Mhandisi awa mganga mkuu wa wilaya Shinyanga!!

aliye waambia 'District Medical Officer' = Mkuu wa Idara ya Afya ni nani?
 
aliye waambia 'District Medical Officer' = Mkuu wa Idara ya Afya ni nani?

Nziku, idara ya afya ina nyanja mbali mbali sawa lakini "DMO" anayezungumziwa na mwandishi anatakiwa kuwa na taaluma ya udaktari wa binadamu, sio wa falsafa au utaalamu mwingine wa sekta ya afya. Wananchi watakapotambua haki zao na wanasheria watakapohamia mahospitalini ndio umuhimu wa hizi allocation za kazi na maadili ya kazi utakapoonekana.
 
Nziku, idara ya afya ina nyanja mbali mbali sawa lakini "DMO" anayezungumziwa na mwandishi anatakiwa kuwa na taaluma ya udaktari wa binadamu, sio wa falsafa au utaalamu mwingine wa sekta ya afya. Wananchi watakapotambua haki zao na wanasheria watakapohamia mahospitalini ndio umuhimu wa hizi allocation za kazi na maadili ya kazi utakapoonekana.

Mkuu huyo mwandishi amekosea kama nilivyosema pale awali, naye anatatizo juu ya swali hilo hapo juu. Mhandisi wa maji taka haja kaimu nafasi ya DMO bali Mkuu wa idara ya Afya. Hivyo DMO yupo kama walivyo DHO na Afisa ustawi wa jamii wa wilaya. Nimekwisha sema hapo juu kuwa hizo ni section au vitengo katika idara ya afya. Mwandishi amechanganya DMO na Mkuu wa Idara ya Afya kama unavyochanganya wewe.

Huyo Bwana haendi kukaa hospitali bali anakaa katika ofisi ya Mkuu wa Idara ya Afya. Nimejitahidi sana kuliweka wazi hili kwa kuonyesha idara zingine pia.
 
1. Hawa waganga wakuu wa Mikoa\manispaa na Wiyaya bora waongezewe posho watibu hospitalini.. Tz tunao kama 150 na ushee wakati mahospitali hayana madaktari! Kwani wamesomea kazi za Utawala au kutibu na kuokoa maisha ya watu?

2. Utawala wa Afya Mikoani\Wilayani ni kazi ya Health Administrators ambao kwa sasa Mzumbe hutoa degree!

3. Kwa nchi maskini kama Tz- tunatumia raslimali watu vibaya!
 
Nziku,

Haya hapa chini ni maneno ya mhusika aliyekaimishwa nafasi ya DMO (District Medical Officer) na siyo Mkuu wa Idara ya Afya.

Thadeo alipoulizwa kuhusu suala hilo alikiri kwamba hana taaluma ya udaktari, lakini alikanusha kwamba amepewa nafasi ya kukaimu nafasi hiyo kwa makosa. "Ni kweli mimi si daktari.

Nilikaimishwa ofisi hii baada ya daktari aliyekuwepo kwenda masomoni na kabla ya kurudi akafariki dunia akiwa huko na baada ya hapo nikaendelea kuwa DMO kwa sababu nina taaluma ya usafishaji 'cleanliness' na hii ilitokana na utaratibu wa ofisi hii kuwa na vitengo viwili ambavyo ni kitengo cha kinga na tiba ambalo ndilo eneo la daktari na eneo jingine ni la usafishaji ambalo ndilo eneo langu, hivyo mimi nikawa kama msimamizi wa masuala ya usafi na si masuala ya kinga na tiba," alisema Thadeo na kuongeza

Ninafikiria kwamba kinachoongelewa ni post ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya na siyo Mkuu wa Idara ya Afya. In fact kwa uelewa wangu, kila halmashauri huwa ina Bwana/Bibi Afya wa Halmashauri Wilaya/Mji/Manispaa na pia huwa inakuwa na Mganga Mkuu, tatizo ambalo ninaliona sasa ni kwamba nahisi DMO ni post ya ulaji ama ni post ambayo iko above Mkuu wa Idara ya Afya.

Huwezi kuwa Medical Officer wakati huna taaluma ya Medicine, kwa hiyo hata utetezi wake hauna mashiko. Amekiri kwamba anakaimu nafasi ya DMO wakati yeye siyo mtu medicine. Idara ya Afya iko broad na hivyo yeyote anaweza kuishika (bwana/bibi afya, medical officer, sanitation engineer, na wengine walio kwenye hilo eneo). Lakini eneo la tiba/mganga huwezi kumkaimisha mtu wa nje ya medicine, hilo ni kosa na hapo ni sawa na kucheza na afya za binadam.
 
Huyu si ameshikilia kwa muda tu hadi hapo mwenye taaluma hiyo atakapofika,au vipi?

Sishangai hili kwa nchi yetu. Kama mnakumbuka mtoto wa darasa la saba alishwahi kushika nafasi ya daktari cum nurse wa kijiji maeneo ya kaskazini mwa Tanzania. Suala ni je waliconsult wizara kuomba mtu wa kwenda kukaimu hiyo nafasi nyeti? Afy za watanzania zilishawekwa rehani siku nyingi . we unafikiri kwa nini viongozi wetu ukimbilia kwenda kutibiwa nje kukwepa hizi ajira za kujuana zaidi kuliko fani?
 
Mkuu Keil, na haya maelezo ya Meya umeyasoma?

[QUOTEAkizungumzia suala hilo, Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mstahiki Hassan Mwendapole alisema kwamba, Thadeo alishika nafasi hiyo kwa sababu ndiye pekee mwenye elimu ya chuo kikuu katika idara ya afya ya Manispaa hiyo.

Alisema akiwa mwajiri wa Thadeo, anafahamu kwamba hana taaluma ya udaktari, bali ya afya ya mazingira na kwa nafasi hiyo aliyonayo katika manispaa hiyo ni ya utawala na si matibabu.

"Ni kweli huyo bwana hana taaluma ya afya na wala si daktari, bali ana taaluma ya afya ya mazingira na ni mtu pekee mwenye elimu ya chuo kikuu katika idara ya afya, hivyo tuliamua tumpe nafasi hiyo kwa sababu nafasi kama hiyo haiwezi kushikwa na mtu asiyekuwa na elimu ya chuo kikuu," alisema Mwendapole.
[/QUOTE]

Pia huyo Bwana amesema kuwa yeye anafanya kazi za utawala (ie Mkuu wa Idara) na siyo kazi za Kitabibu, na ameongeza kwamba kazi za kitabibu wanafanya madaktari yeye anachokifanya ni kuwa karibu nao kama mtawala.
Meya ameweka wazi kwamba kanuni za Tanzania nafasi hiyo inatakiwa kushikwa na mtumishi mwenye degree sasa madaktari waliopo hawana degree hivyo hawawezi kuwa wakuu wa idara! panua mtazamo wako kwa kusoma maelezo yangu mengine juu ya idara zingine za halmashauri.

Wakuu lazima tukubali kuwa tatizo la Rais kuitwa Nyerere lipo pale pale. Kwakuwa DMO alikuwa Mkuu wa Idara na huyu Mhandisi wa usafi kajiita DMO. Its our problem. Utakwenda Halmashauri nyingi tu utamkuta land surveyor anajiita Town Planner kwakuwa Mkuu wa idara aliyepita alikuwa Town Planner.
 
Nziku,

Majibu ya Meya bado sijaridhika nayo, najua unajua vizuri sifa za mganga mkuu ziko wazi meya ameshindwa kuwasiliana na mkoa au hata wizara kupata mtu wa kuja kukaimu hiyo nafasi. jamaa huyo anaweza kukaimu kwa kipindi fulani dhen kuna suala la kuwa confirmed kuwa mganga mkuu kasheshe hapo. Tuwe makini na utendaji wetu, ni sawa na kumpa mtu cheo cha kukaimu urubani mkuu, wakati yeye ni injinia wa tairi. Kweli tutafika hivi? Mimi hapo ni mala 100 kumpa mtu aliye na elimu ya mganga msaidizi ambaye anaweza kudeal na majanga.
 
Nziku,

Majibu ya Meya bado sijaridhika nayo, najua unajua vizuri sifa za mganga mkuu ziko wazi meya ameshindwa kuwasiliana na mkoa au hata wizara kupata mtu wa kuja kukaimu hiyo nafasi. jamaa huyo anaweza kukaimu kwa kipindi fulani dhen kuna suala la kuwa confirmed kuwa mganga mkuu kasheshe hapo. Tuwe makini na utendaji wetu, ni sawa na kumpa mtu cheo cha kukaimu urubani mkuu, wakati yeye ni injinia wa tairi. Kweli tutafika hivi? Mimi hapo ni mala 100 kumpa mtu aliye na elimu ya mganga msaidizi ambaye anaweza kudeal na majanga.

anyway Mkuu Shadow, ninasema ninachokijua kwani nimeshawahikufanyakazi na Serikali za Mitaa kwa miaka mingi tu. Hivyo ninaelewa shida iliyopo katika kutofautisha vyeo vya maofisa na Mkuu wa Idara.

Nimewahi kusoma kwamba Mfumo wa Maboresho wa Serikali za Mitaa utapitiwa upya, mpangilio na majina ya vyeo vya maofisa hasa wakuu wa idara ili uwe mmoja kwa taifa zima. Sijui kwasasa mfumo huo ulishafanyika au bado.
 
anyway Mkuu Shadow, ninasema ninachokijua kwani nimeshawahikufanyakazi na Serikali za Mitaa kwa miaka mingi tu. Hivyo ninaelewa shida iliyopo katika kutofautisha vyeo vya maofisa na Mkuu wa Idara.

Nimewahi kusoma kwamba Mfumo wa Maboresho wa Serikali za Mitaa utapitiwa upya, mpangilio na majina ya vyeo vya maofisa hasa wakuu wa idara ili uwe mmoja kwa taifa zima. Sijui kwasasa mfumo huo ulishafanyika au bado.

asante mkuu nziku kwa maelezo yako. Happy Holidays!
 
Sio suala la kushikiria kwa muda utashangaaaaaaaaaaaaa atamaliza mwaka miaka.
Alafu ata kama ni utawala ni lazima awe Dr ili aweze kuendana na mahitaji ya wenzake otherwise wenzake watataka iki yeye atasema mbona sioni kama kina umuhimu.
Chukua mhasibu akawaongoze maingeneer utaona mziki wake.
Si lazima ila ni vyema uongoze watu ambao mnaoana kiprofessional so that u can all be in the same wavelength interms of problem solving,setting goals,team work etc

Mkuu Njowepo
Mimi nadhani acha akaimu hata milele. Kama sheria ya kukaimu ipo, inajulikana na wanaojua wanafaa kuchukua hiyo nafasi wanajishaua/ wanasubiri wabembelezwe/wanogopa kulogwa/kupiga kelele sheria inapindishwa, tutafanyaje? Tanzania hakuna serikali, kitu cha msingi ni kuunda mfumo wa mtu mmoja mmoja kukemea upindishwaji wa sheria mpaka waliolala wafie usingizini maana hawataamka.
 
naona shinyanga wanapewa mhandisi kuwa daktari wa mkoa, mkurugenzi aliye shindwa kazi ilala wao, matokeo ya elimu ya msingi kuwa mwisho wao, na kuwa pigia kura mafisadi wao, kuuziwa shule ya green sijui nini wao, kuibiwa madini, wao, kuwekewa reli ya kifisadi wao, kiwanda cha nyama kisichofanya kazi wao. kweli shinyanga itaingia/imeingia katika karne ya 21 kwa mwendo mdundo.
 
Sijaona tatizo hapa ..au mi ni kihiyo? kupewa nafasi ya utawala hakuhitaji uwe na taaluma ya hicho kitengo unachotawala.

Anyway magazeti naona yanataka kuuza tu.

Mods: Vipi hii ikienda kwenye habari mchanganyiko?
 
Jamani pia tuna tatizo la Madaktari wetu wenye Degree kutokuwa tayari kwenda huko Wilayani...Vijana wote wanataka kuwa DSM wafyatue Maisha faster faster...au wakae ktk Mikoa ambao imeendelea kiasi au access ya kuja kila weekend ipo...Kazi ya Kujenga nchi si ndogo...!!!!
 
sawa kabisa Mkuu Masatu, tupo ukurasa mmoja hapa kuna mtu ananyatia cheo hicho anashindwa kukitafuta kwa taaluma na uzoefu sasa anatumia media.

Hapana...

Mbona tunazungukazunguka..? Unasema kuna mtu anakinyatia cheo ila anachafua hali ya hewa kwa kukosa taaluma na uzoefu? Sasa sanitary engineer ndo ana taaluma husika?
 
mwandishi huyu wa Mwananchi hajui kabisa mfumo wa Serikali za Mitaa ulivyo. Hivi nani aliye mwambia kwamba Mkuu wa idara ya afya lazima awe daktari? Katika idara ya afya kuna Madaktari, Ma-Bwana afya, Ma-afisa ustawi wa jamii, wahandisi wa usawi (sanitation engineers). Wote hawa wanahaki sawa kuwa wakuu wa idara endapo elimu yao na uzoefu unaruhusu.

Sambamba na idara ya afya ni hivyo hivyo kwa idara zingine kama vile Ujenzi. Kuna wahandisi wa majengo (Arctects), mitambo (mechanical), bara bara na halmashauri zingine kuna mhandisi wa maji. Yeyote kati ya hawa anweza kuwa Mhandisi wa wilaya.

The same way kwenye idara ya Mipango miji, kuna Ma-afisa mipango miji, Ma-afisa ardhi, Wadhamini (valuers), ma-surveyor na Ma-afisa misitu/mazingira. Pia yeyote anaweza kuwa Mkuu wa Idara ya Mipango Miji.

Idara ya kilimo kuna Ma-daktari wa mifugo, Ma-afisa kilimo, Ma-land use planners au soil specialists, ma-afisa ushirika nk. Idara ya elimu kuna afisa elimu taaluma, takwimu, elimu ya watu wazima, utamaduni nk.

Tofauti ipo katika idara za fedha, utumishi, vitengo vya mwanasheria na mkaguzi wa ndani kwani hawa taaluma yao ni moja.

Nadhani unaongelea kitu tofauti.. Hizi unazozizungumzia ni habari kuhusu clusters za TAMISEMI kiidara..this has nothing to do with the kadhia under discussion..Tuwe makini na michango yetu..
 
at post #001,

Mganga Mkuu wa Wilaya lazima awe mtu wa fani husika...kwa sababu itakuwa ni ajabu watu wenye fani yao wapo halafu top wao awe mtu ambaye hana idea na anachokisimamia..Hii ni ajabu ya jua kuchomoza magharibi..!! Only in bongo things like this happens..
 
Mkuu Mtindiowaubongo, let me make a summary.
Katika Idara ya afya kuna maafisa/wataalamu wafuatao:-
Ma-daktari, Ma- Bw./Bi. Afya, Ma- afisa ustawi wa jamii na Ma-sanitary engineer.
Katika hizo clusters kuna wakuu wa section wafuatao
1. Daktari wa Wilaya (Mkuu wa section ya Tiba)
2. Bw./ Bi./ Afisa afya wa Wilaya (Mkuu wa section ya Kinga)
3. Afisa Ustawi wa Jamii wa wilaya (Mkuu wa section ya ustawi wa jamii) na
4. District sanitation engineer (Mkuu wa sanitation section)

Kati ya hawa wakuu wa section yeyote anaweza kuwa Mkuu wa idara ya afya. Sasa kwa Shinyanga nafasi hiyo inakaimiwa na sanitation engineer.

Tatizo hapa ni kasumba yetu ya kumwita Rais ni Nyerere. Kwamba huyu jamaa, mwandishi wa habari husika, wewe nk, mnamwita Mkuu wa idara ya afya ni DMO. Hili ni tatizo kwa nchi nzima na idara zote. Ndo maana maboresho ya Serikali za mitaa yalitaka ku-harmonize hilo. sijui wamefikia wapi.

Wewe kama unataka uuhakika wasiliana na watu wa Shinyanga wakueleze vizuri kama huyo Mhandisi ni Mkuu wa section ya Tiba au mkuu wa idara. Wenyeji wa Shinyanga tunalijua hilo vizuri.

anyway, nimejitahidi sana kulieleza kwa upana na mifano mingi tu. Ni vema pia kupitia makala za Karugendo juu ya Mfumo wa Serikali za Mitaa. Otherwise, pitia ripoti za Halmashauri mbalimbali na uwahoji wahusika.

You can't fool me that a sanitary engineer awe subordinate milele katika idara yake tena awe chini ya watu wasio na degree na yeye anadegree eti kwasababu tu kitengo chake kipo ndani ya idara ya afya yenye madaktari au Medical Officers na Assistants wao. LOL
 
Mkuu Mtindiowaubongo, let me make a summary.
Katika Idara ya afya kuna maafisa/wataalamu wafuatao:-
Ma-daktari, Ma- Bw./Bi. Afya, Ma- afisa ustawi wa jamii na Ma-sanitary engineer.
Katika hizo clusters kuna wakuu wa section wafuatao
1. Daktari wa Wilaya (Mkuu wa section ya Tiba)
2. Bw./ Bi./ Afisa afya wa Wilaya (Mkuu wa section ya Kinga)
3. Afisa Ustawi wa Jamii wa wilaya (Mkuu wa section ya ustawi wa jamii) na
4. District sanitation engineer (Mkuu wa sanitation section)

Kati ya hawa wakuu wa section yeyote anaweza kuwa Mkuu wa idara ya afya. Sasa kwa Shinyanga nafasi hiyo inakaimiwa na sanitation engineer.

Tatizo hapa ni kasumba yetu ya kumwita Rais ni Nyerere. Kwamba huyu jamaa, mwandishi wa habari husika, wewe nk, mnamwita Mkuu wa idara ya afya ni DMO. Hili ni tatizo kwa nchi nzima na idara zote. Ndo maana maboresho ya Serikali za mitaa yalitaka ku-harmonize hilo. sijui wamefikia wapi.

Wewe kama unataka uuhakika wasiliana na watu wa Shinyanga wakueleze vizuri kama huyo Mhandisi ni Mkuu wa section ya Tiba au mkuu wa idara. Wenyeji wa Shinyanga tunalijua hilo vizuri.

anyway, nimejitahidi sana kulieleza kwa upana na mifano mingi tu. Ni vema pia kupitia makala za Karugendo juu ya Mfumo wa Serikali za Mitaa. Otherwise, pitia ripoti za Halmashauri mbalimbali na uwahoji wahusika.

You can't fool me that a sanitary engineer awe subordinate milele katika idara yake tena awe chini ya watu wasio na degree na yeye anadegree eti kwasababu tu kitengo chake kipo ndani ya idara ya afya yenye madaktari au Medical Officers na Assistants wao. LOL

Labda nikuulize, Mganga Mkuu wa Manispaa ni mkuu wa cluster au idara..tutaendelea kuanzia hapo..
 
Labda nikuulize, Mganga Mkuu wa Manispaa ni mkuu wa cluster au idara..tutaendelea kuanzia hapo..

Mkuu nikisema Halmashauri ninamaanisha Jiji, Manispaa, wilaya, na miji midogo. Mfumo katika Halmashauri ni mmoja tofauti ni majina tu ya cluster.

Kwa kujibu swali lako: Mganga Mkuu wa manispaa ni Mkuu wa section ya tiba yaani ni daktari kwa kifupi MMO au MMOH.

Katika Manispaa nyingi daktari pia ndiye Mkuu wa idara (hili ndo linalokuchanganya) na Shinyanga ilikuwa hivyo kabla ya huyo daktari kwenda masomoni kisha kufariki.

Isipokuwa kama daktari atakuwa na elimu ndogo (hana degree) hawezi kuwa Mkuu wa idara. Pia itaangaliwa ni nani mwenye sifa zaidi za kielimu na uzoefu kati ya wale wakuu wa section (wewe unaita cluster).
 
Back
Top Bottom