Mgomo wa madaktari na kiburi cha watawala wetu, nani anaumia?

Pinda amekamilisha mkutano na waandishi wa habari hivi punde na meseji ya kubwa kwa madaktari ni kuwaambia kuwa serikali haiwezekani kushinikizwa na madaktari na kuwafukuza mawaziri Mponda na Nkya. Hivyo, kama wanataka kugoma, wagome tu

Huyo tushamzoea.
Kesho utasikia ''milango ya majadiliano iko wazi''
 
kuna tetesi serikali imeomba madakitari 350 kutoka india na 300 kutoka china wanaweza wakaingia muda wowote kuanzia kesho.

pinda is smacking hard ball stuff, huh?

basi, wasisahau kuwaandalia vifuatavyo:

1. bullet proof outfit
2. boardguards
3. waje na vyakula vyao na wajipikie wenyewe
4. wasisahau kuja na wanawake zao + wanaume zao kwa ajili ya chakula cha usiku

kama noma na iwe noma!
 
Mwenye nguvu akiwa na tamaa ya pesa, watu huwatesa
Maisha hayana mrejesho , huwezi fanyia mchezo
Naliona kama kichekesho, mnalotenda ninyi wawili. ….. Mnyamahodzo wa Paluhengo

Irene Sanga katika wimbo wa Mjomba aliandika,
“Taifa liwapo na huzuni lazima wote tufunge mikanda kiunoni ili matanga yaishe upesi,
Majanga yanapozidi kimo mioyo ya wanadamu huota kutu
Hizo ni salam zangu kwako eeehh!
Pepo hazina sifa ila pawapo Jehanamu, uzuri ni kipimo cha ubaya,
Kwani kiumbe chenye uhai na mauti huongozwa na tamaa
Salam zangu kwako eeehh!”

Haji Mponda na Lucy Nkya;
Tafakarini pesa na cheo utakachopewa kinathamani gani ya kuuzidi uhai wa mtu aliopewa mara moja tu na Mwenyezi Mungu.
Ni vyeo vingapi mlivyowahi kuvishika hadi leo kuwa hapo mlipo? Mmewahi kufa mara ngapi hadi kufika hapo mlipo?
Itawafaidia nini watu wakifa kwa kutokuwa na busara na kuifanya mioyo yenu kujaa kiburi?

Kiburi
Kinapofusha macho kwa aliyenacho
Inaumiza moyo kwa wanaotendwa
Baraka hukimbiziwa mbali
Uangamivu hukaribishwa ghafla
Radhi haifanyi makao
Ighh! Huwapata wadharau makuzi

Haji Ponda
Itakufaidia nini Haji Ponda watoto wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Haji Ponda wanawake wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Haji Ponda vijana wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Haji Ponda wazee wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?

Lucy Nkya
Itakufaidia nini Lucy Nkya watoto wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Lucy Nkya wanawake wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Lucy Nkya vijana wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?
Itakufaidia nini Lucy Nkya wazee wakifa kwasababu umekataa kujiuzuru?

Ni kweli wataokufa si watoto wenu, siyo wake/waume zenu, siyo wazazi wenu wala siyo ndugu zenu.
Haiwaumi kwasababu siyo wakwenu.
Kiburi ndivyo kinavyofundisha.
Mtawatupia lawama wengine, ndiyo ni madaktari. Mtaonyesha ufundi wa kujitetea
Nayo ni tabia ya mwenye kiburi

Ni nini maana yake hii?
Imezoeleka kusikia kipindi cha uchaguzi na kuunda baraza la mawaziri wagombea na wabunge kwenda Bagamoyo, Mahenge na kwingineko kufanya ushirikina ili kupata ushindi na vyeo pia. Mshirikina na mchawi wote lao moja, furaha yao huwa kuu wanapomuua au kumwangamiza mshindani. Huruma mioyoni mwao hamna. Mwatuaminisha kwamba madaraka mliyopata ni kwa kumwaga damu za watu (mchawi akionja damu au nyama ya mtu haachi) na sasa mwataka kula nyingi zaidi na kunywa nyingi zaidi. Halafu mtakapotosheka kwa awamu hii ndipo muachie madaraka kwa kusema tunajiuzuru sasa. Kweli mmefikia hapo?

Mmefikia hapo!! Kwanini kutenda kama Dracula?
Mchana mnakuwa wenzetu, usiku adui zetu.
Mchana tunawapa maji yetu, usiku mnakunywa damu zetu.
Mchana tunawapa chakula chetu, usiku mnakula nyama zetu
 
Pinda akumbuke wananchi wanauwezo wakumfukuza rais licha ya waziri eg egypt,tunisia,libya

Mkuu hii kitu ndio ina dalili ya kutokea bongo,maana nipo mkoani kuna radio wameweka mjadala juu mgomo wa madaktari imagine karibu 80 ya wananchi wanaopiga simu na ku sms wanaiponda serikali na wanaunga mkono madai ya madaktari
 
ni ngumu kuwaelewa hawa watu in the gvt.what did pinda expect from the drz?hivi anakumbuka aloyasema 2wks ago?hivi aliona kuna need ya kuwaondoa mpönda na nkya au alikurupuka kuongea tu akifikiri anaongea na watu wasio na akili?Pinda kashajipambanua kama 'a lier' (refer to ishu ya lema bungeni,then posho ya wabunge etc..).je,tuamini anachokisema leo?kikwete hatokuja na jibu lingine kesho?'kwa mtazamo wa pinda,(nachelea kuuita wa serikali maana hii serikali kila mtu anajisemea kivyake) bora wagonjwa wanyanyasike,wafe kuliko mponda na nkya kuondoka kwa shinikizo!!!what a big joke!!
 
Huu mgomo ni wa kisiasa zaidi kuliko kudai masilahi. Nina waomba vijana wetu madktari, achaneni na mambo ya kisiasa kabisa. Taaluma yenu si siasa bali ni kutibu. Msikubali kabisa kutumiwa na wanasiasa.

Za mbayuwayu changanya na za kwako
 

Mkuu kwani Serikali ni nani? Au PM anaposema Serikali haiwezi kufanya kazi kwa shinikizo ka Madaktari kuwafukuza kazi hao Mawaziri, hiyo Serikali ndiyo ipi? Ni mtu mmoja au ni Baraza la Mawaziri au ni Rais au ni PM? Ni nini hiki kinachoitwa Serikali? Je ni kweli Serikali nzima ndiyo inakuwa na kigugumizi ktk suala hili la Madaktari? Labda nikukumbushe kitu kidogo, tu kwa uelewawangu mdogo, Serikali ni Wananchi, kwa hiyo wakiamua leo Serikali itoke madarakani wanaweza kufanya hivyo. Kuna mifano mingi ambayo haihitaji hata kuitaja. Hembu fungueni macho na akili zenu.

Mtu aliye elimika na mwenye utamjua tu kwa kauli zake,endelea kuelimisha wale vichwa maji mkuu,big up sana,well said!
 
Nakuunga mkono mheshimiwa Pinda, wacha madaktari wagome.

Kwani wakigoma anayeumia nani? si babu zao, bibi zao, shangazi zao ,kaka zao wa Namtumbo, Nachingwea, Tandahimba, Kilindi na Kahama?
.......baada ya hapo, ama kweli we nunda!!!!!!!!!
 
Wacha niwahi jioni hii nikang'oe jino kwani kesho wakigoma itakuwa imekula kwangu. Madaktari hawana mchezo ukizingatia ajira yao ni Hot-Cake kwa nchi jirani. Duh! Tunakufa huku viongozi tuliowachagua ili watuongoze wanachekelea!
 
Kweli Mungu yu mwema alinena na Watanzania kupitia mafuta ya Petrol na sasa nauli zimekuwa kubwa kiasi kwamba usafiri tu wa kwenda mjini na kurudi inakaribia 1000 au elfu na zaidi ila sisi Mitanzania(sorry Watanzania) bado hatujafunguka macho kwa kupanda mafuta vyakula vimepanda matunda yamepanda kwa sasa buku tatu ukiacha nyumbani kwa ajili ya chakula cha mchana na usiku haitoshi kabisa na bado watu wa DSM tumelala.

Yule kijana,bibi,babu na baba wa kijijini hawajali hali hii wao CCM tu leo ni CCM hii inatakakutuua wagonjwa Muhimbili halafu tutabaki tukisema kazi ya Mungu haina Makosa. Ndugu zangu waalimu wa vijijini na mijini wanaoteseka na ndio wasimamizi wakuu wa vituo vya uchaguzi bado wanatusaliti baada ya wao kuongea na wale wazee kuweza kuwabadilisha utakuta wanatumiwa kuiba kura.

Kweli Mungu yu mwema ameaumua kutumia madaktari na Waziri mkuu kuweza kuendelea kufikisha ujumbe jinsi gani serikali ya Chama Cha Mapinduzi inavyotutesa kwa kunyang'anya maliasili zetu ambazo yeye alitupa bure kwa sababu zake azijuazo ili tuweze kuishi maisha mema na Bora zaidi. Mungu hapendi watu wadhulumiwe na wachache na ndio maana kipindi hiki kaamua kutumia Sekta inayogusa zaidi binadamu kwani alitumia Richmond akaona wengi hawana umeme hivyo halitawagusa, akaja mafuta lengo likiwa chakula kikipanda bei tutashtuka lakini wapi wengi wetu tukajifanya hatuna magari. Sasa kagusa sekta Muhimu afya kwamba itatuuma sana tutakapoona ndugu, Jamaa na marafiki zetu wanaaga dunia kwa kumkosa daktari. Baba niliyeamini haambiwi kitu kuhusu CCM naona kabadilika sana hataki hata kuisikia sababu ya kundokewa na mjomba kipindi cha mgomo

Kweli Mungu yu mwema na kwa hili bado hatutafunguka macho na vichwa vyetu

wenu aandikaye kwa masikitiko kwa kufiwa na mjomba wake kwa sababu ya Serikali ya CCM iliyosababisha mgomo wa madaktari
Kasimba123
 
raia wasio na hatia wanaoendelea kupoteza maisha ama kwa hakika watakua chimbuko la ukombozi wa nchi yetu.
 
Jamani mimi kidogo nashindwa kuelewa hapa.kama madai ya msingi ya madaktari kwa maana ya maslahi yao na maboresho ya mazingira yao ya kazi yote serikali imekubali kuyashughulikia sasa kwani hao Dr Mponda na Nkya wanawapunguzia nini madaktari wakiendelea kuwa mawaziri?Wakumbuke kuwa kwa umuhimu wao katika jamii hapa hawaikomeshi serikali bali wanatukomesha watanzania tusiokuwana kosa lolote!!
 
huyu mzee ni wa kupewa polonium maana ana kauli za kipumbafuuuuu sana.....yaani mawazo yake ni kama mpagazi
 
Huwa nachanganyikiwa sana kwamba ni wakati gani nitenganishe shughuli za serikali na siasa. Ninavyojua mimi hivi vitu havitengani. Waziri Mkuu Pinda (kiongozi wa serikali) aliwahaidi Madaktari (watumishi wa serikali) kuwa atashirikiana na Rais (kiongozi wa serikali) kuwawajibisha mawaziri wa Afya (viongozi wa serikali), kwa kufanya uzembe na kuleta maafa na hasara nyingine kwa wananchi (wenye serikali). Sasa hapa naona watu wanachangia kuwa Madaktari waachane na siasa na wasigome. Kwani wanafanya siasa na nani? Sisi wananchi ndiyo waamuzi wakubwa sasa maana tuliowapa dhamana wameshindwa kututumikia na tumeshapoteza imani. Kwani hata hii KATIBA mbovu inasemaje kuhusu kuiwajibisha serikali yetu pindi inaposhindwa kutusimamia. Kwani hatuna haki ya kuandamana, ama kupiga kelele mataifa ya nje watusaidie kabla hatujadhurika zaidi?. Hapa naona Serikali inatunishiana misuli na madaktari wakati waathirika wakubwa ni sisi wananchi. Natafuta jinsi ya kulianzisha hili na kweli ilitokea hadi panakucha kesho hakuna ufumbuzi wowote wa kunusuru haya itabidi tuanze vyovyote vile. Sasa nimeshafikia hatua kwamba liwalo na liwe lakini nisifanyiwe majaribio kwenye haki zangu za msingi.
 
Back
Top Bottom