TUSHIRIKISHANE Mjadala wa Mipango ya Maendeleo kwa Jimbo la Nzega

Suala la maji nawapa pongezi sasa hivi mgao wa Maji unaeleweka, vile vile maji yamekuwa ya uhakika tofauti na mwanzoni tunaomba msikate tamaa
 
Nzega nursing college ipo mkuu
Screenshot_2017-02-03-20-24-30.png
Mianman natumia haya mawasiliano yatakuwa msaada tosha kwako karibu nzega
 
Afisa mawasiliano vip mbona umepowa sana umekula mrungura nini si kawaida yako hii habari za maendeleo ya kazi zakozimepungua vipi afisa habari wetu unajua wewe ni jembe basi tu ebu leta mambo hapa bwana
 
Habari zenu wadau, nazi embe na wadau wengine, ukimya wa kutopata habari za maendeleo ya miradi yetu katika jimbo la nzega mjini inatokana na miradi kukamilika katika hatua moja, kwaiyo kipindi hatua nyingine inasubulia kuanza ndio ukimya unatawa hapa katika mijadala yetu na ndio maaana kuna kipindi habari zinakuja kwa wingi sana kipindi ambacho mradi unaanza awamu nyingine

Pengine wadau mtajiuliza Kwanini sasa hatua moja ikikamilika, kunakuwepo na uchelewaji wa kuanza hatua nyingine

Jibu ni kwamba miradi hii inategemea pesa za umma na wahisani kwaiyo upatikanaji wa pesa ajiri ya kuendeleza mradi huwa zina mchakato yake , hivyo basi kipindi hiyo michakato inafanyika ndio ukimya utawala kama huu

Muda si mrefu miradi yetu inaendelea, vile vile wananzega msisite kutumia mjadala huu kuelezea changamoto nyingine za kimaendeleo zilizopo katika halmashauri ya mji wa nzega
 
IMG_20170217_132547.jpg
IMG_20170217_132412.jpg
Kusimamia ukamilishaji wa ujenzi wa kituo kipya cha mabasi Nzega
MAENDELEO YA MPANGO HUU

Kisima cha maji ambacho ujenzi wake ulikuwa unaendelea katika kituo kipya cha mabasi Nzega sagara, umekamilika na kisima kipo tayali ajiri ya matumizi kama picha inavyoonekana.
 
IMG_20170218_104903.jpg
tanki la maji uswilu
IMG_20170218_110243.jpg
Gati la maji maporomoko
IMG_20170218_123003.jpg
Gati la maji ipilili

Haya ni mantaki ambayo yamewekwa katika magati ya maji ambayo upatikanaji wa Maji katika maeneo hayo bado ni wa mgao hivyo basi Siku maji yanatoka, maji huifadhiwa katika matanki hayo, Siku ambayo maeneo hayo wana mgao wa Maji basi wananchi huweza kupata maji katika mantaki hayo hivyo basi kufanya upatikanaji wa Maji uwe kila siku upo, mantaki haya yamewekwa katika Gati la maji maeneo ya maporomoko, Gati la maji eneo la ipilili, na tanki la mwisho limewekwa eneo la uswilu

Hatua hii ni moja ya mpango kazi wa mradi wa Tushirikishane katika jimbo la nzega ambao ni
Kukamilisha mpango wa muda mfupi wa upatikanaji wa Maji safi na salama-Nzega kwa kuongeza mita za ujazo 1300
 
Great, well planned. Kiu ya wadau hapa ni ya muda mrefu ila mnakwenda na ratiba japokuwa changamoto za hapa na pale zipo. Mipango ya muda mrefu ya maendeleo ianze kujadiliwa na iwekewe utaratibu wa implementation hata vizazi vinavyokua hivi sasa wakue na matarajio hayo.
 
IMG_20170218_111926.jpg
Gati la maji eneo la parking
IMG_20170218_114526.jpg
Gati la maji eneo la hospitali ya wilaya nzega mjini.
IMG_20170218_115955.jpg
Gati la maji eneo la kachoma sokoni nzega mjini, Gati hili La kachoma sokoni, Gati la eneo la parking, na Gati la maji eneo la hospitali ya wilaya ni magati ya maji ambayo kwa sasa maji ya napatikana masaa ishirini na nne 24,

Tofauti na awali kabla miundombinu haijafanyiwa marekebisho, magati haya yalikuwa yanatoa maji Mala mbili kwa siku ina maana katika kipindi cha mwezi mmoja maji katika magati haya yalikuwa yanatoka Mala nane tu 8, lakini hivi sasa maji yanatoka kila siku

Upatikanaji wa huduma ya maji kwa uhakika katika mpango wa mda mfupi kwa kurekebisha miundombinu ya maji katika mji wa nzega ni mpango moja kazi mmoja wapo ambao utekelezaji wake unasimamiwa na mradi wa tushirikiane katika jimbo la nzega mjini.
 
Kwa hili suala la kupunguza kero ya maji kiukweli niwape pongezi, sasa hivi ingawa majumbani ni maji ya mgao ila sasa hivi uhakika tena maji yanatoka masafi, mengi haya kwenye magati hayo uhakika wa Maji upo kiukweli kwa hili tuwape pongezi sema muawambie tu idara ya maji wajaribu kuwa wanapita mitaa uko kwani mabomba mengi sasa yamepasuka kwaiyo maji yanavuja na hii nadhani kwa sababu maji yamekuwa mengi hivyo basi miji mingi mabomba yanafungwa kwaiyo maji yanabaki katika mabomba kwaiyo mabomba yaliyokuwa na tatizo ndio haya yanapasuka ila hongera Sana kazi nzuri
 
Yani hali isipobadilika basi hata bustani za mboga mboga japo matuta mawili msimu wa kiangazi tutalima hongereni sana kuhusu hili la maji kiukweli maji kwa sasa yanapatikana
 
cleardot.gif


TARIFA YA KUKAMILISHA MPANGO WA MUDA MFUPI WA UPATIKANAJI MAJI SAFI NA SALAMA -

NZEGA KWA KUONGEZA MITA ZA UJAZO 1300

Tarifa hii itagusia zaidi ukamilishwaji wa ahadi ya maji ya uhakika ambayo ilikuwa moja ya kipaumbele kwenye

mpango kazi wa Mradi wa Tushirikishane katika Jimbo la Nzega. Ahadi hii imekamilika kwa kwa asilimia mia.

Na hatua hii imefikiwa ndani ya miezi saba tu ikiwa ni miezi miwili mapema zaidi ya tarehe iliyopangwa.

Katika ahadi ya maji ya uhakika, lengo liliwekwa kuwa na vyanzo vyenye uwezo wa kuzalisha na kusambaza

mita za ujazo 1300 kwa siku. Matokeo ndani ya miezi saba yanadhihirisha kufanikisha na kuvuka lengo kwani

sasa bwawa la Uchama linasabaza maji safi na salama zaidi ya mita za ujazo 1700 kwa siku.

Kwa mujibu wa makubaliano ya wadau na kalenda ya mradi, mpango kazi huu ulipaswa kukamilika mwezi

Aprili, 2017.

Tarifa ifuatayo ni majumuisho ya ukamilishaji wa ahadi ya maji ya uhakika katika Jimbo la Nzega Mjini.

1. Umefanyika ujenzi wa mfumo wa kuzahisha maji (slow sand filter) wenye uwezo wa kuzahisha maji

kiwango cha kubiki mita za ujazo 1200 kwa siku

2. Umejengwa mfumo wa kusafisha maji kwa kiwango cha kubiki mita za ujazo mita 30-40 kwa saa sawa

na wastani usiopungua kubiki mita za ujazo 600 kwa siku

3. Zimenunuliwa pumps za kuongeza ujazo wa Maji ghafi kwenye mfumo wa kusafisha (70m3/hr)

ingawaje baada ya kuamua kutumia bwawa la Uchama pump ya TUWASA imeendelea kubakia hapo

kwani ina uwezo wa kutosheleza mfumo mzima bila kuegemea bwawa la Uchama (140m3/hr)

4. Zimefugwa (bulk meter) kwa maji ghafi na maji yanayozalishwa ili kujua uwiano wa uzalishaji na

usambazaji

5. Kumerekebishwa mfumo wa pump za kusafirisha maji ili kuwa na uwezekano wa matumizi ya pump

tatu.

6. Umefanyika ukarabati wa tank la maji la parking (135m3) ambalo lilikuwa halitumiki kabisa kwa sasa

linatumika na kufanya Gati la parking kutoa huduma ya maji masaa yote 24.

7. Yamefungwa matanki matatu ya (5000Ltd) kwenye vituo vya maji Ipilili, Maporomoko na Uswilu

8. Vile vile zimenunuliwa pikipiki mbili kwa ajiri ya kusaidia shuguli za uzalishaji na usambazaji maji katika

halmashauri ya mji wa Nzega.
 
Tunashukuru timu nzima ya halmashauri ikishirikiana kwa karibu na mbunge na timu yake, haya ni mambo ya kuendelezwa. you have been a good team big up guys..
 
vipaumbele ambavyo watu wa nzega walichagua vifanyiwe kazi katika mradi wa tushirikiane katika jimbo la nzega mjini ni miongoni mwa vipaumbele ambavyo vinapatikana katika ilani ya Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe Hussein bashe, katika kipindi cha uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Wadau wa maendeleo katika jimbo la nzega mjini walipitia vipaumbele mbali mbali vinavyopatikana katika ilani hiyo ya Mbunge na kuamua kuchagua vipaumbele vinne ambavyo ndio vinafanyia kazi kwa sasa na mradi wa Tushirikishane katika jimbo la nzega mjini.


IMG_20170307_063220_599.jpg
 
Back
Top Bottom