

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,701
9,780
Aisee, kumbe ndoani ni pagumu. Kama mambo yenyewe ndio haya, basi nitaoa mwaka kesho kutwa. Kweli mke wa ndoa unaingia ndani saa 9 usiku ukiwa na rafiki yako mumelewa chakari, plus bodaboda wenu pembeni!!!? Mnategemea mlale kwa nani!!?

Nawasikia wanabisha mlango hili mwanaume awafungulie😂 Na akiwafungulia, basi atakuwa mwanaume jalala. Yaani hii ya leo kali, baba kaamua kuwafungia komeo mama na mtoto, mama karudi saa 9 kakuta lock, binti aliingia saa 5 kakutana na athumani mfupi mlangoni. Hii vita atawapigania Mola baba. Kwa jeuri wamefungua ka glocery ka dharura hapo nje. Ila wanawake ni pasua kichwa kwa kweli
 
Unaripoti matukio kutoka wapi "Livee bila chenga
😂😂 Niko live bila chenga kutoka Daslam Tanzania. Naombeni niwaibieni siri, pameanza kuchangamka huku, naskia skia habari za mwanaume kusaidiwa baadhi ya majukumu na huyo mwanamke, na hii ndo jeuri inayomfanya mwanamke kurudi usiku

Subiri nisogeze vyema antena zangu kwa dirisha

Wanaume tutafute hela. Siogopi chochote, ntawaletea kila kitu
 
😂😂 Niko live bila chenga kutoka Daslam Tanzania. Naombeni niwaibieni siri, pameanza kuchangamka huku, naskia skia habari za mwanaume kusaidiwa baadhi ya majukumu na huyo mwanamke, na hii ndo jeuri inayomfanya kurudi usiku

Subiri nisogeze vyema antena zangu kwa dirisha

Wanaume tutafute hela. Siogopi chochote, ntawaletea kila kitu
Hao ni kenge kama kenge wengine utamlatua mtu makofi
 
Kipara umekipaka mafuta?
Screenshot_20240407_043058_TikTok Lite.jpg


Eti majukumu kwani hela zake au kahongwa?
 
UPDATES: Binti aliyeingia nyumbani saa 5 usiku na kufungiwa mlango na baba yake, mama aibua mazito asubuhi hii kuwa sio mtoto wa huyo baba. Ninyi wanawake ninyi😂

Tunamsubiri arudi kutoka kwa mjumbe. Naripoti nikiwa dirishani kwangu hapa, niko live bila chenga. Tuvideo twa umbea tutafuata muda si mrefu
 
UPDATES: Binti aliyeingia nyumbani saa 5 usiku na kufungiwa mlango na baba yake, mama aibua mazito asubuhi hii kuwa sio mtoto wa huyo baba. Ninyi wanawake ninyi

Tunamsubiri arudi kutoka kwa mjumbe. Naripoti nikiwa dirishani kwangu hapa, niko live bila chenga. Tuvideo twa umbea tutafuata muda si mrefu
Kwahiyo unataka kunambia leo haujalala na umbea wako?
 
Back
Top Bottom